Nitakufa Mara Ya Pili

Nitakufa Mara Ya Pili

Poa sana!
Dah cjakuona sehem tunazokutanaga!

Hahahah
Kule Leo Sijatembelea sana,Niko Hapa Na Majiwe Yangu
Kupunguziana Stress Za Wiki Nzima!

Karibu Sana GOOGLE!
 
wivu utakuuu.povu linakutoka mwache mwenzako asimlie.roho mbaya hiyo.majigo endelea mwaya

Heheheh
Mazima Kiongozi Wangu, Nakaza Ndole Mwendo Wa Typ Ni Kutoana Baru Speed 2222.67875
 
Heheheh
Mazima Kiongozi Wangu, Nakaza Ndole Mwendo Wa Typ Ni Kutoana Baru Speed 2222.67875

Jamani, mimi nimekuja haraka nikijua umepost anaza episodi kumbe hola! Khah
 
24--“Mbona kuna wengine wapo katika jumuia ya kanisa na kuonekana wacha Mungu wakubwa ?”
“Hapo ndipo ujue atakayeurithi ufalme wa mbinguni hajazaliwa.”
“Na kwa nini mwalimu amejiingiza kwenye kazi ile?”
“Mmh, kwa kweli sijui, Lakini Shija unajua mwalimu Vene huingia darasani na kufundisha uchi?”
“Uchi?” kauli ile ilinishtua.
“Bila nguo yoyote mwilini huwa kama alivyozaliwa .”
“Mmh, mbona sijamuona.”
“Nasema kama si mchawi au mtaalamu wa mambo hayo huwezi kuona.”
“Wewe huwa unamuona?”
“Ndiyo, hata Helena.”
“Sasa ninyi si watoto wadogo kwa nini anakaa uchi mbele yenu.”
“Shija ulipokuja kwenye ngoma nani ulimuona kavaa nguo kama sio wewe peke yako?”
“Mmh, kweli wachawi hawana aibu.”
“Tena hawajui vibaya , unataka siku moja na wewe umuone?”
“Ndiyo, nitaweza?” “Utamuona, ila nakuomba kitu kimoja usioneshe kushtuka tulia kama hukuona kitu.”
“Mmh, nitaweza?”

“Basi siwezi kukupa dawa ya kumuona.”
“Hapana nitajitahidi.”
“Basi kesho tukikutana shuleni nitakupa dawa ya kumuona mwalimu Vene anavyomwaga radhi.”
“Hakuna tatizo, Sabina muda umekwenda kiza kimeingia na tunaporudi ni mbali, tufanye tuondoke,” nilimshauri Sabina kutokana na kiza kuanza kuingia.
“Hakuna tatizo mpenzi, nakuomba nipo chini ya miguu yako, japo sikupaswa kutoa siri ya wachawi na nikigundulika ni kifo.
Kama utakosa uvumilivu basi kifo changu wewe ndiye utakayesababisha.”
“Sabina moyoni mwangu kuna siri nzito ambayo itaungana na hii ambayo ni nzito yahitaji msaada wa haraka wa kumkomboa kaka yangu.”
“Tusifanye haraka tukikosea tumempoteza au tukimtoa bila kujipanga vilevile tutampoteza.”

Baada ya kukubaliana tulirudi nyumbani wakati huo kiza kilikuwa kimetanda, tulirudi nyumbani njiani nilimuuliza. “Vipi kwenu ukichelewa hugombezwi?”
“Nagombezwa, kwenu vipi?” “Najua kutakuwa msala, kumbe ule ugomvi wetu wa siku ile baba alikasirika na kutaka kunipiga lakini alinikanya nisipigane tena na niwe mtoto mzuri.”

“Sasa utamwambiaje?”
“Nitajua cha kumwambia hilo usihofu kwa mganga hakuishi nyimbo.”
“Mmh, Shija kwa Kiswahili sikuwezi.”
“Tunajifunza tukitumie.”
“Asikubane ukatoa siri, elewa utakuwa umenimaliza,”
Sabina alizidi kunisisitiza.
“Siwezi kufanya hivyo na hata akinibana nitamdanganya lakini ulilonieleza litabakia moyoni mwangu.”

Tulipofika njia panda tuliachana wakati huo kiza kilikuwa kimeishaingia, Sabina alielekea kwao na mimi kuelekea kwetu.
Nilipofika nyumbani nilimkuta baba amekaa kwenye kiti chake akivuta sigara.
Nilipomuona nilishtuka kitu ambacho baba alikiona.

”We Shija muda wote huu, unatoka wapi?”
“Nilikwenda kuwinda ndege baba, shikamoo.”
“Marahaba, ndege gani mpaka usiku wote huu, hujachota maji leo huogi?”
“Nitaoga yaliyopo kesho nitachota kabla ya kwenda shule.”
“Shija mwanangu nazungumza nini?
Unafanya nini?”
“Samahani baba.”
“Basi kabadili nguo haraka.”
Niliachana na baba na kukimbia chumbani kwangu kubadili nguo huku nikimshukuru Mungu kutoulizwa maswali magumu. Baada ya kubadili nguo nilikwenda kumsalimia mama aliyekuwa jikoni akipika.
“Shikamoo mama.”
“Marahaba Shija, ulikuwa wapi?”
“Mama nilipitia kuwinda.”
“Mpaka usiku?”
“Leo tu mama.”
”Kuwa makini inaonekana siku hizi utundu umekujaa.”
“Nitajitahidi mama.”
“Basi nenda ukaoge chakula si muda mrefu kitakuwa tayari.”

Nilikwenda kuoga na kusubiri muda wa kula na baada ya kula nilipanda kitandani, usingizi ulikuwa mbali sana. Niliwaza mambo mengi niliyoelezwa na Sabina juu ya matukio ya uchawi yaliyoizingira familia yetu hasa uchu wa kuutaka uhai wangu bila kosa.
Pia ugomvi wa mpaka wa shamba uliozua mtafaruku mkubwa wa watu kutoana roho. Nilijikuta nikitokwa na machozi kila nilipomkumbuka kaka yangu na mambo waliyomfanyia kwa kisingizio cha bangi. Nilijiuliza nitafanya nini mtoto mdogo kama mimi, mdomo wangu ulikuwa na makufuli mawili.
La mzee Manoni na la Sabina ambalo ni zito lililoufanya moyo wangu kutetemeka kwa hofu.


Msiondoke Inaendelea...
 
Majigo kuchelewa kwako kupost Shauri yako. Na wewe utakufa, bora uharakishe. Hahahahaa..hadithi zinatufunza mengi sana.
 
25--Nilijiuliza maisha ya kaka yangu ya msukule ataishi mpaka lini, na msaada wa Sabina angenisaidia vipi kumtoa kaka yangu katika kifungo cha kuzimu. Uwezo wake kwa kweli ulikuwa mdogo kwani hakuwa na uwezo zaidi ya kuwategemea watu wakubwa . Niliamini msaada wa Sabina ungekuwa na nguvu kama mzee Manoni, uwezekano wa kunisaidia ungekuwa mkubwa sana. Lingine lililoniumiza akili ni kuhusu uhai wangu unaowindwa na kundi dogo la wachawi ambao wapo tayari kuhakikisha wananipoteza katika sura ya dunia. .

Hata kama nilikuwa nimesema kuwa wao ni wachawi , sikuzungumza kwa kuujua huo uchawi zaidi ya kusema kwa hasira tu. Niliwaza mbona mzee Manoni alinielewa hakunipa adhabu yoyote wala kunikanya itakuwa wao, niliamini ule ulikuwa wasiwasi wao tu. Kama jaribio la kumtuma Sabina limeshindikana kwa uwezo wa Mungu bado wasiwasi wangu ulikuwa katika usalama wangu. Bado niliamini msaada mkubwa wa maisha yangu yapo kwa baba yangu. Lakini ningemueleza vipi wakati Sabina kaniomba chonde nisiiseme siri ile ambayo akijulikana yeye kasema basi nitakuwa nimeutoa uhai wake kwa wachawi wa kijijini. Na kukaa kimya nilikuwa nakaribisha matatizo makubwa, wazo la kwenda kumueleza mzee Manoni nililiona linafaa. Lakini bado swali lilikuwa lilelile nikimueleza nilitaka kuuawa na wachawi aliowakataza wasiniue, lazima ataniuliza swali nani kaniambia, nitamwambia nani kaniambia?
Lazima atanitisha na kumtaja Sabina ambaye wasiwasi wangu ningempoteza kutokana na kuwa mtu muhimu sana kwa kipindi kile. Nalo niliamua kulikalia kimya kuongeza ukubwa wa mfupa kooni mwangu, ambao kwangu yalikuwa mateso mazito sana yaliyoniweka katika wakati mgumu.

Suala la mwalimu kufundisha uchi kwa kweli sikukubaliana nalo japo Sabina alinihakikishia kesho yake angeniletea dawa ya kumuona mwalimu Vene akifundisha darasani bila nguo mwilini. Kuhusu kwenda kumuona kaka yangu Luhemeja, nilijiuliza kama nikimuona nitafanya nini?
Nitaweza kuvumilia kumuona akichunga ng’ombe tukijua amekwisha kufa?
Niliamini kabisa mwaka ule ulikuwa wangu, mwaka ambao katika maisha yangu ningeuita mwaka wa maajabu.

Usingizi ulinipata majira ya saa kumi alfajiri baada ya kukesha kwa mawazo na kumsikia jogoo akiwika kuonesha kumekaribia kupambazuka. Asubuhi kama kawaida baba aliniamsha kuwahi shule, niliamka huku macho yakionekana kuvimba kwa usingizi. Nilitoka nje na kukutana na baba ambaye aliniangalia bila kusema kitu kisha alitikisa kichwa. “Shikamoo baba,” nilimsabahi bila kumtazama.
“Marahaba.”

Baada ya kuitikia nilimpita kwenda kunawa, nilipopiga hatua mbili baba aliniita.
“Shija.”
“Naam baba.”
“Una matatizo gani?” Kauli ya baba ilinishtua na kutulia dakika nzima kabla sijamjibu.
“Sina baba.”
“Mbona sikuelewi?”
“Kivipi?”

”Ni muda mrefu nakuchunguza kutokana na mwenendo wako, muda mwingi ukiwa peke yako unakuwa hapo kimawazo, huna furaha niliyoizoea mara nyingi umekuwa ukinikimbia na kukaa peke yako. Siku za nyuma ulipenda kunidadisi mambo mengi lakini sasa imekuwa tofauti, una tatizo gani?”
“Hapana baba nipo sawa.”
“Hapana niambie mwanangu inavyoonekana siku hizi usiku hulali.”
“Nalala baba.”
“Hapana hii ni mara ya tano nakuona ukiamka macho yamevimba kwa kukosa usingizi kitu kinachosababisha ulale darasani.”

Mmh, maneno ya baba yalinifanya niwe katika wakati mgumu wa kumjibu. Kutokana na maneno yake ya kunifanyia uchunguzi ilionesha kabisa amegundua vitu vingi kwangu bila mwenyewe kujua. Niliona kuna maswali ataniuliza lazima ataninasa pengine akijua namdanganya anaweza hata kunipiga. Mara nyingi baba alinionya nijiepushe na uongo kwani ni adui mkubwa wa maisha yangu. Nikiwa bado natafakari cha kumwambia, alinisogelea na kusema huku akinishika kichwani.
“Shija mwanangu najua kifo cha kaka yako kimekuchanganya kwa kiasi kikubwa , umepoteza uchangamfu najua jinsi gani ulivyokuwa ukimpenda. Kifo ni kitu ambacho mwanadamu hawezi kukikwepa . Wote tutakufa la muhimu tukubaliane na kilichotokea, kaka yako amekufa la muhimu tuzidi kumuombea kwa Mungu apate makazi mema huko mbinguni.”

Sikuamini kama baba atanivua zigo la mawazo la kumjibu juu ya maswali yake mazito. Kunieleza vile nilishusha pumzi baada ya baba kuamini mabadiliko yangu yanatokana na kifo cha kaka.
“Nashukuru baba kwa kunifariji.”

“Basi kanawe uwahi shule.” Nilikwenda kunawa na kubadili nguo kisha nilipitia vitu vyangu na kuwahi namba shule, njiani nilikutana na Sabina aliyeonesha alikuwa akinisubiri aliponiona alitabasamu huku akionesha kunishangaa.
“Shija una tatizo?”
“Hapana.”
“Au jana baba yako amekupiga?”
“Walaa, kwa nini unaniuliza hivyo ?””
“Unaonesha una tatizo.” “Mbona nipo sawa.” “Hapana Shija mtu yeyote akikuona atajua una tatizo uso umekuwa mzito unaonesha hukulala kabisa.”


Msiondoke,Inaendelea....
 
26--“Ni kweli.”
“Tatizo nini?”
”Mawazo.”
“Ya nini tena?”
“Kwa yote uliyonieleza jana.” “Shija utaharibu kila kitu, kukueleza umekuwa hivyo je, ukiona itakuwaje?”
“Sidhani kuna mtu atahoji kwa nini sikulala.”
“Basi pole sana.”
“Asante, vipi umeleta?” nilimwuliza.
“Nimeleta, lakini utaweza? Unanitia wasiwasi .” “Nitaweza,” nilimhakikishia.

“Shija usifanye vituko darasani mwalimu akikugundua vita yenu itakuwa kubwa na pengine kuniponza mimi.”
“Nitajitahidi nina imani nitaweza.”
“Mmh, haya.”
Tulikuwa ndiyo tunaingia eneo la shule na kengele ya namba iligongwa, tulikimbilia kuhesabu namba kisha kila mmoja alielekea kwenye eneo lake kufanya usafi.

Baada ya usafi kengele ya msitarini ili iligongwa, tulijumuika pamoja. Wakati tunaelekea mstarini Sabina alinifuata na kunipa kikaratasi kidogo na kunieleza kwa sauti ya chini.
“Ndani kuna unga mweupe, paka kidogo chini ya macho yote utaona ya kuyaona.”
Sikumjibu nilipokea na kukimbilia msitarini, baada ya ukaguzi tuliingia darasani.
Kama kawaida walimu waliingia kwenye vipindi, kipindi cha mwalimu Vene kilikuwa cha tatu cha saa tatu na dakika ishirini mpaka saa nne wakati wa mapumziko.

Kama kawaida aliingia darasani kwa macho yangu nilimuona amevaa nguo, nilimuona Sabina akinitazama. Nilijifanya simuoni, nilitulia kama hakuna kitu chochote. Kutokana na hofu yangu sikutaka kuiweka haraka kwa kuhofia kugundulika. Baada ya kuandika na kutuachia kazi, wakati anajiandaa kutoka kwa kutuambia tukusanye daftari, niliutoa ule unga uliokuwa kwenye karatasi na kujipaka kidogo chini ya macho.

Mmh, kweli ukishangaa ya Musa utayaona ya Firauni, sikuamini niliyoyaona mbele yangu. Kama isingekuwa kujipaka dawa na kuelezwa nitakayoyaona ningepiga kelele.
Mwalimu Vene alikuwa kama alivyozaliwa mkono wa kushoto alikuwa amejifunga hirizi kubwa nyeusi, mkononi alikuwa ameshikilia kitu kama kidole cha mtu. Shingoni alikuwa na kamba iliyokuwa imebeba kichwa cha mtoto mdogo.

Moyo ulitetemeka na hofu ilinijaa, nilimuomba Mungu kimoyomoyo mwalimu aondoke mapema. Wasiwasi wangu Sabina aliuona na yeye nilimuona akiingiwa wasiwasi , pengine alidhani naweza kupiga kelele za mshtuko au mwalimu Vene kugundua nimemjua yupo uchi. Ili kukwepana na kile kilichokuwa mbele yangu, sikuangalia mbele tena mpaka mwalimu alipotoka. Kengele ya mapumziko ndiyo iliyoniokoa, baada ya kutoka nilihisi kichwa kizito, nilichoshukuru Sabina muda wote alikuwa karibu yangu kufuatilia kila kilichokifanya .Wakati wanafunzi wote wanatoka alikuja na kuniuliza. “Vipi Shija?”
“Kichwa,” nilimjibu huku nikishika mkono kichwani.
“Vipi umeona?”
“Ndi..yo..o..o.”
“Pole sana, kanawe na maji utarudi katika hali ya kawaida.”
“Kaniletee, naweza kukutana naye nje.”
“Si nilikuambia sasa unamuogopa.”
“Hapana hii kufuru.”
“Shija vipo vitu vingi utaviona yataka uwe na moyo mgumu.”
“Mmh, kweli yataka moyo wa ujasiri.”

Sabina alinifuatia maji na kunawa uso, baada ya kunawa nilirudi kwenye hali ya kawaida. Pamoja na kurudiwa na hali ya kawaida, bado mazingira ya shule sikuyaelewa .
Nilikwenda kuomba ruhusa kurudi nyumbani kusingizia naumwa, kwa vile haikuwa tabia yangu waliniruhusu. Sabina alijitolea kunisindikiza japo wanafunzi walimwita wifi na wengine shemeji.
Nilijua nini alichokifanya Sabina alinisindikiza hadi nyumbani.
Njiani aliniuliza ninavyojisikia .
“Vipi Shija unajisikiaje?”
“Hata sijielewi.”
“Si nilikuambia?”
“Ni kweli, lakini ni mshtuko tu kwa leo nisingeweza kusoma tena labda kesho.”
“Basi kuna dawa nitakuletea ukiinywa itakutia ujasiri kila kitu atakachokiona utakiona cha kawaida.

Sitakupeleka kwa kaka yako mpaka nikupatie hiyo dawa.” “Nitashukuru.”
“Wacha nikufuatie sasa hivi kwa vile wazazi wapo shamba.”
Sabina aliondoka na kuniacha nikiwa nimejipumzisha na yeye kukimbia kwao, baada ya robo saa alirudi.
Alikuwa na dawa nyeusi ya unga ambayo niliikoroga kwenye maji na kuinywa kisha alinipa kipande kidogo cha ngozi sikujua ya mnyama gani ambayo alinieleza hata yeye hakujua ni ya mnyama gani.


Shija ameanza kufumbuliwa mambo kwa kuona na macho nini kitakacho mtokea? Kuyajua yote
Husiondoke Tafadhari.....
 
27--Ajabu baada ya Sabina kuondoka nilijikuta narudi kwenye hali ya kawaida maumivu ya kichwa yalitoweka . Niliamua kujilaza kwa vile sikuwa na la kufanya muda ule, usingizi nao haukuchelewa kunichukua. Sauti ya Sabina ilinishtua usingizini na kunifanya ninyanyuke kitandani. Nilipotoka nje nilimkuta Sabina akiwa katika mavazi ya nyumbani kuonesha amekwishatoka shule.
“Vipi umeishatoka shule?”
“Mmh, mbona muda mrefu.”
“Kwani muda huu ni saa ngapi?”
“Karibia saa kumi na moja.” Nilikwenda jikoni na kuchukua viazi ambavyo nilikula na Sabina kisha tuliondoka pamoja kupitia njia ya kwenye vichaka na mashamba ya watu kuelekea ziwani kwenda kumuona kaka yangu.

Pamoja na Sabina kunihakikishia kumuona bado sikuamini. Ilitokana na kushuhudia kifo cha kaka yangu hata mazishi yake, muda ulikuwa umekwenda sana ilikuwa inakimbilia saa kumi na mbili na nuru ya anga ilianza kutoweka taratibu kuukaribisha usiku. Tulivuka maeneo ya watu na kuingia kwenye mashamba ya mpunga. Baada ya kuvuka mashamba ya mpunga tuliingia kwenye matete maji yaliyokuwa mengi na kuingia mpaka ziwani kando ya ziwa, woga ulianza kunitawala kutokana na eneo lile kuwa tulivu huku sauti za mawimbi zikisikika.

“Sabina huogopi humu tunaweza kukutana na wadudu wakali?”
“Shija usihofu kitu, niamini.
” Baada ya kunieleza vile tuliendelea kukatiza kwenye matete maji kwa kuyakanyaga maji yaliyokuwa yakitufikia magotini.
Nilishangazwa na ujasiri wa Sabina japo msichana mdogo.
Tulitembea kwenye matete maji kwa muda huku tukikwaruzwa na majani yake.

Baada ya kuyavuka matete hayo tuliingia kwenye maji na nguo zetu ambayo yalikuwa yanatufikia kifuani. Tulitembea ndani ya maji pembeni ya matete kuelekea mbele. Nilijiuliza tunaelekea wapi, Sabina alikuwa mbele yangu akitembea kuelekea mbele bila hofu yoyote , nijikuta naingiwa na wasiwasi na kujiuliza mbona maji yanazidi kwenda juu kwa vile yalikuwa ya tumbo na hatimaye yakafika mabegani.

“Sabina...,” nilimwita.
“Shiiii,” aliweka kidole mdomoni kuonesha ninyamaze.
Nilinyamaza kimya nisijue kwa nini kaniambia vile, baada ya kunyamaza kimya Sabina alisimama na kunishika mkono kunivutia kwake . Tulikuwa tumeyavuka matete na kufika kwenye majani yaliyokuwa yameota pembeni ya ziwa. Sabina alisita kidogo na kuonesha wasiwasi ; nilijiuliza kaona nini. Mara alinishika kichwani na kunizamisha chini, woga ulinitawala lakini nilitiii amri na kuzama chini ya maji.

Tulitulia kwa muda kisha tuliibuka juu, nilitaka kuhoji. Lakini nilipotaka kusema kitu alinishika mdomo nisizungumze lolote. Kila alilofanya aliangalia mbele kama kaona kitu lakini mimi sikuona lolote. Mara alinishika mkono na kunivuta hadi nyuma ya matete maji, alijifuta maji yaliyokuwa yakimtiririka usoni na kusema...


Husiondoke Tafadhari....!
 
Da we jamaa yaani leo nimeshinda na sim, imeisha charge nimechomeka kwenye umeme huku nasubili story iendelee. Umenikamata hakika
 
28--“Unajua nini Shija?”
“Hata sijui.”
“Wakati tunafika eneo lile mama Helena alikuwepo na shoga zake, niliogopa anaweza kutuona. Kama angeniona mimi asingekuwa na tatizo ila angekuona wewe na mazingira haya ungeleta utata mkubwa.”
“Mbona asikuwaona?”
“Walikuwa kikazi usingewaona, sijakupaka dawa kwa kuhofia hali ambayo ungeiona lazima ungepagawa, pengine ungepiga kelele.”
“Sasa kama ulijua hivyo kwa nini ulinileta huku?”
”Lazima kila kitu utaona tu mpenzi wangu.”
“Kwa hiyo?”
”Turudi tena.”
“Si watatuona?”
”Walikuwa wakiaga ili waondoke, sasa hivi najua hawapo.”

Muda ulikuwa unazidi kuyoyoma kigiza nacho kilizidi kuchukua nafasi yake, ubaridi ndani ya maji nao ulizidi kuongezeka. Ujasiri wa Sabina ulinifanya nami nifiche hofu yangu japo niliamini maeneo tuliyokuwepo hata kama tungetokewa na tatizo asingekuwepo wa kutusaidia.
Alitoa kikaratasi kilichokuwa na unga mweusi ambao haukuwa mgeni tena kwangu, alichovya kidole na kunipaka chini ya macho.

Baada ya kujipaka tulirudi tena taratibu, tulipokaribia lile eneo nilishangaa kuona kuna ng’ombe wengi waliokuwa wakila majani na wengine wakinywa maji pembeni ya ziwa. Nilijiona kama nipo dunia nyingine tofauti na ya mwanzo, nikiwa bado nipo katika dimbwi la mawazo. Sabina alininong’oneza.
“Umeona mabadiliko yoyote ?”
“Ndiyo.”
“Umeona nini?”
“Ng’ombe wengi.”
“Mchungaji umemuona?”
“Hataa.”

Mara nilimuona kijana mmoja akiwa katika vazi la rubega la kaniki, nilipomuangalia vizuri nilimtambua. Alikuwa akiswaga ng’ombe wasiingie ndani ya maji.
“Ha! Huyu si Samweli tuliyekuwa tunasoma naye?” nilisema kwa sauti kidogo.
Alikuwa ni mwanafunzi mwenzetu aliyegombana na Helena na kumuapia ataona, na siku ya pili Samweli alianguka akicheza na kupoteza maisha.

Kila mmoja alijua Samweli amekufa baada ya kuhudhuria mazishi yake. Japo baada ya mazishi maneno yalienea kuwa Samweli hakufa. Pamoja na maneno ya chinichini, hakukuwa na ukweli wowote , siku zilikatika watu tukaamini kweli Samweli amekufa. Nilibakia nimetokwa na macho pima.

Je nini kitatokea?


Inaendelea....
 
Da we jamaa yaani leo nimeshinda na sim, imeisha charge nimechomeka kwenye umeme huku nasubili story iendelee. Umenikamata hakika

Pamoja Kiongozi, Mpaka Kisimu Kibast
Nashusha Madude Tu!
 
endelea mkuu wangu,wanakuombea mabaya ukute ndio wanashnda humu kusoma story yako.uko juuu
 
Back
Top Bottom