Nitakufa Mara Ya Pili

Nitakufa Mara Ya Pili

9--Nilihamishia mawazo yangu shule kuwaza masomo hasa somo la jiografia ambalo jana yake nilikosa maswali mengi tofauti na nilivyojiamini kwa kuyaona maswali mepesi. Sikutaka kuumiza akili yangu kuwaza nilioyaona na kukutana nayo, kwani niliamini hata kama nisingekatazwa bado hakuna mtu angeniamini na kuniona mtu niliyekuwa nikiona ndoto na vitu visivyo na ukweli. Kingine nilichokiogopa ni kuonekana mchawi wa ukweli kuyasema mambo ya usiku watu wamelala.

Nilitembea kwa mwendo wa kawaida kwa kuamini bado sijachelewa kutokana na wanafunzi wengi kuonekana kutembea bila wasiwasi wowote . Nilipokaribia uwanja wa shule nilianza kusikia mlio wa ngoma niliyoisikia usiku iliyokuwa ikipigwa palepale uwanjani. Lakini nilipokaribia sauti ile ilipotea akilini taratibu na mwisho wake ilipotea kabisa.

Nilifanikiwa kuwahi namba, baada ya kuhesabu namba nilikwenda kwenye eneo langu kufanya usafi na kumwagilia maua. Baada ya usafi ilipigwa kengele na wanafunzi wote tulikusanyika kwa ajili ya usafi, baada ya usafi muda wa kuingia darasani ulipofika tuliingia madarasani. Nilipoingia darasani nilikwenda kukaa kwenye dawati langu. Dawati nililokuwa nakaa lilikuwa la wanafunzi wawili . Kutokana na uwezo wangu darasani, katika dawati nilikuwa nakaa na mtoto wa mwalimu mkuu wa kike. Japo hakuwa na akili sana lakini tulisaidiana japo sehemu kubwa ya masomo alinitegemea mimi.

Ajabu ilikuwa baada ya mwalimu kuingia darasani, tulimsalimia vizuri kama kawaida alituruhusu tukae chini . Baada ya kukaa chini mwalimu wakati anaanza kufundisha somo lake, nilipitiwa na usingizi mzito uliopelekea niote yote niliyoyaota jana yake baada ya kurudi kutoka shuleni baada ya kuamka muda usio wa kawaida. Ilikuwa ndoto nyingine iliyonipeleka tena kwenye ngoma ya wachawi , ilikuwa ajabu ile ngoma haikuwa tena kwenye uwanja wa shule. Ilikuwa chini ya mti mkubwa, ngoma ilikuwa imepamba moto kila mtu kucheza anavyojua . Watu walikimbia na fisi na wengine kupaa na kutua na ungo.

Mara moja sikujua sherehe ile inahusu nini kwa wachawi kufurahi namna ile, kitu kingine kilichonishtua kwenye njozi yangu ilikuwa kumuona mmoja wa walimu wetu naye akiwa anacheza ngoma ile huku vumbi likiwa kubwa sana. Kutokana na vumbi kubwa kutimka nilijikuta nikiingiwa na vumbi mdomoni na puani na kusababisha nikohoe mfululizo. Kumbe kukohoa kwangu ndiko kulikowashtua wanafunzi na mwalimu darasani kuwa nimelala, hata mwalimu alipokuja bado nilikuwa nimelala sijitambui. Kila walivyoniita sikuweza kuwasikia , nililala juu ya dawati huku nikiendelea kukohoa sana. Walinichukua na kunitoa nje na kuniweka chini ya mti wenye hewa. Mwalimu aliwaeleza wanafunzi waliokuwa wamepagawa na hali yangu, waniache nipigwe na upepo huku akiwekwa msichana mmoja pembeni yangu aniangalie.


Itaendelea...
 
Wakuu Eeh...Nitarusha Mpaka Ya Kumi
nyingine Tukutane Kesho Hapa Hapa Kwenye Mtandao Wetu Kipenzi Wa JF!
 
10--Njozi yangu iliendelea hadi kulala na kuamka siku ya pili kwenda shule ndipo niliposhtuka na kujikuta nimelala chini ya mti. Pembeni yangu alikuwepo msichana aliyekuwa amenipa mgongo, kwa vile nilimfahamu nilimwita.
“Leti,” alishtuka na kunikuta nimekaa kitako.
“Haa! Shija!”
“Vipi?”
“Mmh, hata siamini, kwani ulikuwa ukijisikiaje?”
“Kivipi, kwani hapa nimefikaje?”
“Wenyewe tulishtuka tukiwa darasani ulipokohoa mfululizo.
tuliposogea na mwalimu, tulikuona umelala, hujitambui hata tulipokubeba kukutoa nje bado ulikuwa hujitambui.”
“Mungu wangu.”
“Kwani ulipatwa na nini Shija?”
“Hata najua!” Nilikumbuka masharti niliyopewa na mzee Manoni ya kutokusema kitu chochote nilichokiona wala kusikia.
“Pole sana.”
“Asante.”
Tulinyanyuka kuelekea darasani, mwili wote ulikuwa umechoka sana japo ilikuwa ndotoni lakini niliamini kutokana na ngoma ya kichawi niliyocheza.

Nilipoingia darasani wote walishtuka, wakaja kwenye dawati langu kunipa pole huku wakitaka kujua nilipatwa na kitu gani, kwani toka nianze shule sijawahi kutokewa na hali kama ile, si mimi hata wanafunzi wenzangu, hakuna aliyewahi kukumbwa na sakata kama langu. Nikiwa darasani nilipepesa macho kuwatafuta wanafunzi ambao niliwaona kwenye ngoma ya wachawi , nilipowakosa niliuliza.
“Jamani Sabina yupo wapi?”
“Leo hatujamwona.”
“Helena?”
“Mmh, hata yeye leo hajaja shule.”
Majibu yale yalinishtua kidogo kutokana na njozi niliyoota muda mfupi na kukosekana kwa wale wasichana.
“Shija, kwani vipi! Mbona unawaulizia hao?”
“Hata, basi tu, maana wote nimewaona kasoro wao.”

Mwalimu aliyeshuhudia tukio lile aliniita ofisini kwake na kunihoji juu ya mkasa ulionikuta.
“Shija upo sawa?”
“Nipo sawa, ila nahisi uchovu.”
“Jana umelala saa ngapi?”
“Kama kawaida baada ya kula tuliingia chumbani kulala.”
“Saa ngapi?”
“Saa tatu mwalimu.”
“Kweli?”
”Kweli mwalimu.”
“Unaweza kunieleza nini kilikutokea darasani kilichosababisha ulale na kupoteza fahamu?”
Nilitulia kidogo kabla ya kumjibu huku nikiyakumbuka maneno ya mzee Manoni, nilitikisa kichwa kama ishara ya kukataa kuwa, siwezi kumwambia.
“Kweli mwalimu sikumbuki chochote.”
“Ni hali gani ilikutokea kabla ya kupoteza fahamu?”
“Mwalimu kusema kweli wakati unaingia darasani na kutwambia tukae chini, ghafla usingizi mzito ulinijia, kilichoendelea sikijui mpaka nilipojikuta nimelazwa chini ya mti.”
“Ooh, pole sana.”
“Asante.”
“Unasema mwili unajisikiaje?”
“Nimechoka sana, kama nilikuwa nalima.”
“Basi itakubidi urudi nyumbani ukapumzike, lakini usisahau kuwaeleza wazazi wako kilichokutokea, sawa?” “Sawa mwalimu.”
Kabla ya kutoka, nilimuulizia mwalimu yule niliyemwona kwenye ngoma ya wachawi .


Itaendelea...
 
11--“Mmh, aliomba ruhusu toka juzi, lakini kesho atakuwepo, kwani vipi?”
“Hapana, ila sijamwona tokea jana.”
“Kweli upo makini, wanafunzi wengine wapo hawajui nini kinaendelea shuleni.”
Nilitoka ofisini huku walimu wengine wakiniuliza maswali mengi juu ya tukio lile lililowashtua wengi. Kilichonishtua zaidi kilikuwa ni kukosekana kwa wote niliowaona kwenye ngoma ya wachawi .
Nilibaki na maswali mengi, kuna ukweli gani katika njozi zangu na matukio ya kweli. Wengi waliamini huenda nachelewa kulala, niliomba Mungu wote waamini hivyo kuliko tofauti, kwani wangeniweka kwenye wakati mgumu na mzee Manoni.

Baada ya kuniuliza na kuwajibu ya uongo nilirudi nyumbani taratibu huku nikijiuliza kule, wazazi wangu nitaanzaje kuwaeleza kilichonitokea shuleni? Wasiwasi wangu mkubwa ulikuwa kwa baba, kama ningemweleza uongo, akanibana kwa maswali na kujikuta nasema ukweli ambao ungegharimu maisha yangu. Njiani kama kawaida, nilikutana tena na mzee Manoni ambaye sikumwona alipotokea ila ghafla alisimama mbele yangu. Nilishtuka sana na kutaka kutimua mbio, lakini miguu ilikuwa mizito kama imefungwa mawe. Aliniangalia kwa muda bila kuniambia kitu, ikabidi nijifanye natazama chini kwa aibu na woga, mwili ulinitetemeka kwa hofu.
“Shija,” aliniita.
“Abee babu,” nilijikuta nakosea kuitikia kwa woga.
“Shija wewe mtoto wa kiume unaitikiaje hivyo ?”
“Samahani babu, naam.”
“Mbona unatoka shule mapema?”
“Sijisikii vizuri.”
“Kama nilivyokueleza , kila ulichokiona na kukisikia kiache moyoni mwako, sawa?”
“Sawa babu nitafanya hivyo ,” nilimjibu kwa unyenyekevu .
‘Haya kwa heri.”

Niliagana na mzee Manoni, kama kawaida baada ya hatua tatu nilipogeuka sikumwona, kitendo kile kilizidi kunitia hofu moyoni. Sikufanya lolote, nilifika nyumbani na kuingia chumbani kwangu. Kutokana na mwili kuchoka sana nilijitupa kutandani ambako nilishikwa na usingizi mzito sana. Niliota ndoto za kawaida mpaka waliporudi wazazi wetu jioni kutoka shamba ndiyo walioniamsha. Nilifikiria kuwaeleza kilichonitokea, niliogopa vitisho vya mzee Manoni, niliamua kukaa kimya kama hakuna kitu kilichonitokea


Itaendelea Kesho Asubuhi....
 
kuna Jamaa Kani PM Eti Anastress Na Hana kwa Kuziondolea
Wakuu Ninatupia Mbili Za Mwisho Kwa Leo!
 
12--“Vipi mbona umelala,” baba aliniuliza.
“Uchovu tu baba,” nilimjibu kwa kuficha kilichonitokea mchana.
“Mbona umelala na nguo za shule au kesho huendi?”
“Naenda, niliporudi shule nilijilaza kidogo usingizi mzito ukanipitia.”
“Basi nenda kisimani ukachote maji ya kuoga.”
Sikumjibu kitu nilipitia dumu la maji kuelekea kisimani kwa kuhofia baba kuniuliza kitu ambacho angekiona kigeni kwangu. Nilikwenda hadi kisimani na kuchota maji, wakati narudi nilikuwa na mawazo mengi juu ya uamuzi wangu wa kumueleza baba yaliyonitokea shuleni kwa kuhofia kunichimba sana. Nilimuomba Mungu, baba yangu asijue lolote juu ya kilichonitokea shuleni kwa kuamini lazima atataka kujua kwa undani. Hata nikijitahidi kuficha lazima angegundua kitu, kwa vile yeye ni mtu mzima siwezi kumficha au kumdanganya kutokana na kujua vitu vingi.

Nilipofika nyumbani nilikwenda kuoga, wakati huo mama alikuwa jikoni akiandaa chakula cha usiku, usiku ulipofika tulijumuika pamoja kupata chakula cha usiku. Siku ile nilikuwa muoga kupita kiasi baada ya chakula tu, niliingia chumbani kwangu na kupanda kitandani. Nikiwa chumbani nimejilaza, nilishtushwa na sauti ya baba aliyokuwa akiniita huku akiingia chumbani kwangu. Moyo wangu ulishtuka na kujua nilichokificha kimemfikia baba hivyo anataka kujua ukweli.
“Shija!” “Naam baba.”
“Vipi baba unaumwa, mbona leo mapema kitandani wakati muda si mrefu umetoka kulala?”
“Basi tu leo mwili nahisi uchovu.”
“Pengine maralia?”
“Sidhani, nahisi ni uchovu tu.”
“Basi pumzika usiku mwema.”
“Na wewe pia.” Nilishukuru baba aliondoka bila kunidadisi wakati moyoni nilikuwa na wasiwasi wa siri ya shule kumfikia baba.

Nilijilaza kitandani huku nikiwaza vitu ambavyo hunitokea huku nikikatazwa nisimwambie baba. Niliamini kama baba angejua matatizo ninayokumbana nayo angeweza kunisaidia. Nilijiuliza kwa nini mzee Manoni hataki wazazi wangu wajue na wakijua itakuwaje. Swali lingine nilijiuliza kama nikimwambia baba nini kitanitokea, katika habari nilizowahi kusikia juujuu kuhusu wachawi nilielezwa ni watu wabaya wanaoweza kuua na kula nyama. Niliogopa pengine kuitoa siri na kumueleza baba nitauawa na kugeuzwa kitoweo cha wachawi . Kwa kweli nilijikuta kwenye wakati mgumu maishani mwangu, mzigo niliobebeshwa haukulingana na umri wangu. Niliamini walikuwa wakinionea pengine walihofia siri yao kutoka nje, ni kweli ningeweza kuwaeleza wazazi wangu niliyokutana nayo.


Inaendelea...
 
13--Bado wazazi wangu wasingejua nani anayehusika katika uchawi,
kujitokeza kwa mzee Manoni kulijidhihirisha wazi wasiwasi wao pengine nimewajua. Nilimuomba Mungu aniepushe na janga lile kwa kuamini kama wataendelea kunifuata, nitashindwa kusoma vizuri. Usingizi nao haukuchelewa kunichukua baada ya kitu kizito kunipitia na kunifanya nilale usingizi wa pono. Siku ya pili kama kawaida baba aliniamsha kujiandaa kwenda shule, niliamka nikiwa na nguvu kama kawaida. Nilijiandaa kuwahi namba shuleni, niliwahi namba na kufanya usafi kama kawaida. Muda wa kuingia darasani ulipowadia tuliingia. Ajabu siku ile wale wanafunzi niliowaota wakicheza ngoma ya wachawi katika ndoto na nilipoamka sikuwakuta darasani na kuwauliza kama walikuwepo darasani. Hata mwalimu aliyekuwepo kwenye ngoma alikuwepo siku hiyo shule, kila sekunde ya pumzi yangu nilijiona kama sipo katika dunia ya kawaida ambayo naishi peke yangu. Sikutaka kuhoji lolote nilikaa kimya na kuendelea na masomo kama kawaida.

Siku ile nilisoma kama kawaida hakuna kilichonitokea cha ajabu. Jioni ilipofika nikielekea nyumbani, mara nyingi nilipenda kuwinda ndege kila nikitoka shule. Niliacha njia ya kuelekea nyumbani na kuingia vichakani kuwinda ndege, nikiwa katikati ya kichaka, nilisikia sauti ya wale wasichana niliowaota wakicheza ngoma ya wachawi .
“Shija.” Kabla ya kuitika niligeuka kuwaangalia, nilishtuka kuwaona ni wale wale, nilijiuliza wamefuata nini kule porini.
Niliwaitikia huku nikitabasamu kuficha hofu yangu.
“Naam, aah Helena na Sabina,” Helena na Sabina walikuwa wakubwa kwangu kiumri.
“Mbona uko huku peke yako?”
“Nawinda ndege.”
“Eti jana ulituulizia?”
“Eeh, kwani mlikuwa wapi jana?”
“Mmh, nyumbani.”
“Wote?”
“Kwani vipi mbona unauliza hivyo ?”
“Si rahisi wote muwe nyumbani kwa pamoja bila sababu, ikizingatiwa hamkai pamoja.”
“Kwani wewe wasiwasi wako nini?”
“Hakuna tatizo, ila niliwaulizia kama wanafunzi wenzangu.”
“Shija ilianza lini na jana iwe ya pili, ina maana mimi na Sabina ndiyo jana kukosekana kwa pamoja?”
“Tena nasikia sijui ulipitiwa usingizi na kuanza kukohoa na ulipopata fahamu watu wa kwanza tulikuwa sisi.
Tunaomba utueleze ukweli nini kilichokufanya utuulize.
” Helena aliongezea.


Shija ataeleza nini, wenzie wamuelewe?
ITAENDELEA ASUBUHI..
 
Wakuu Mlale Salama
Mola Awalinde Nyote Inshaallah!
 
13--Bado wazazi wangu wasingejua nani anayehusika katika uchawi,
kujitokeza kwa mzee Manoni kulijidhihirisha wazi wasiwasi wao pengine nimewajua. Nilimuomba Mungu aniepushe na janga lile kwa kuamini kama wataendelea kunifuata, nitashindwa kusoma vizuri. Usingizi nao haukuchelewa kunichukua baada ya kitu kizito kunipitia na kunifanya nilale usingizi wa pono. Siku ya pili kama kawaida baba aliniamsha kujiandaa kwenda shule, niliamka nikiwa na nguvu kama kawaida. Nilijiandaa kuwahi namba shuleni, niliwahi namba na kufanya usafi kama kawaida. Muda wa kuingia darasani ulipowadia tuliingia. Ajabu siku ile wale wanafunzi niliowaota wakicheza ngoma ya wachawi katika ndoto na nilipoamka sikuwakuta darasani na kuwauliza kama walikuwepo darasani. Hata mwalimu aliyekuwepo kwenye ngoma alikuwepo siku hiyo shule, kila sekunde ya pumzi yangu nilijiona kama sipo katika dunia ya kawaida ambayo naishi peke yangu. Sikutaka kuhoji lolote nilikaa kimya na kuendelea na masomo kama kawaida.

Siku ile nilisoma kama kawaida hakuna kilichonitokea cha ajabu. Jioni ilipofika nikielekea nyumbani, mara nyingi nilipenda kuwinda ndege kila nikitoka shule. Niliacha njia ya kuelekea nyumbani na kuingia vichakani kuwinda ndege, nikiwa katikati ya kichaka, nilisikia sauti ya wale wasichana niliowaota wakicheza ngoma ya wachawi .
“Shija.” Kabla ya kuitika niligeuka kuwaangalia, nilishtuka kuwaona ni wale wale, nilijiuliza wamefuata nini kule porini.
Niliwaitikia huku nikitabasamu kuficha hofu yangu.
“Naam, aah Helena na Sabina,” Helena na Sabina walikuwa wakubwa kwangu kiumri.
“Mbona uko huku peke yako?”
“Nawinda ndege.”
“Eti jana ulituulizia?”
“Eeh, kwani mlikuwa wapi jana?”
“Mmh, nyumbani.”
“Wote?”
“Kwani vipi mbona unauliza hivyo ?”
“Si rahisi wote muwe nyumbani kwa pamoja bila sababu, ikizingatiwa hamkai pamoja.”
“Kwani wewe wasiwasi wako nini?”
“Hakuna tatizo, ila niliwaulizia kama wanafunzi wenzangu.”
“Shija ilianza lini na jana iwe ya pili, ina maana mimi na Sabina ndiyo jana kukosekana kwa pamoja?”
“Tena nasikia sijui ulipitiwa usingizi na kuanza kukohoa na ulipopata fahamu watu wa kwanza tulikuwa sisi.
Tunaomba utueleze ukweli nini kilichokufanya utuulize.
” Helena aliongezea.


Shija ataeleza nini, wenzie wamuelewe?
ITAENDELEA ASUBUHI..

Big up Majigo nimekubali kazi yako kumbe na wewe una kipaji kizuri namna hii.Nasubili leo asubuhi kuendelea.UBARIKIWE.
 
Last edited by a moderator:
endelea bwana mkubwa...asubuhi kuna stress za siasa ambazo ni hatari kwa afya
 
Babuu kubwa achana na hao wanaokukatisha tamaa kwani kwenye msafara wa mamba na kenge wapoo
 
13--“Jamani kuna ubaya mtu kumuuliza mwanafunzi wenzake?” nilijitetea.
“Hakuna ubaya lakini kuuliza kwako kuna sababu, haiwezekani ukurupuke toka nje ulipolala kitu cha kwanza kutuuliza sisi. Huoni unatutengezea picha mbaya shuleni?”
“Jamani si nimewaeleza au kuna kingine ambacho mnajua mimi sikijui?”
“Halafu unataka kutuambia tuliokosa darasani jana ni sisi wawili , mbona Emma, Mihayo, Koleta na God hawakuwepo darasani jana hukuwauliza ukatuuliza sisi?” walizidi kunibana kwa maswali.
”Nataka kuwauliza swali, kwani ninyi mnafikiria nini?”
”Unakijua lakini hutaki kukisema.”
“Naomba mnisaidie ili nijue mnachokitaka kwangu.”
“Tunataka kujua kwa nini jana ulituuliza sisi tu?”
“Sina jibu zaidi la nililowaeleza.”
“Unajifanya mjanja sio, utaona.”
“Hamna lolote msinitishe.”

Baada ya kusema vile waliondoka na kuniacha nikijiuliza ndoto ile kukosekana kwao shuleni na maswali yao yalikuwa yakiashiria nini. Nilianza kupata picha kuwa wale wasichana wanahusika katika masuala ya kichawi, wasiwasi wao mkubwa kuitoa siri yao. Nilijiuliza walikuwa na maana gani kunitishia kuwa nitaona, baada ya kujifanya mjanja kamna walivyosema . Sikutaka kuwapuuza kusema vile walikuwa na maana gani na kwa nini wanitishe.
Nilingiwa na wasiwasi kutokana na kusikia eti kati ya wale wasichana kuna mmoja alimuambia mwanafunzi mmoja kuwa utaona siku ya pili hakuamka wakamzika . Nilijiona naingia kwenye mtihani mwingine, mzee Manoni alinikataza nisimwambie mtu. Na wale wasichana walikuwa wakinilazimisha huku wakinitisha nitaona, nilijiuliza nini hatima yangu.
Wazo la haraka lilikuwa kwenda kwa mzee Manoni kumueleza jinsi nilivyotishwa na wale wasichana. Nilikumbuka katika njozi tulionana uso kwa macho na wale wasichana wote katika ile ngoma ambayo ilinitatiza kuwa ya kweli tofauti na njozi yenyewe .

Niliamua kuachana nao na kuendelea kuwinda ndege, kwa kuamini ilikuwa ni kunitisha tu ili nisimwambie mtu, japo bado niliamini huenda wakanigeuzia kibao. Nilijikuta nikibadili mawazo na kuona kuna umuhimu wa kuonana na mzee Manoni jioni ile kabla usiku haujaingia ili yasijenikuta kama yaliyomkuta mmoja wa wanafunzi waliotishiwa na Sabina na mwisho wa siku alikufa kifo cha ghafla. Kwa vile nilikuwa nimeingia katikati ya vichaka kuwinda ndege, niliamua kurudi ili niende kwa mzee Manoni kumueleza nilivyotishwa na wale wasichana.
Kama isingekuwa hivyo ningerudi nyumbani kumueleza baba jinsi nilivyotishwa na Helena na Sabina.

Wakati najiandaa niliona wanyama wawili weusi kama mbwa waliokuja mbio mbele yangu wakinifuata niliposimama. Nilipoangalia vizuri niliwafahamu ni fisi, woga uliniingia na kuanza kukimbia kuingia ndani ya vichaka kuwakimbia . Wale fisi walinifuata mbio nyuma yangu. Toka nizaliwe sikuwahi kukimbia vile kwani fisi waliponikaribia niliongeza mwendo, wapotaka kunishika walikosa kwa kuwaponyoka . Walionekana wamenipania kunimaliza. Kila waliponikosa walilia kwa hasira, nilimuomba Mungu aniokoe na lile balaa. Fisi mmoja alifanikiwa kunipiga kucha za mguuni na kunifanya nianguke chini, walinivamia ili waanze kunitafuna. Lakini nilishangaa kuangukia kwenye shimo ambalo mwanzo sikuliona. Wale fisi walibakia wakitazama nikiwa ndani ya shimo, niliwaona wakijilamba kwa uchi wa kunitafuna.


Itaendelea....
 
14--Mara nilisikia fisi wale wakilia kilio cha maumivu na kutimua mbio kuonesha kuna mtu aliwatupia jiwe lililowaumiza na kuamua kuniacha. Nikiwa bado nimo kwenye shimo, nilimuona mzee Manoni aliyenitoa shimoni na kunipa pole. “Pole sana kijana.”
“Asante mzee, fisi hawa walipania kunitafuna.”
“Ni kweli Shija, ningechelewa wangekuua.”
“Mungu wangu.”
“Usijali, nitakusaidia ila ukirudi nyumbani usimwambie mtu kitu chochote ulichokiona na kukisikia, sawa.”
“Sawa mzee.”
“Na hili jereha la mguuni?”
Mzee Manoni alitema mate na kunipaka, kisha alinieleza.
“Nenda nyumbani wala usihofu, jeraha hili ukiamka asubuhi halitakuwepo.”
Niliagana na mzee Manoni na kurudi nyumbani nikiwa bado na hofu nzito moyoni, nikijiuliza wale fisi walitoka wapi. Niliwaza huenda ni kisasi cha wale wasichana walioniambia nitaona na kuamua kunitumia fisi waniue kwa kunila nyama. Pamoja na kutokewa na tukio lile la kutisha bado sikutakiwa kuwafahamisha wazazi wangu.

Niliporudi nyumbani sikutaka kuwa karibu nao kuogopa kuulizwa maswali juu ya jeraha langu ambalo lilikuwa chini ya mguu wa kushoto. Usiku ulikuwa mgumu sana kwangu kwa kusumbuliwa na milio ya fisi waliokuwa wakizunguka nyumba yetu. Hali ilikuwa ikitisha, fisi walikuwa wakiparamia mlango wangu, kilichonishangaza ni wazazi wangu kutulia tuli bila kutoka nje. Hali ile ilinishtusha sana iweje vishindo vyote vya fisi na vilio vyao baba asisikie, mara nyingi kitu chochote kisicho cha kawaida, ilikuwa lazima baba atoke nje.
Lakini siku ile sikupata msaada wowote zaidi ya kuingia chini ya uvungu kujificha.

Vishindo vya kuuparamia mlango wangu, vilinifanya niamini nimekwisha mtoto wa kiume, niliomba Mungu baba asikie vishindo vile ili aamke kuniokoa. Lakini haikuwa hivyo vishindo na vilio vya fisi ambao walionekana walipania kunitoa roho yangu vilizidi. Nilijaribu kupiga kelele lakini hazikuweza kusikika zilimezwa na kelele za vishindo na milio ya fisi. Niliamini siku ile ndiyo ilikuwa kiama changu. Bado sikujiona nina kosa la kutakiwa kutolewa roho, baada ya muda nilisikia sauti ya mtu akiwafukuza fisi wale. Nilivisikia vishindo vya fisi vikipotea taratibu, niliamini asubuhi kungekuwa na nyayo na fisi hata michubuko kwenye ukuta na mlango wa chumba changu.
Kabla sijatoka uvunguni nilipojificha ili nisiliwe na fisi, nilisikia sauti ya baba akigonga mlango wangu huku akiniita jina langu. “Shija amka kumekucha.”
Sikuitikia mara moja, nilitulia ili kuwa na uhakika wa sauti ile, nilinyanyuka huku nikitetemeka na kwenda hadi mlangoni kuchungulia anayeniita kweli ni baba.
Nilipoangalia vizuri nilipata uhakika kumbe kweli ni baba yangu mzazi nilifungua mlango na kutoka nje.

Baba alinishangaa jinsi nilivyokuwa nimechafuka kwa vumbi la uvunguni nilipojificha vitisho vya fisi. Alinishangaa nilivyotapakaa vumbi mwili mzima, mnajua jinsi sakafu za nyumba za vijijini chini hakuna sementi zaidi ya udongo mtupu.
Kama ujuavyo chumbani kwetu bila kukumbushwa kufagia tunaweza kukaa mwaka mzima bila kufagia.
Basi chumbani kwangu uvunguni vumbi mtindo mmoja.
Nilikuwa kama kinyago bila kujijua huku kichwa kikiwa kizito kwa usingizi, baada ya kukesha usiku kucha kwa vitisho vya fisi.
“Shija mwanangu mbona upo hivyo kama ulikuwa umelala uvunguni?”
Baba alinishangaa na kuniuliza huku akinizunguka kunitazama jinsi nilivyokuwa mweupe kwa vumbi.
Nami nilijiangalia huku nikijishangaa jinsi nilivyokuwa , nilijiuliza nitamdanganya kitu gani baba ili akubaliane na hali ile.
“Shija kwa nini umekuwa mchafu siku hizi mtu niliyekuwa nikikutegemea kwa usafi, kuna siku ulilala kitandani na matope.
Leo unatoka ukiwa umepauka kwa vumbi una tatizo gani?”
Nilikaa kimya huku nikitafuta jibu la kumueleza, lakini kila nililofikiria nililiona haliwezi kumkidhi. Ilibidi niseme ukweli wa mambo yaliyonitokea kwa kuamini hata yeye alisikia pengine aliyapuuza.
“Baba, jana fisi walivamia nyumba yetu.”
“Ulijuaje?”
“Baba ina maana vurugu za usiku hukuzisikia?” “Sikuzisikia.”
“Basi jana fisi walivamia nyumba yetu na kutaka kuingia chumbani kwangu huku wakikwaruza kuta na milango.”
“Hao fisi walifika saa ngapi mimi nisiwasikie?”
“Baba, sijui saa ngapi ila wameondoka muda tu nawe ukagonga mlango.”
“Mmh, na hili vumbi?”
“Niliingia uvunguni kuogopa kuliwa na fisi.”
“Sasa mbona kauli yako inapingana na mazingira halisi?”
“Kweli kabisa baba, mlango usingekuwa mzuri wangenitafuna.”
“Hebu njoo.”

Nilizunguka nyumba nzima na baba kutafuta nyayo za fisi hazikuwepo uwanja ulikuwa msafi kama mtu aliufagia. Pia hata kwenye kuta hakukuwa na dalili zozote za mlango kukwaruzwa .
“Haya nioneshe hizo nyayo za hao fisi ulionieleza?”
baba aliniuliza baada ya kuzunguka nyumba nzima bila kuona dalili zozote za kuja kwa fisi kwetu.
“Lakini baba, fisi kweli walikuwepo labda wamefuta nyayo .”
“Shija mimi si mtoto mwenzio sitaki kutaniwa, hao fisi unaowasema mbona hata nyayo zao kwenye uwanja wa nyumbani hazionekani au hao fisi walikuwa wakiruka angani?”
“Baba si angani hata vishindo vyao vilikuwa vikisika nikashangaa kwa nini baba hukuamka.”
“Shija siku hizi umekuwa mtoto mtukutu, mchafu wewe , muongo wewe , ona ulivyokuwa kama umelala nje.”
“Baba kweli,” nilitetea kauli yangu.


Itaendelea....
 
15--“Ungeniambia umeota unafukuzwa na fisi kwa woga ukaingia uvunguni ningekubali,
lakini si kusema kuna fisi walikuwa wakicheza kwenye uwanja wa nyumba yangu.
Basi leo ingekuwa ya kwanza toka nianze kuishi hapa huu mwaka wa ishirini na tisa, sijawahi kuona kitu chochote hapa hao fisi huwasikia kwa mbali.”
Mmh, maneno ya baba ya kuukataa ukweli wangu kwa upande mwingine niliona kama unanisaidia kumdanganya.
Kabla sijamjibu alinieleza.
“Hebu nenda kaoge uwahi shule.”
Sikuongeza neno nilikimbilia kuoga ili niwahi shule, baada ya kuoga nilivaa nguo za shule na kupitia vifaa vyangu kuwahi shule.

Nikiwa njiani huku kichwa kikiwa kizito kwa usingizi, niliwaza mengi juu ya tukio lililotokea usiku wa kuamkia siku ile.
Nilijiuliza ilikuwa ndoto au kitu cha kweli kilichonitokea, sikuamini kama ni kweli kwani kila kilichotokea nilikuwa macho wala si ndotoni.
Kingine kilichonishangaza ni hali ya uwanja kuukuta msafi hauna dalili za kuwepo fisi waliokuwa wakicheza huku wakitaka kuingia chumbani kwangu.
Nilijikuta katika wakati mgumu huku nikijiuliza nini hatima ya matukio yale, kingine kilichonitisha ni kuvunja amri ya mzee Manoni ya kumueleza baba chochote nitakachokiona au kukisikia.
Lakini kwa upande wangu swali la baba halikuwa na jibu la kudanganya zaidi ya kusema ukweli ambao hata hivyo baba hakuuamini.

Nikiwa nakaribia eneo la shule, nilishtushwa na sauti za wale wasichana walionifuata wakati nawinda ndege na kunitisha kuwa nitaona.
“Shija,” Helena aliniita.
Sikujibu niligeuza shingo na kuwatazama kisha niliendelea na safari yangu.
“Shija si tunakuita?” Sabina aliongezea.
“Mna shida gani?”
“Bado hujakoma kiburi eeh”
“Nakuuliza mna shida gani”
“Tulitaka kukueleza una bahati la sivyo ungetutambua sisi kina nani?”
“Ninyi kina nani,mtanifanya nini?”
Siku zote sikupendwa kutishwa na mwanamke.
“Eeh, unatufanyia kiburi, eh'?''
“Hamuwezi kunifanya lolote hata mkijiunga wote.”
“Shija unatuambia sisi hivyo?” Helena alinitisha.
“Hamna lolote wachawi wakubwa ,”
kwa hasira nilijikuta nimeropoka.
“Sisi wachawi ...Sisi wachawi .”
Walisema na wakataka kunivamia wanipige.

Nilijikuta nikipata ujasiri wa ajabu na kuwa tayari kwa lolote juu ya vitisho vya wale wasichana. Ilitokana na tabia yangu ya tangu utotoni kukataa kuonewa na mwanamke.
Baada ya kuhesabu namba tulijichanganya katika kufanya usafi kwenye eneo langu.
Nikiwa nafanya usafi nilifuatwa na mmoja wa wale wasichana niliopigana nao na kuwapiga.
“Shija unaitwa na mwalimu.”
“Si amesema atatuita baadaye”
nilimjibu bila kumtazama. “Siyo huyo.”
“Na mwalimu nani?”
“Mwalimu Vene.” Niliacha kufanya usafi na kwenda ofisini ambako kulikuwa na walimu watatu, mwalimu wa zamu, mwalimu Vene na mwalimu mwingine aliyekuwa akikaa karibu na shule.

Nilipoingia nilimkuta Sabina amekaa kwenye meza ya mwalimu, nilipoingia mwalimu Vene aliniangalia kwa jicho kali kabla ya kunieleza nikae kwenye benchi lililokuwa mbele ya meza yake. Mwalimu Veneranda au kama tulivyomzoea kumwita jina lake kwa ufupi Vene, ndiye niliyemuota na kumuona kwenye ngoma ya wachawi . Baada ya kukaa aliniuliza. “Shija umewaitaje wenzako?” “Sijawaita vyovyote .” ”Mwongo, walimu amesema eti sisi ni wachawi ,” Helena aliingilia mazungumzo.
“Shija, kwa nini umewaita wenzako wachawi ?”
Sikujibu nilikaa kimya, kwa vile sikuwa na jibu, niliinama chini. Mwalimu alipaza sauti kutaka jibu langu.
“Shija nakuuliza kwa nini umewaita wenzako wachawi ?”
Sikujibu tena nilibakia kimya nimeinama, mwalimu kwa hasira alinyanyuka na kuzunguka meza huku akisema. “Unanifanyia kiburi, hunijui eeeh.” Baada ya kunisogelea aliniuliza, huku akiunyanyua juu uso wangu.
“Nakuuliza, uliwaona wanawanga ?”
“Mwalimu nilimwona siku ile,” Helena alidakia bila kujua alimaanisha nini.
“Weeeee, shatapu, unataka kuzungumza upumbavu gani, tena ukome nisikusikie siku nyingine,” mwalimu alimkata kauli Helena, na kunigeukia mimi huku akisema.
“Sasa nataka kukukomesha ukome kuwaita wenzako wachawi . Nakumbuka siku za nyuma uliitisha mkutano kwa kuitwa mchawi, leo hii unafurahia kuwaita wenzako. Kama uliona vibaya sasa nataka nikukomeshe usirudie tena,” mwalimu alisema huku akifuata fimbo nyuma ya meza yake, nilijua kumewaka moto ilibidi nijiteteee kabla sijaadhibiwa. “Mwalimu walikuwa wakinitishia.”
“Kukuroga?”
“Hapana walinieleza nitaona.”
“Sasa mtu akikueleza utaona ndiyo umwite mchawi? Kwa nini hukuwashtaki kwa mwalimu?”
“Mwalimu zilikuwa ni hasira tu.”
“Basi lala chini nizipulize hizo hasira.”


Itaendelea...
 
Huku Net Haijakaa Poa
Mnisamehe Wadau, Natupia Kimitego Tu!
 
16--Nilipochelewa kulala, fimbo ya mgongoni ilinipeleka chini, mwalimu alinipiga fimbo zisizo na idadi kisha alinipa adhabu ya kuchimba shimo la taka. Sikutaka kubisha kwa vile niliamini kama nitabisha au kulipeleka mbele lingezua mjadala mkubwa. Nilitekeleza ile adhabu huku vipindi vitatu vya asubuhi vikinipita, baada ya kumaliza adhabu nilirudi darasani kuendelea na masomo huku wanafunzi wakinipa pole, wakisema nimeonewa. Lakini mwalimu wa darasa alinipoza na kuniomba niwe mtulivu na kuniona nisichukue sheria mkononi kama nitachokozwa basi nipeleke mashitaka kwa mwalimu yeyote .

Nilijiuliza mambo mengi kutokana na vitendo vingi kufanyiwa nje ya shule huku nikizibwa mdomo na mzee Manoni. Japo niliumia moyoni lakini niliendelea kuumeza mfupa wa siri nzito ambayo sikuamini kama baba angeijua kusingekuwa na usalama. Baba nilimjua vizuri hakupenda kuona mtoto wake akinyanyasika , alishapigana na jirani yetu baada ya kunipiga kutokana na mbuzi wetu kuingia kwenye shamba lake. Niliamini kama nitamweleza kila kilichonitokea kungekuwa na vita kubwa kati yake na mzee Manoni, hata familia ya wale watoto watukutu. Nilikubali niwe mjinga ili kufunika kombe mwana haramu apite.

Baada ya masomo nilirudi nyumbani nikiwa na zigo zito la mawazo juu ya mambo yaliyokuwa yakinitokea huku nikikatazwa nisiwaambie wazazi wangu.
Nilijiuliza hali ile itaisha lini, nilitembea kwa mwendo wa taratibu kurudi nyumbani.

Kila dakika iliyokuwa ikija mbele yangu ilikuwa ya maajabu, baada ya mwendo wa dakika kumi nilijikuta nimetokea sehemu ambayo ilikuwa mbele zaidi na ninapoishi.
Nilijishangaa kutembea na kupita kwetu bila kujijua, kabla sijaamua nifanye nini nikiwa najishangaa kufika sehemu ile, akili yangu ilinielekeza kwenye mawazo kiasi cha kushindwa kuona mbele. Lakini sikuwa na mawazo kiasi cha kushindwa kutambua naelekea wapi. Sauti ya mzee Manoni iliyokuwa imezoeleka akilini mwangu iliniita kwa nyuma. “Shija!”
Kabla ya kuitika nilishtuka na kugeuka kutokana na kushtukizwa na sauti ile, eneo lilikuwa jeupe na sehemu niliyokuwepo chini ya mti kulikuwa na majani mengi yaliyokauka .
Mtu akija nyuma yako lazima umsikie kutokana na kelele za majani makavu. Kila dakika nilizidi kumwogopa mzee Manoni na kuamini ujaji wake si wa kawaida ni wa miujiza na kuamini siku nitakayomweleza baba huenda akatokea mbele yangu.
Ujaji wake sikuweza kumsikia na kumshtukia nyuma yangu, baada ya kushtuka bila kujibu mzee Manoni alicheka mfululizo na kusema...


Itaendelea...
 
17--“Shija mbona mwoga hivyo ?”
“Mzee Manoni, umenishtua sana.”
“Ooh, pole na huku umekuja kufanya nini?”
“Hata sijui, nashangaa kujikuta huku.”
“Ooh, pole sana.”
“Asante.”
“Mmhu, nasikia leo umepigana shule?”
“Mmh, hamna; nani kakwambia ?”
“Nijibu sio kuniuliza swali.”
“Ndiyo.” “
Kwa sababu gani?”
“Walinitisha nitaona.”
“Ehe?”
“Basi nami sikukubali ndipo tuliposhikana.”
“Kweli?” Mzee Manoni ilionesha anajua kila kitu.
“Kweli mzee Manoni.”
“Shija nakuamini, mbona unanidanganya.”
“Ni kweli mzee Manoni.” “Sababu ya kupigana ilikuwa nini, uliwaambia wao ni nani?”
“Wachawi.”
“Kwa nini?”
“Ni hasira tu.”
“Shija nilikueleza nini, mbona siri unaanza kuitoa nje mapema?”
“Nimekosa mzee Manoni ni hasira tu, Lakini sirudii tena,” nilijitetea.
“Basi yamekwisha , ukitoka hapa kama kawaida yetu usimwambie mtu.”
“Sawa, mzee Manoni.”
“Unaweza kwenda nyumbani,”
alinieleza huku akiondoka eneo lile.
Niligeuka na kuanza kurudi nyumbani taratibu bila kumuangalia tena mzee Manoni aliyekuwa akiyeyuka kama upepo, sikutembea hatua nyingi nilijiona nimetokea kwenye uzio wa nyumbani.

Kama kawaida yangu hata lile nililimeza moyoni mwangu. Hata wazazi wangu waliporudi shambani hawakujua nini kilichotokea shuleni, sikumueleza baba nilikaa kimya. Niliendelea kumuomba Mungu kila kitu kilichotokea na kuonekana mbele ya macho ya watu baba asijue.

Siku zilikatika huku hali ya utulivu ikijirudia, nililala usingizi mzuri bila vitisho shuleni nilisoma bila usumbufu na wale wasichana walibadilika na kuwa marafiki zangu. Niliamini wagombanao ndio wapatanao. Lakini akili yangu ilikosa amani kwa kushindwa kuutua mzigo mzito wa vitu vilivyonitokea ambavyo baba ndiye angekuwa matatuzi wangu.
Kila dakika nilijiuliza kama nikimueleza baba juu vitu nilivyokutana navyo na onyo nililipewa na mzee Manoni itakuwaje?
Wasiwasi wangu ulikuwa kwa vile mzee manoni ni mchawi pia chama chao ni kikubwa , kama nilichokiona mara mbili ndotoni ningeweza kumpoteza baba yangu.
Niliamua kuumeza mfupa wa siri ili siku ziende mbele, kwa kuamini kila lenye mwanzo lina mwisho, japo sikujua mwisho wake nini.

Pamoja na utulivu uliojitokeza bado nilikosa amani moyoni mwangu kila nilipokumbuka yote yaliyonitokea . Uwezo wangu kimasomo haukushuka sana pamoja na matatizo lukuki kichwani mwangu bado niliongoza darasani. Wakati wote huo kaka yangu aliyekataa shule alitoweka bila kujua amekwenda wapi, tuliamini amepotea baada ya kupotea zaidi ya miezi miwili bila kuonekana.
Tulijikuta tukisubiri siku atakaporudi, lakini hakukuwa na taarifa zozote za kuonekana au kusikia tetesi kaonekana wapi.

Mwezi wa tatu toka kaka atoweke nyumbani, siku moja tukiwa uani tumekaa tukisubiri chakula cha usiku, sote tulishangaa kumuona kaka akirudi.
Kitu cha ajabu hakutaka kuzungumza na mtu, aliingia chumbani kwake na kulala. Baba alisema tumuache ajipumzishe akiamka atazungumza naye siku hiyo au ya pili. Tulimuacha alale ili asubuhi tumuulize alikuwa wapi siku zote hizo pamoja na akili yake kuharibiwa na bangi.
Hata chakula hakutaka hivyo haikutusumbua, mama alimuwekea chakula kama njaa ingemshika basi angeamka na kula.

Baada ya kupanda kitandani kwake na kulala muda wangu wa kulala ulipofika nilipanda kitandani kwangu.
Usiku wa siku ile ulikuwa wa mang’amu ng’amu kutokana na kusikia vitu vya ajabu ambavyo sikuwahi kusikia. Pia milio ya ngoma na vishindo vya watu katika nyumba yetu vilikuwa vikubwa , hali ile ya kutisha ilichukua zaidi ya masaa mawili nje ya nyumba yetu huku watu wakichelekea kama siku niliyohudhuria ngoma ya wachawi waliokuwa wakishangilia nyama za watu.
Kuna kipindi nilihisi kama ukuta wa nyumba yetu umepasuka eneo kilipokuwa kitanda cha kaka. Lakini sikuona kitu chochote na ukuta ulikuwa vile vile japo nilisikia mlio huo, nilijikuta nikisikiliza kwa vile nilianza kuzoea ile hali ambayo ilionesha haikuwa ya kunidhuru. Niliamini pengine ni kujifurahisha katika michezo yao ya kichawi.

Baada ya matukio mazito nje ya nyumba yetu yaliyodumu kwa masaa zaidi ya mawili, ngoma ile iliondoka huku nikiwasikia wakiondoka eneo la nyumbani huku wakishangilia. Nilizidi kushangaa baba kutoamka wala kutoka nje kutokana na kelele zilizokuwa nje ya nyumba yetu. Baada ya muda hali ya utulivu ilijirudia nami usingizi haukuchelewa kunichukua.

Kwa vile siku ya pili ilikuwa Jumamosi, niliamka saa moja kwa ajili ya kwenda kisimani. Baada ya kuamka nilipitia vyombo ili niende kisimani, kaka alikuwa bado amelala usingizi mzito. Wakati huo wazazi wetu tayari walikuwa wamekwishakwenda shamba, baada ya kutoka kuchota maji nilishangaa kaka kuendelea kulala kitu ambacho siku za nyuma haikuwa kawaida yake, kilichonishangaza mlalo aliolala toka jana hakujigeuza alilala vilevile mpaka asubuhi. Lakini niliogopa kumwamsha kutokana na kiburi alichokuwa nacho kwani ningeambulia makonzi. Lakini mpaka inafika saa tano bado alikuwa kitandani.
Niliamua kwenda kumwamsha ili anywe uji, nilipomtikisa ili aamke mwili wake ulikuwa umelegea kila nilimpomtikisa alinifuata. Hali ile ilinitisha nilikumbuka siku moja kuna mtoto alianguka shuleni na kulegea vile. Baadaye tuliambiwa alikuwa ameisha kufa kitambo. Hali ile ilinitisha sana na kutoka mbio hadi shambani na kuwaeleza wazazi wangu hali aliyokuwa nayo kaka.


Itaendelea...
 
18--“Ina maana toka jana alipoingia ndani hajaamka?” Mama aliuliza..
“Ndiyo mama.”
“Mmh, yatakuwa mabangi yake,” baba alisema bila kuonesha kushtushwa sana.
“Baba si mabangi, amekuwa kama Jose aliyeanguka shule na kulegea vile baadaye tuliambiwa amefariki dunia.”
“Mmh, si rahisi, hebu twende.”

Niliondoka na baba lakini mama naye hakukubali kubakia shamba tuliongozana wote hadi nyumbani. Tulipofika tuliingia wote chumbani, baba alimuangalia kaka kwa muda kisha alinieleza.
“Shija toka nje mara moja.”
Nilitoka nje na kuwaacha wazazi wangu ndani, sikukaa mbali nilikaa pembeni ya mlango kutaka kujua kaka amepatwa na nini.
Baada ya dakika kama kumi nilisikia kilio cha mama cha sauti ya juu lakini baba alimzuia kulia.
“Jamani mwanangu wamemfanya nini, Paulo baba ulikwenda wapi mwanangu na kurudi hata salamu hukunipa... Kumbe baba ulikuwa na siri nzito moyoni mwako. Kwa nini baba umeniacha, nilitaka nife unizike sasa kama baba umetangulia nitazikwa na nani mimi jamani?”
Maneno ya mama yalinipa picha kuwa kaka alikuwa amefariki, kabla ya kuanza kumlilia kaka yangu nilijawa na maswali yaliyotakiwa kupatiwa majibu na mtu mwingine si mimi mwenyewe .
Swali la kwanza kaka alikuwa wapi?
Swali la pili alipokuja alikuwa na siri gani moyoni mwake ambayo hakutaka tuijue kabla ya kifo chake?
Swali la nne kwa nini hakutaka kuzungumza na mtu?
Na swali la mwisho ile ngoma ilikuwa ikiashiria nini?

Nilijikuta nikiwaza kitu cha ajabu, huenda ile ngoma ilikuwa chanzo cha kifo cha kaka. Kingine kilichonishangaza ni wazazi wangu na ndugu zangu kutosikia ile ngoma. Kwani hakuna hata mmoja aliyehoji asubuhi kusika ngoma na makelele yakipigwa kwenye uwanja wa nyumba yetu.
Yalikuwa maswali ambayo kama nisingekatazwa na mzee Manoni niliamini baba angenipatia majibu.

Kilio cha mama kilikusanya majirani, ambao nao waliungana na mama kumlilia kaka, haikuchukua muda wanakijiji walikusanyika na kuanza mipango ya mazishi.
Katika watu waliofika msibani alikuwepo mzee Manoni hata wazazi wa wale wasichana ambao niligombana nao na mwishowe kupatana nao walikuwepo .
Baada ya maandalizi yote tulimzika kaka kwenye makaburi ya kijiji, baada ya msiba kila mmoja alizungumza lake kuhusiana na kifo cha kaka kutokana na maelezo ya baba aliyosema baada ya kuuzika mwili wa kaka.

Japo kuna watu walinong’ona kuwa kifo cha kaka si cha kawaida huenda ni mkono wa mtu. Lakini baba aliamini kile kifo ni cha kawaida kama vilivyo vifo vingine wala hatajishughulisha na upuuzi wowote kutaka kujua nini chanzo cha kifo cha kaka.

Baba alisema kwa sauti ya huzuni: “Jamani, najua kifo cha mwanangu kimewashtua wengi, mazingira ya kutoweka kwake na kuonekana kwa kweli yanatatiza. Lakini bado naamini kifo chake ni cha kawaida.
Sitakwenda kuutafuta ukweli popote, kufanya hivyo ni mwanzo wa kutafuta uhasama na watu.
Kama amri ya Mungu atajua yeye kama mkono wa mtu vilevile atajua yeye . Hivyo nashukuruni kwa msaada wenu wa hali na mali.”
Baba katika maisha yake pamoja na kukaa eneo ambalo lilikuwa likisadikiwa kuwa kuna baadhi ya watu mchana watufisi usiku hakuliamini.
Na ndiyo maana minong’ono ya watu kuhusiana na kifo cha kaka aliikanusha. Niliamini hata kama ningemueleza yaliyotokea kabla ya kifo cha kaka bado angeona ni uzushi tu.

Baada ya msiba wa kaka nilianza kuweweseka kila siku usiku nilipolala, mambo yaliyotokea siku ambayo asubuhi yake kaka alifariki yalijirudia kila nilipoweka ubavu chini. Hali ile ilinisumbua zaidi ya wiki nzima, kingine kilichoniweka katika wakati mgumu ni sauti ya kilio ya kaka akilalamika kuumizwa na bakora.
Nilimsikia kwa sauti yake kabisa akilia huku sauti za bakora akichapwa zikisika, kwa kweli iliniuma kusikia sauti ya kaka yangu aliyekufa akipigwa nje ya nyumba yetu kila siku usiku.

Kuna siku uzalendo ulinishinda na kuamua kutoka nje usiku huku nikijisemea liwalo na liwe.
Baada ya kufungua mlango sauti ile ilikoma, sikurudi ndani mara moja nilitulia kusikiliza kama ni ya kweli au naota. Nje usiku kulikuwa kunatisha kutokana na kiza kizito na ubaridi kilinipuliza na kuzidisha hofu moyoni lakini sikurudi ndani nilitaka kujua mwisho wake, sikuhofia kitu nilizunguka nyumba, lakini sikuona kitu chochote, zaidi ya milio ya bundi na fisi kwa mbali.
Nilirudi ndani na kujilaza masikio yakiwa nje, kusikiliza kama atarudi tena, lakini mpaka kunakucha sikusikia kitu chochote.

Kila alfajiri baba aliponiamsha hakuonesha kusikia kitu chochote usiku kwenye uwanja wa nyumba yetu. Nilijiuliza ni kweli yote yanayotokea ni viini macho au kweli, bado niliamini mtatuzi wa yote yale ni baba, lakini nilijiuliza nitaanzia wapi na baada ya kumueleza nitambebea mbeleko gani mzee Manoni.
Niliamini hali ile ikiendelea hata kusoma nitashindwa, muda mwingi darasani nilikuwa nasinzia au kuhama kimawazo.

Siku moja shuleni tukiwa mapumziko, niliwasikia wanafunzi wenzangu wakizungumzia habari za mtu kugeuzwa msukule. Mtu kuonekana amekufa lakini anakuwepo na kutumikishwa kazi au kuuawa na kugeuzwa kitoweo cha wachawi . Lakini walisema wapo waganga ambao huweza kuwarudisha watu wa aina hiyo. Maneno yale yalinisisimua na kuamini kabisa kaka yangu hajafa kageuzwa msukule, lakini habari zile niliogopa kumueleza baba ningeanzia wapi? Kwani ni mtu aliyekwishasema haamini imani za kishirikina.
Ningeanzia wapi mpaka anielewe na akinielewa mzee Manoni angeniacha hivihivi ? Niliendelea kufa kizungu na tai shingoni.
Kama kawaida maendeleo yangu ya shule yaliendelea kuporomoka kufikia hatua ya kushika nafasi ya kumi darasani kitu ambacho sikuwahi kukiota.
Taarifa zilimfikia baba ambaye alipewa msururu wa matukio yaliyonitokea ambayo toka wakati huo maendeleo yangu yamekuwa yakiporomoka kila siku.
Bila kuwa na habari siku moja baada ya chakula cha usiku baba aliniita kuniulizia kwa nini simuelezi matatizo yaliyonikuta kufikia hatua ya kuporomoka kimasomo.


Itaendelea...
 
Back
Top Bottom