Nitakufa Mara Ya Pili

Nitakufa Mara Ya Pili

72--Niliendelea kutii amri na kumfuata kwa nyuma kila kona aliyopita kwa kuvuka milima na mabonde. Muda ulionyesha ni alfajiri kutokana na nuru hafifu kuitawala anga huku baridi kali ikiendelea kunipiga.

Baada ya mwendo usiopungua saa mbili tulifika kwenye kijito, hapo Helena aliniamuru nioge kwa sabuni aliyokuwa nayo. Maji yalikuwa ya baridi sana, nilihisi kama damu inataka kuganda mwilini.

Nilipomaliza kuoga, alinipa dawa ya unga kulamba. Baada ya kulamba nilijiona mwepesi kuliko kawaida na kujiona nipo dunia mpya na mimi mtu kwenye watu.


“Shija unajikiaje?” Helena aliniuliza. “Yaani nauona mwili mwepesi kama nimevuliwa kitu kizito nilichokuwa natembea nacho mwilini. Pia nimeona vitu vingi ambayo toka niingie ndani sikuwa kuviona, inaonesha nipo dunia ile niliyoizoea miaka mingi iliyopita na vile vile napata hewa safi ambayo ni nyepesi puani kwangu tofauti na mwanzo,”
ilikuwa ajabu ya mwaka baada ya kulamba dawa nilijiona nimeingia dunia mpya.


Baada ya kuona tofauti ya mwanzo na muda ule nilipolamba dawa, Helena alitoa dawa nyingine na kuanza kunisugua baadhi ya sehemu za mwili wangu. “Helena kufanya hivi unamaanisha nini?” “Hapa nafuta chale za kichawi ambazo huwa kama muhuri wa kutambulika popote kuwa wewe ni mtu wao.”


“Baada ya hapa inakuwaje?” “Shija mpaka sasa upo katika dunia uliyoizoea na hapa tupo maeneo ya Kahangara.” “Kahangara ya Magu?” “Ndiyo.” “Usiniambie Helena!” Nilishtuka nisiamini.


“Kweli?” “Ina maana tayari umenitoa kwenye dunia ya wafu?” “Ndiyo Shija.” “Siamini.” “Kweli.” “Hawawezi kutukamata?” “Hawawezi .” “Siamini! Nimetoka kwenye umsukule.” “Amini sasa hivi wewe si msukule tena.” “Helena kweli?”


Bado sikuamini niliona kama ananifurahisha kwa kitu kisichowezekana . “Kweli kabisa Shija.” “Yaani dunia naiona mpya bila kunieleza hapa wapi wala nisingepajua.” “Kweli, inaonekana kukaa ndani muda mrefu umeanza kusahau vitu vingi.” “Siamini kama kweli mimi si msukule sasa?” “Amini, sasa hivi tuna kazi ya kujipanga kufika kwenu na mtu yeyote asikutambue.”


“Si umesema nisirudi nyumbani?” “Ndiyo, hii safari kwa mjomba wako.” “Tutafikaje?” “Nitakutanda khanga uonekane mwanamke, nilitaka nikuache uende peke yako lakini wasiwasi wangu unaweza kupotea na kuwa kituko kwa watu.


Nitakupeleka mpaka kwa mjomba wako ukiifahamu nyumba mimi nitarudi.” “Kwa nini usiingie ndani?” “Kumbuka hii ni siri yetu wawili , hatakiwi mtu yeyote kuijua.” “Helena mama yako yupo wapi?” “Mmh! Amesafiri na baadhi ya wachawi wenzake.”


“Wamekwenda wapi?” “Wamekwenda kwenye mkutano mkuu wa wachawi Sumbawanga.” “Mmh! Mkutano huo unachukua siku ngapi?” “Siku mbili.” “Tokea lini?” “Jana usiku na leo.” “Asiponikuta itakuwaje?” “Hawezi kunifanya lolote.” “Si atanitafuta?” “Atakupata wapi?”
“Chale nilizokufuta zitamfanya asikuone tena, labda mkutane kawaida lakini kichawi hawezi kukuona.”


“Tutakwenda Mwanza kwa miguu?” “Hapana, tutapanda basi.”
“Nauli unayo?” “Shija mpango huu nimeupanga muda mrefu kwa hiyo kwa hilo usiwe na wasiwasi .” “Siamini mpaka nikutane na mjomba.” “Shija naomba uniamini sitaki tena maswali ya kijunga,” Helena alichoshwa na maswali yangu ya kijinga. “Samahani Helena kama nimekuudhi.”

“Maswali gani kila nikikueleza unielewi?” “Najua nitakuudhi lakini bado naona kama ndoto.” “Pole Shija, samahani kwa kukukaripia, lakini sasa hivi kama mfungwa upo huru labda ufungwe kwa kosa lingine.” “Barabara ya kuelekea Mwanza iko wapi?”
“Ni mwendo kidogo, tufanye tuondoke eneo hili kabla wanakijiji hawajaanza kupita kwenda kwenye kilimo.” Helena alifungua mfuko wa plastiki na kutoa kaptura na fulana ambavyo alinipa nivae na kuzitupa za zamani.


Baada ya kubadili nguo, alinipa khanga mbili, moja nilijifunga chini na nyingine nilijitanda juu na kuwa kama mwanamke. Helena alifanya vile vile kisha tuliondoka eneo lile la mto na kufuata njia aliyokuwa akiijua Helena kuelekea barabarani.



Ni kweli Helena amefanikiwa kumtoa Shija kwenye umsukule?

ITAENDELEA BAADAYE kidogo.....
 
Kweli adui wa leo ndiye rafiki wa kesho, tenda wema nenda zako usingoje shukrani
 
Wapi Majigo?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
73--Tulitembea kwa mwendo wa dakika kama kumi na kutokea kwenye barabara kuu itokayo Musoma kwenda Mwanza. Baada ya kuiona barabara, akili yangu kidogo ilianza kupata mwanga japo bado sikuelewa ile ni sehemu gani pamoja na kuelezwa kuwa ni Kahangara


Muda ulionesha kuwa kunazidi kupambazuka kutokana na mwanga kuongezeka. Pia watu waliongezeka, kila mmoja akiwa na lake. Wakulima walielekea mashambani na wanafunzi mashuleni, pia kituoni tulipokuwa tumesimama watu wachache waliongezeka.


Kijua nacho kilianza kuchomoza kuonesha kumepambazuka. Tulisimama kituoni nikiamini kabisa watu walijua sisi sote ni wanawake . Baada ya muda, basi la kutoka Magu liliwasili. Tulipanda na kusimama kutokana na siti zote kuwa na watu.


Helena aliniuma sikio kwa sauti ya chini. “Usizungumze kitu, mambo yote niachie mimi.” “Sawa,” nilimjibu kwa sauti ya chini. Basi lilielekea Mwanza huku nikiwa bado siamini kama kweli nimetolewa kwenye umsukule japo ilikuwa tofauti na siku za nyuma Helena alipojaribu kunitoa kwenye himaya ya wachawi na kukutana na matukio ya ajabu yaliyonikwamisha .


Japo gari lilikuwa likienda, bado sikuamini kama tutavuka salama. Basi lilipofika maeneo ya Kisesa, wingu zito lilitanda mbele na upepo mkali ukaanza kuvuma na kusababisha tufunge madirisha. Wasiwasi uliniingia nikajua mambo yameiva , nilijiuliza kama nikikamatwa tena na wachawi watanifanya nini?


Haukupita muda mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali ilishuka. Kutokana na upepo mkali, nusura gari tulilokuwa tumepanda lianguke baada ya kuyumba na kuteleza mpaka pembeni ya barabara. Wakati huo mbele kulikuwa hakuonekani vizuri kutokana na mvua kuwa kubwa.


Moyo ulinienda mbio kwa hofu na kuamini kabisa wachawi tayari wameshatuzingira. Pamoja na kuwa na baridi kali kutokana na mvua ile ya asubuhi, mimi kijasho kilikuwa kikinitoka. Helena aliugundua wasiwasi wangu na kuniuliza:
“Shija vipi?” “Naona mambo yameharibika.” “Mambo gani?” “We huoni mvua.”
“Sasa mvua imeharibu nini?”
“Naona kama tumefuatwa.” “Na nani?” “Si wachawi !” “Shija hebu acha hofu, kwani mvua yote ni ya wachawi ” “Lakini si unaona jinsi hali ilivyo , bado kidogo gari lianguke.”


“Ni hali ya mvua tu, inaonekana upepo umemfanya dereva asione vizuri mbele. Wazo la kusubiri mvua ipungue ni zuri, la sivyo anaweza kutuangusha. Barabara inateleza sana kwa muda huu.” “Helena ni kweli usemayo si hila za wachawi ?” “Walaa, niamini mimi.



Hakuna kitu chochote kibaya kitakachokutokea , kama kikitokea ni amri ya Mungu wala si wachawi .” “Basi niliogopa sana, nilijua ni yale yale ya siku zote.” “Shija usiwe na wasi, mpango huu hakuna anayeujua mpaka mama arudi kwenye mkutano, muda huo utakuwa umeshafika kwa mjomba.”

“Ooh, afadhali maana kwa upande wangu hali ilikuwa mbaya.” Tulisubiri mpaka mvua ilipokatika ndipo tulipoendelea na safari.

Nilimshukuru Mungu baada ya kuingia Mwanza salama. Tulipanda daladala hadi Pasiansi kwa mjomba. Tulipokaribia, kutokana na maelezo ya Helena kuwa hataki kufika pale, aliomba nimuoneshe nyumba kisha tuagane. “Helena, tumekaribia kwa mjomba.”


“Ni wapi?” “Nyumba hiyo hapo yenye rangi ya maziwa, nje kuna nguzo ya umeme.” “Sasa Shija, nafikiri kazi yangu imekwisha. Nakuomba uende salama na Mungu akulinde kwa kila jambo.” “Asante Helena, nawe Mungu akulinde japo najua nimekuachia mtihani mzito na mama yako.”


“Shija hilo lisikutie hofu, hakuna chochote kitakachotokea. Muhimu katika ahadi yangu ilikuwa ni kukulinda. Niliposhindwa niliapa kukutoa kwenye dunia ya wafu, namshukuru Mungu ahadi yangu kwako imetimia.” “Nashukuru sana Helena, sijui nikulipe nini?”

“Hakuna cha kunilipa, Shija umenifundisha vitu vingi maishani mwangu ambavyo sikutegemea kuvipata kwa kijana mdogo kama wewe .” “Helena busara si umri bali uwezo wa kuchambua baya na zuri na kufikisha maneno yenye kumfanya mtu apate kitu kupitia wewe bila kujali umri wako.”

“Shija nakuomba tena usikubali kurudi kijijini. Kwa muda huu baki kwa mjomba, pia siri hii ibakie moyoni mwako.” “Nitafanya hivyo Helena.” “Mwisho Shija nakutakia maisha marefu yenye furaha, kwa vile nimepajua nitakuja siku moja, kwa heri! Msalimie mjomba, mkewe na wadogo zako.”
Helena alisema kwa sauti ya majonzi huku machozi yakimtoka , kitu kilichofanya nami nitokwe na machozi.

”Asante Helena, nawe nakutakia harusi njema na Mungu akuepushe na nguvu za kichawi.” “Asante Shija.” Tulikumbatiana kabla ya kuagana, tulishikana kwa muda huku kila mmoja akilia kilio cha kweli.
Baada ya kuachiana, Helena alisema kwa sauti ya mafua kutokana na kutokwa na kamasi nyembamba.

“Shija nakupenda sana, hata sijui moyo wangu umeuwekea kitu gani.
Nimekubali kuolewa kwa vile nauchukia uchawi lakini bila hivyo nisingeolewa kamwe, ningekusubiri.”

“Asante Helena kwa kunipenda, hata mimi nakupenda na nitaendelea kukupenda siku zote za maisha yangu. Nakuona ni zaidi ya pumzi ninazovuta. Helena olewa ukijua Shija anakupenda sana.”


“Na Sabina?” Helena aliniuliza swali la uchokozi.

“Wote nitaendelea kuwapenda kama tulivyokuwa tukipendana tukiwa shule ya msingi.” “Asante Shija, kwa heri,” Helena aligeuka na kuondoka huku akilia kilio cha kwikwi , kitu kilichoniacha njia panda. Nilitaka kumwita lakini mdomo ulikuwa mzito.


Nilimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea machoni mwangu. Nilisimama kwa muda nikijiuliza Helena kanifikisha mpaka jirani kwa mjomba, sawa lakini swali kubwa ni mjomba atakaponiona atanipokea vipi? Niliamua niende tu, mengine yangejulikana huko huko.



Nini kitaendelea, mtu aliyekufa akionekana mzima itakuwaje, fuatilia mwisho ya simulizi hii
 
Nasubiri jinsi watu watakavyotimua mbio kuiona maiti inatemebea
 
Umetisha kiasi kwamba umerudisha mood yangu iliyopotea kitambo big up
 
Namhala Majigo, nhaga ginhuko togulindelaga!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hizi stori, sitafuatilia tena maana nimekuwa teja toka kwa mjeda na my wit wake.

Hapa waweza limwa memo
 
74---Nilitembea taratibu kuelekea nyumbani kwa mjomba, muda ulionesha bado asubuhi kwani hata mlango ulikuwa haujafunguliwa.
Kabla ya kugonga nilijifikiria nizivue zile khanga au niingie nazo vilevile . Niliamua kuingia na khanga zangu ili wasishtuke mapema.

Niligonga mlango na kusubiri, mke wa mjomba ndiye aliyekuja kunifungulia, nilijua hakunifahamu baada ya kuniona. “Karibu, una shida gani?”
Aliniuliza akiwa bado amesimama mlangoni. “Nataka nimuone mjomba.” “Mjomba wako nani?” “Mayunga.” “Mayunga! Wewe nani?” “Shi..,” nilisita kulitaja jina langu. “Umesema nani?” “Shija.” “Shija si jina la kiume hilo?” “Ndiyo.”


Nilisema huku nikitoa khanga niliyojitanda kichwani, nilimuona macho yakimtoka pima kama kaona ngamia akipita kwenye tundu la sindano.
Akitaka kujirudisha nyuma ili anikimbie, niliamini kabisa aliniona si mtu wa kawaida bali mzimu wangu kwa vile aliamini nimekwisha kufa na kuzikwa . Shangazi alipiga kelele: “Jamani nakufa..,” alianguka chini na kupoteza fahamu, mjomba ambaye alionekana amemaliza kujiandaa ili aende kazini.

Alikuja mbio na kumuwahi mkewe bila kuniangalia mimi ni nani. Bila kunitazama usoni aliniuliza: “Amefanya nini huyu,” aliendelea kumtazama mkewe aliyekuwa amepoteza fahamu.

“Ameshtuka baada ya kuniona.” “Kukuona?” Aliuliza huku akinitazama aliponiona ni mimi alishtuka kiasi cha kumbwaga mkewe chini. “Ha! Wee nani?” “Shija mjomba.”

“Hapana, hiwezekani haya ni maajabu.”
“Siyo maajabu, sikufa mjomba.” “Kama hukufa aliyekufa ni nani?” “Mjomba kile ni kiini macho cha wachawi .” “Muda wote huo ulikuwa wapi?” “Mjomba mshughulikie kwanza shangazi nina mengi ya kuzungumza juu ya kifo changu cha bandia.”


Mjomba alimpatia huduma ya kwanza shangazi ambaye alirudiwa na fahamu lakini ilionesha bado ananishangaa. “Huyu si Shija?” Shangazi aliuliza kwa sauti ya juu. “Ndiye.” “Mungu wangu! Haya si maajabu Shija katoka kuzimu si alikufa huyu?”

“Sijafa Shangazi kilikuwa kiini macho cha wachawi .” “Kama hukufa nani alikufa tukamzika?” “Shangazi mimi sikufa ila kilichotendeka siku ile ni kiini macho tu, hamkuzika mtu bali kipande cha mgomba.”

“Na wewe ulikuwa wapi siku zote?” “Ni stori ndefu shangazi.” “Jamani haya ni maajabu ni kweli Shija hujafa?” Shangazi aliendelea kunishangaa. “Kama ningekuwa nimekufa nisingeonekana leo.” “Muda wote ulikuwa wapi?” Mjomba aliniuliza.

“Nilikuwa naishi maisha ya kimsukule.”
“Mungu wangu! Umewezaje kutoka katika maisha hayo? Hizi khanga umezitoa wapi?” “Ni mtoto wa mchawi aliyenichukua msukule.”
“Ndiye aliyekutoa?”
“Ndiyo.”
“Na siku ya msiba wako ulikuwa wapi?” “Nilikuwa nyuma ya mlango, yote mliyokuwa mkifanya niliyaona, wakati mnakuja nilisikia hata mlipoingia ndani kumpa pole mama na kuangua kilio, yote nilikuwa nayaona.

Hata makaburini nilihudhuria mazishi yangu.” “Hii kali kweli wachawi viumbe wa ajabu,” alisema mke wa mjomba huku akishika mikono kiunoni.


“Sasa wamekuachia au imekuwaje?” “Nimetoroshwa.” “Mungu wangu ilikuwaje mpaka ukatoroshwa?” “Ni habari ndefu, naomba nioge niondoe nuksi ya maisha ya nusu kuzimu na nipate chakula maana hapa njaa inaniuma kama kidonda.”


Nilipatiwa vitu vyote kwa haraka hata safari ya mjomba na mkewe kwenda kazini iliahirishwa ili kutaka kujua maajabu chini ya jua. Baada ya kuoga na kupata kifungua kinywa nilikaa kitako kuwaeleza yaliyonisibu huku nikiificha siri ya kumtaja Helena na mama yake kwa usalama wa kijijini.

Siku hiyo nilichukuliwa na kupelekwa kwenye kanisani kufanyiwa maombezi kwa utukufu wa Mungu kuonesha jinsi nguvu zake zinavyoweza kuushinda uchawi.

Mjomba alitaka kunipeleka nyumbani, nilimweleza masharti niliopewa na mtu aliyenitoa kule kuwa nisirudi tena kijijini.


Mjomba alikubaliana na mimi nibakie kwake , wazazi wangu walifuatwa , hawakuamini lakini niliwaeleza ilivyokuwa na kukubaliana na mimi, ilikuwa furaha isiyo kifani.


Baada ya muda niligundua kumbe niliishi maisha ya umsukule kwa mwaka mmoja na miezi sita.
Mjomba alinitafutia shule ambayo nilisoma kwa miaka miwili na kufanya mtihani wa kidato cha nne.

Majibu yalikuwa mazuri kwa kupata ‘division two’ iliyoniwezesha kuingia kidato cha tano mpaka chuo kikuu



NAMSHUKURU MUNGU, NA NYOTE GUEST NA MAMBER WENZANGU WA JAMII FORUMS
MLIOKUWA PAMOJA NAMI TOKA MWANZO WA SIMULIZI HII YA KWELI KABISA
NAWAPENDA SANA NA MUNGU AWABARIKI!

[><MAZIMA><]
 
Back
Top Bottom