60--Helena alinikanda mwili nzima huku maumivu ya majeraha nikiyasikia kila yalipoguswa na maji. Nilishangaa jinsi Helena alivyojitolea kunisaidia kwa kunikanda.
Baada ya kumalizaa nilivaa nguo zangu na kunisindikiza hadi nyumbani, tulipokaribia kufika tulisimama na Helena alinipatia kipande cha ngozi kama alichonipa Sabina. Shija nakuomba ngozi hii usiitupe, hakikisha muda wote unakuwa nayo, iweke pembeni wakati wa kuoga tu, zaidi ya hapo hakikisha ipo mwilini mwako.
Nakwambia hivyo kwa kujua kipindi hiki ni kibaya kuliko chochote kilichotokea. Sasa hivi wachawi hawana pingamizi lolote watafanya watakavyo , hivyo hii ngozi ndiyo kinga yako kipindi hiki cha kujiandaa na mtihani, ukimaliza tu nakuomba uende mjini kwa mjomba wako.
Nimekuelewa Helena, nashukuru sijui bila wewe leo ningekuwa katika hali gani, kwani muda huu ni saa ngapi? Nilipokea kipande cha ngozi na kuuliza. Inakimbilia saa nane za usiku. Mungu wangu! Sijui nyumbani wamenitafuta sana.
Lazima watakuwa wamekutafuta . Sijui nitawajibu nini, lakini nimekumbuka nitawaeleza kuwa nililala kwa rafiki yangu kwa ajili ya kujisomea. Na haya makovu? Mmh, hapo sasa sijui nitawadanganya vipi?
Sasa, sikiliza wakikuuliza waeleze mlikwenda kucheza mpira wakati wa kurudi aliangukia shimoni ndipo rafiki zako walipokusindikiza , mlipofika usiku ulikuwa mkubwa uliingia chumbani kwako kulala.
Mmh! Sidhani kama watanielewa . Basi kapumzike usiku mkubwa, nina imani bado wanakutafuta mwisho watakuja kwako usiogope hawawezi kukuona. Nashukuru Helena. Nilitaka kusahau nakuomba usiwaeleze chochote wazazi wako. Nitafanya hivyo .
Niliagana na Helena kwa kuingia ndani kulala, wasiwasi wangu mkubwa nilijiuliza nitaweza kulala kwa kuhofia maumivu ya mwili. Lakini haikuwa hivyo , nilipogusa ubavu tu usingizi mzito ukanichukua. Nilishtuka siku ya pili pale nilipoamshwa na sauti ya baba.
Niliamka kwa kuhofia maumivu, sehemu kubwa ya mwili ulikuwa na maumivu madogo, kasoro kwenye goti kulikuwa na maumivu makali yaliyonifanya nitembee kwa kuchechemea. Baba aliponiona alishtuka. Vipi tena? Ajali baba. Ya nini na imetokea saa ngapi? Nilidondokea kwenye shimo wakati wa kurudi nyumbani, kutokana na giza sikuweza kuliona na kupoteza fahamu kwa muda.
Mungu wangu! Lakini mchezo wa kutembea usiku umeuanza lini Shija? Imetokea tu baba, roho haikunipa kulala kule kwa kuwa sikuaga. Siku ya pili hata kama hukuaga, lala hukohuko mpaka asubuhi usitembee usiku ni mbaya sana, ona sasa yaliyokukuta , unafikiri ungekufa nani angejua? Samahani baba, nimekuelewa.
Na umerudi saa ngapi? Sikujua ni muda gani ila ulikuwa usiku sana. Ona sasa, sisi tulifikiri utalala kwa rafiki zako kujisomea, kumbe umekumbwa na masahibu mazito. Ni kweli nilitaka kulala, lakini sikuaga niliamua kurudi japo usiku. Mama naye alikuja kunijulia hali na kuniasa kwamba nisitembee usiku,
nilimkubalia huku bado nikificha siri moyoni mwangu.
Sikuweza kwenda shule kutokana na jeraha la goti lililokuwa likiniuma sana. Ilibidi nitafutiwe mti wa kutembelea. Baada ya wazazi kuondoka nilibakia peke yangu nyumbani, kutokana na kuhisi uchovu, nilirudi chumbani na kujilaza. Niliwaza mengi kutokana na kupoteza mfuko wangu wa shule na kiatu kimoja.
Kiatu hakikuniuma sana japo hali yetu ya kujikongoja ilinikatisha tamaa kukipata haraka. Kilichoniuma sana ni counter book zangu zilizokuwa na notice nyingi nilizotumia kujisomea kila nilipopata muda. Nikiwa katika lindi la mawazo, sauti ya Helena alinizindua.
Shija...Shija. Helena. Abee, Helena aliitikia huku akisukuma mlango. Vipi Shija, umeamkaje? Sijambo ila jeraha la kwenye goti ndilo linanisumbua. Hebu, niliusogeza mguu karibu yake.
Nilipojaribu kujinyanyua na kutembea maumivu yalinifanya nishike ukuta. Basi Shija, pole eeh. Asante. Vipi wazazi wako umewambiaje? Nimewadanganya wameniamini. Ooh, afadhari, Helena alishusha pumzi ndefu. Vipi mbona hivyo ? Nilimuuliza baada ya kushusha pumzi kama ameshusha mzigo mzito.
Nilikosa usingizi juu ya maswali ya wazazi wako, nilijua wangekubana lazima ungesema ukweli. Helena, mpaka mzee Manoni anafariki nimebaki na siri nyingi ambazo wazazi wangu hawazijui, kama wangezijua, baba yangu angemkata mapanga mama yako. Ooh, asante Shija kwa kuficha siri hizo.
Helena huu mguu ni wa kawaida au wa kichawi? Wa kawaida, wachawi hawakuwahi kukugusa, ila kuna dawa nitakuletea itakusaidia, ambayo hutumiwa na wachawi wanapopata majeraha kwenye kazi zao na wakiumia hupona kwa muda mfupi.
Nitashukuru, Helena nataka kusoma, nikikaa nyumbani nitapitwa na vitu vingi hata couter book zangu na kiatu kimoja vimepotea. Ooh kweli nilisahau, nilitaka kukuuliza jana kuhusu kiatu na mfuko wa madaftari. Kiatu sijui nilivuka wakati gani, ila mfuko wa madaftari niliutupa wakati nakimbia baada ya kuuona mzigo.
Basi hebu niachie hiyo kazi nitakutafutia nina imani kuwa asubuhi hii hakuna aliyeviokota . Vipi usiku hukutoka? Nilimuuliza. Shija hayo si muhimu kama kutafuta vitu vyako vya shule. Sawa. Baada ya mazungumzo Helena aliondoka huku nikiamini ni vigumu kuvipata vitu vile.
Nilijilaza kitandani kumsubiri, kutokana na uchovu usingizi ulinipitia, nilishtushwa tena na sauti ya Helena. Shija umelala? Si unajua uchovu vipi za huko? Nzuri vitu vyako nimevipata, wala sikupata shida kuviona, Helena alisema huku akiwa ameshikilia mfuko wa madafutari na kiatu. Ha! Siamini umevipata wapi? Ulipoviangushia
Kilichonishangaza kilikuwa ni mfuko wangu wa madaftari, ulikuwa mkavu pamoja tofauti na mvua ilivyonyesha . Helena mbona mfuko unaonesha kama hakukuwepo na mvua jana. Shija mbinu za kichawi huziwezi, hakukuwa na mvua yoyote zaidi ya kiini macho.
Baada ya kifo cha mzee Manoni wachawi wametangaza vita nzito na Shija, Je, Helena ataweza kumvusha salama?
INAENDELEA.....