NITAIBURUZA MAHAKAMANI BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU KWA UZEMBE WA KUTONIKATA MAKATO YA MAREJESHO YA SHAHADA NILIYOSOMA
Mimi Deogratius Kisandu, nasema kuwa; Yai ukililea vizuri litazaa Kuku lakini yaani Ukililea vibaya litazaa yai vinza. Kwanza kabisa natumia fursa hii kumshukru Mungu kusoma kwa miaka mitatu Shahada ya Elimu Maalum katika Chuo Kikuu Kishirki cha Sebastian Kolowa, Chini ya Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira (Sekuco), kwasasa kinaitwa Sebastian Kolowa Memorial University(Sekomu). Kwa kipindi chote cha masomo nimelipiwa na Bodi ya Mikopo elimu ya juu, nikipewa mkopo kwa 70% kipindi chote cha masomo kuanzia mwaka wa masomo 2009/2010 mpaka 2011/2012 ambapo nilihitimu huko Lushoto, Tanga.
Chakushangaza kila aliyeingia kwenye ajira alianza kukatwa mara moja na wengine walichelewa baada ya mwaka mmoja walianza kukatwa na hata Salary Slip zao zinaonesha kuwa wanakatwa tena hii ilikuwa ni automatic bila hata kupewa taarifa. Leo tunashangaa kutangaziwa kuwa tujisalimishe, kivipi ili hali kwasisi ambao ni watumishi wa Umma tayari majina yetu yapo kwenye system ya Utumishi na kwa mantiki hiyo, sisi hatuhusiki bali mwajiri wetu ndio anawajibika kwa kutokutoa taarifa ya watumishi wake kila mwaka katika bodi ya mikopo.
Mimi nachoshangaa, jina langu hata kwenye Orodha ya wadaiwa Sugu halimo na ilihali ninadaiwa na sijaanza kukatwa tangu nimalize chuo mwaka 2012, lakini wenzangu wanakatwa makato ya kurejesha mkopo bila hata kupewa taarifa yoyote. Kwanini jina langu lisionekane na wakati natakiwa kulipa mkopo au mnasubiri nikikaribia kustaafu ndio mtoe jina langu ili mje mnikate vizuri kwenye mafao ya kustaafia? Kwa hili natangaza rasmi kuishitaki Bodi ya Mikopo elimu ya juu mahakamani. Mimi sitajisalimisha Ofisi zao bali bodi itajisalimisha mahakamani, naendelea kutafta msaada wa kisheria zaidi ili kuweka mambo sawa. Namba yangu ya Chuo ni Sek/BedSN/130/09-KISANDU DEOGRATIUS PIO.
Kwa niaba ya wahangaa wenzangu nimejitoa sadaka kutetea Utu wa Watumishi wa Umma wanyonge tulionyongwa kifikra.
Deogratius Kisandu
Mwenyekiti wa Jukwaa la Walimu na Wanafunzi-Tanzania.
17/11/2016