Habari gani Watanzania wenzangu.
Naomba wadau mnisaidie ushauri wenu maana nipo njia panda. Mimi ni kijana umri miaka 30. Nina wanawake (mademu) wawili ambao nawapenda sana na kila mmoja ananipenda sana.
Kwakweli nimefanikiwa kuishi nao bila wao kujua kama ninawachanganya; nimedumu nao kwa miaka miwili sasa, na wote wananiamini sana na kila mmoja anaamini nitamuoa.
Sasa umefika wakati ambapo natakiwa nianze harakati za kuoa kama kumtambulisha mchumba kwa wazazi na kumchumbia. Napata wakati mgumu nimuache yupi na nimuoe yupi; wote ni wema sana kwangu na nakosa hata sababu ya ku-force ili nimuache mmoja
Wote ni wapole; nimesubiri mmoja anikosee nimuache lakini wapi, na ninapoelekea nakarbia kubambwa kwa ujinga niliowafanyia. Sasa nitumie kigezo gani kumuacha mmoja nibaki na mmoja nimuoe?
Naombeni msaada au nitumie kigezo gani ambao nitapata sababu ya kumuacha mmoja wao maana naona naaibika sio mda mrefuu.