Nipo njia panda

zimbo

New Member
Jul 1, 2010
2
0
Wadau naombeni ushauri wenu nipo njia panda,Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 29 sasa,nipo njia panda katika kutoa maaamuzi,nina wachumba wawili lakini sijui ni yupi nimchague awe mwenza wangu wa maisha, mmoja amenizidi umri yeye kwa sasa ana miaka 34.

Yeye tangu utotoni tulikuwa tunaishi jirani, tulizoeana sana kama kaka na dada na familia zetu zinajuana vizuri, kwa bahati nzuri mimi nilipokuwa masomoni nchini Africa ya kusini, na yeye pia alikuwa anafanya kazi nchini humo, kwa hiyo tukazidi kuwa marafiki, lakini mwaka 2007 tukajikuta tunaangukia kuwa wapenzi, kwa kweli tulipendana sana na kuzidi kuwa karibu sana, na kusema kweli huyo dada ni dada asiye na makuu na pia anajiheshimu sana,

Tuliendelea na mapenzi yetu mpaka mwaka 2008 mwishoni ambako mimi nilimaliza masomo yangu na yeye pia akawa anamaliza mkataba wake wa kufanya kazi nchini humo.wote tukarudi nyumbani Tanzania, lakini mimi mwanzoni wa 2009 nikapata nafasi ya kwenda USA kuendelea na masomo zaidi, na kumuacha yeye Tanzania kwa kuwa alikuwa anafanya kazi tayari.

Kwa bahati mbaya au sijui nzuri, nilipofika US kuna msichana mmoja ambaye alikuwa rafiki yangu high school Tanzania, mimi nilikuwa Shaban Robert na yeye alikuwa Mziziima , Yeye ana umri wa miaka 26.Alinipokea na kusema kweli huyo msichana nilimpenda sana tena sana tangu tulipokuwa high schoool japokuwa sikuwahi kumwambia,tukawa marafiki tena.

lakini katika huo urafiki wetu tukajikuta tunangukia kuwa wapenzi, kusema ukweli sijawahi kupenda kama ninavyompenda huyu msichana. na nakubali kuwa nilifanya kosa kubwa la kutomueleza ukweli kuwa mimi tanzania nimeacha mtu.

Lakini mwishoni wa 2009 yeye alimaliza shule na wazazi wake wakamtafutia kazi Tanzania kwa hiyo ikambidi aniache mimi nikimaliza masomo na yeye kurudi Tanzania, kwa matumaini ya kuwa nikimaliza na mimi nitarudi Tanzania tufunge pingu za maisha.Hapo ndio tatizo linapokuja, wote wawili wananisubiri nirudi, japokuwa yule wa kwanza haijawahi pita siku bila kunipigia simu, na pia najua ananipenda sana lakini naogopa naona amenizidi sana umri inaweza kuleta matatizo hapo baadaye.

Japokuwa yeye tunajuana vizuri sana nje ndani, na anajiheshimu sana tena sana na hata mama yake anajua mimi ndie mchumba wake pia uwa ananipigia simu naongea na mama yake pia , Lakini mimi nampenda sana huyu wa pili japokuwa huyu wa pili yeye inaweza pita hata siku tatu hajanipigia simu wala messegi, na pia naona kama yuko desperate sana na kuolewa, maana anataka kufanya mambo kwa haraka sana, mpaka nakuwa nahisi anaweza pata mtu huko nyumbani ambaye tayari ameshasettle akamuoa.

japokuwa naye mama yake ananijua mimi ndie mchumba wake na hata dada yake na kaka yake wanajua hilo,nilikuwa niiende tanzania likizo mwezi huu lakini nimearisha kwa kuogopa itakuwaje nikifika Tanzania maana wote wananisubiri, na huyu wa pili alitaka sana nije eti anitambulishe kwa wazazi wake na mimi nimtambulishe kwa ndugu zangu, hapo ndio roho yake itatulia maana kwa sasa hana uhakika kama mimi ni wake kweli.

Na juzi huyu wa pili kanipigia simu anasema kwa kuwa siendi Tanzania yeye atakuja huku US mwezi wa tisa ili eti nimpe mimba then tuwe na kitu ambacho kitatufanya tuwe pamoja.Na yule dada wa kwanza naye anataka kuja huku x-mas japokuwa yeye ajasema kama anataka mimba au lah ila nahisi naye ni hilo hilo anataka, sasa hapo ndio maisha yangu yanapokuwa magumu mpaka nakosa raha naombeni sana ushauri wenu wadau tafadhari japokuwa najua mimi ndie nimejitakia yote hayo lakini naombeni ushauri, yupi ananifaa kati ya hao nichukue uamuzi?​
 
Wadau naombeni ushauri wenu nipo njia panda,Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 29 sasa,nipo njia panda katika kutoa maaamuzi,nina wachumba wawili lakini sijui ni yupi nimchague awe mwenza wangu wa maisha, mmoja amenizidi umri yeye kwa sasa ana miaka 34.Yeye tangu utotoni tulikuwa tunaishi jirani, tulizoeana sana kama kaka na dada na familia zetu zinajuana vizuri, kwa bahati nzuri mimi nilipokuwa masomoni nchini Africa ya kusini, na yeye pia alikuwa anafanya kazi nchini humo, kwa hiyo tukazidi kuwa marafiki, lakini mwaka 2007 tukajikuta tunaangukia kuwa wapenzi, kwa kweli tulipendana sana na kuzidi kuwa karibu sana, na kusema kweli huyo dada ni dada asiye na makuu na pia anajiheshimu sana,Tuliendelea na mapenzi yetu mpaka mwaka 2008 mwishoni ambako mimi nilimaliza masomo yangu na yeye pia akawa anamaliza mkataba wake wa kufanya kazi nchini humo.wote tukarudi nyumbani Tanzania, lakini mimi mwanzoni wa 2009 nikapata nafasi ya kwenda USA kuendelea na masomo zaidi, na kumuacha yeye Tanzania kwa kuwa alikuwa anafanya kazi tayari,Kwa bahati mbaya au sijui nzuri, nilipofika US kuna msichana mmoja ambaye alikuwa rafiki yangu high school Tanzania, mimi nilikuwa Shaban Robert na yeye alikuwa Mziziima , Yeye ana umri wa miaka 26.Alinipokea na kusema kweli huyo msichana nilimpenda sana tena sana tangu tulipokuwa high schoool japokuwa sikuwahi kumwambia,tukawa marafiki tena, lakini katika huo urafiki wetu tukajikuta tunangukia kuwa wapenzi, kusema ukweli sijawahi kupenda kama ninavyompenda huyu msichana. na nakubali kuwa nilifanya kosa kubwa la kutomueleza ukweli kuwa mimi tanzania nimeacha mtu.Lakini mwishoni wa 2009 yeye alimaliza shule na wazazi wake wakamtafutia kazi Tanzania kwa hiyo ikambidi aniache mimi nikimaliza masomo na yeye kurudi Tanzania, kwa matumaini ya kuwa nikimaliza na mimi nitarudi Tanzania tufunge pingu za maisha.Hapo ndio tatizo linapokuja, wote wawili wananisubiri nirudi, japokuwa yule wa kwanza haijawahi pita siku bila kunipigia simu, na pia najua ananipenda sana lakini naogopa naona amenizidi sana umri inaweza kuleta matatizo hapo baadaye,Japokuwa yeye tunajuana vizuri sana nje ndani, na anajiheshimu sana tena sana na hata mama yake anajua mimi ndie mchumba wake pia uwa ananipigia simu naongea na mama yake pia , Lakini mimi nampenda sana huyu wa pili japokuwa huyu wa pili yeye inaweza pita hata siku tatu hajanipigia simu wala messegi, na pia naona kama yuko desperate sana na kuolewa, maana anataka kufanya mambo kwa haraka sana, mpaka nakuwa nahisi anaweza pata mtu huko nyumbani ambaye tayari ameshasettle akamuoa, japokuwa naye mama yake ananijua mimi ndie mchumba wake na hata dada yake na kaka yake wanajua hilo,nilikuwa niiende tanzania likizo mwezi huu lakini nimearisha kwa kuogopa itakuwaje nikifika Tanzania maana wote wananisubiri, na huyu wa pili alitaka sana nije eti anitambulishe kwa wazazi wake na mimi nimtambulishe kwa ndugu zangu, hapo ndio roho yake itatulia maana kwa sasa hana uhakika kama mimi ni wake kweli,Na juzi huyu wa pili kanipigia simu anasema kwa kuwa siendi Tanzania yeye atakuja huku US mwezi wa tisa ili eti nimpe mimba then tuwe na kitu ambacho kitatufanya tuwe pamoja.Na yule dada wa kwanza naye anataka kuja huku x-mas japokuwa yeye ajasema kama anataka mimba au lah ila nahisi naye ni hilo hilo anataka, sasa hapo ndio maisha yangu yanapokuwa magumu mpaka nakosa raha naombeni sana ushauri wenu wadau tafadhari japokuwa najua mimi ndie nimejitakia yote hayo lakini naombeni ushauri, yupi ananifaa kati ya hao nichukue uamuzi?​

Ndugu, vipi ungeihariri mada yako na kuiweka ktk aya ili iweze kusomeka vizuri?
 
Kwanza hukufanya vyema kuwa na uhusiano na mtu mwingine ilhali umeacha mpz wako Tz au bora unegesema ukweli kuwa muwe company ila una mtu wako..
Mwamuzi wa mwisho ni wewe kwenye jambo hili,uwe na hekma ya kuchagua mana upo njia panda..dada wa miaka 34 ningeona uwe nae,ulianza kuwa nae na unampenda japo siyo sana kama wa yule mwenye 26..miaka siyo kitu,labda tu wewe kama umempenda zaidi mwingine..
Tusipende kuwapa watu matumaini ya kuwaoa/olewa wakati ni uongo,unazibia wengine bahati zao..Maisha yenyewe mafupi!
 
Kaa chini uamue ni nani kati ya hawa wawili unayempenda sana. Kama ulivyoandika ni huyo wa pili na tena yeye ndiye mwenye umri mdogo hivyo biological clock yake bado ina muda mrefu kabla haijaanza kutick kuelekea ukingoni.

Ni mtihani mgumu kuwemo katika hali kama hii lakini kwa maoni yangu inatakiwa ufanye uamuzi haraka. Kila la heri. Ingekuwa raha sana kama ungeweza kuwaoa wote wawili, lakini hilo haliwezekani.
 
Japokuwa wengi wanasema umri sio kitu, mimi bado napinga mvulana kuoa msichana aliyemzidi umri. Nakushauri mdogo wangu uwe naye huyu wa miaka 26 ambaye umri unawiana na wa kwako wa miaka 29. Hayo ni mawazo yangu tu lakini pia uamuzi ni wako maana wanasema mapenzi hayachagui hata ukimpata msichana sijui mama wa miaka 50 ni poa tu.
 
.........Una wachumba wawili, it means wote hao umeshapeleka posa?Unajua lakini maana ya uchumba?
Mie nadhani hawa ni GF zako na si wachumba.Ungefikia stage ya uchumba ungekuwa na mmoja tu.

........Huyo wa miaka 26 nadhani hajatulia, hadi anataka kujishikisha mimba kwa ajili mje mfunge ndoa...........mhhhhhhh!! Mie ananitia mashaka mbona ana kihere here sana cha kuolewa?Ila mwenyewe umesema hapo ndipo moyo wako ulipo hivyo mkaka wewe mwenyewe chagua pumba na mchele hapo.

......Huyu wa 34 nahisi mtulivu japo umri umekwenda lakini hakupigii kelele za ndoa, na wewe ndio unamfahamu vizuri unasema hana makuu na anajiheshimu........umri sioni tatizo sana kama kweli umempenda, japo inapendeza mwanaume kumzidi mwanamke kiumri.Huyu wa 34 naona kama anafaa japo wewe naona kama humpendi kivileeeeeee!!

Hebu jarbu kuwa mkweli kwa hao wadada, kama mtu huna future naye nafuu tu umwambie ukweli mapema kuliko kumpotezea mtu bahati yake utakuta anapendwa na wengine huko lakini wewe unamletea mizengwe na wakati huna future naye.
 
Wadau naombeni ushauri wenu nipo njia panda,Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 29 sasa,nipo njia panda katika kutoa maaamuzi,nina wachumba wawili lakini sijui ni yupi nimchague awe mwenza wangu wa maisha, mmoja amenizidi umri yeye kwa sasa ana miaka 34.​



Yeye tangu utotoni tulikuwa tunaishi jirani, tulizoeana sana kama kaka na dada na familia zetu zinajuana vizuri, kwa bahati nzuri mimi nilipokuwa masomoni nchini Africa ya kusini, na yeye pia alikuwa anafanya kazi nchini humo, kwa hiyo tukazidi kuwa marafiki, lakini mwaka 2007 tukajikuta tunaangukia kuwa wapenzi, kwa kweli tulipendana sana na kuzidi kuwa karibu sana, na kusema kweli huyo dada ni dada asiye na makuu na pia anajiheshimu sana,​

Tuliendelea na mapenzi yetu mpaka mwaka 2008 mwishoni ambako mimi nilimaliza masomo yangu na yeye pia akawa anamaliza mkataba wake wa kufanya kazi nchini humo.wote tukarudi nyumbani Tanzania, lakini mimi mwanzoni wa 2009 nikapata nafasi ya kwenda USA kuendelea na masomo zaidi, na kumuacha yeye Tanzania kwa kuwa alikuwa anafanya kazi tayari.​

Kwa bahati mbaya au sijui nzuri, nilipofika US kuna msichana mmoja ambaye alikuwa rafiki yangu high school Tanzania, mimi nilikuwa Shaban Robert na yeye alikuwa Mziziima , Yeye ana umri wa miaka 26.Alinipokea na kusema kweli huyo msichana nilimpenda sana tena sana tangu tulipokuwa high schoool japokuwa sikuwahi kumwambia,tukawa marafiki tena.​

lakini katika huo urafiki wetu tukajikuta tunangukia kuwa wapenzi, kusema ukweli sijawahi kupenda kama ninavyompenda huyu msichana. na nakubali kuwa nilifanya kosa kubwa la kutomueleza ukweli kuwa mimi tanzania nimeacha mtu.​

Lakini mwishoni wa 2009 yeye alimaliza shule na wazazi wake wakamtafutia kazi Tanzania kwa hiyo ikambidi aniache mimi nikimaliza masomo na yeye kurudi Tanzania, kwa matumaini ya kuwa nikimaliza na mimi nitarudi Tanzania tufunge pingu za maisha.Hapo ndio tatizo linapokuja, wote wawili wananisubiri nirudi, japokuwa yule wa kwanza haijawahi pita siku bila kunipigia simu, na pia najua ananipenda sana lakini naogopa naona amenizidi sana umri inaweza kuleta matatizo hapo baadaye.​

Japokuwa yeye tunajuana vizuri sana nje ndani, na anajiheshimu sana tena sana na hata mama yake anajua mimi ndie mchumba wake pia uwa ananipigia simu naongea na mama yake pia , Lakini mimi nampenda sana huyu wa pili japokuwa huyu wa pili yeye inaweza pita hata siku tatu hajanipigia simu wala messegi, na pia naona kama yuko desperate sana na kuolewa, maana anataka kufanya mambo kwa haraka sana, mpaka nakuwa nahisi anaweza pata mtu huko nyumbani ambaye tayari ameshasettle akamuoa.​

japokuwa naye mama yake ananijua mimi ndie mchumba wake na hata dada yake na kaka yake wanajua hilo,nilikuwa niiende tanzania likizo mwezi huu lakini nimearisha kwa kuogopa itakuwaje nikifika Tanzania maana wote wananisubiri, na huyu wa pili alitaka sana nije eti anitambulishe kwa wazazi wake na mimi nimtambulishe kwa ndugu zangu, hapo ndio roho yake itatulia maana kwa sasa hana uhakika kama mimi ni wake kweli.​


Na juzi huyu wa pili kanipigia simu anasema kwa kuwa siendi Tanzania yeye atakuja huku US mwezi wa tisa ili eti nimpe mimba then tuwe na kitu ambacho kitatufanya tuwe pamoja.Na yule dada wa kwanza naye anataka kuja huku x-mas japokuwa yeye ajasema kama anataka mimba au lah ila nahisi naye ni hilo hilo anataka, sasa hapo ndio maisha yangu yanapokuwa magumu mpaka nakosa raha naombeni sana ushauri wenu wadau tafadhari japokuwa najua mimi ndie nimejitakia yote hayo lakini naombeni ushauri, yupi ananifaa kati ya hao nichukue uamuzi?​

...Atayekufaa ni huyo mnayependana. Huyo unayempenda atakusumbua bro.
Uamuzi wa mwisho ni wako.
 
.........Una wachumba wawili, it means wote hao umeshapeleka posa?Unajua lakini maana ya uchumba?
Mie nadhani hawa ni GF zako na si wachumba.Ungefikia stage ya uchumba ungekuwa na mmoja tu.

........Huyo wa miaka 26 nadhani hajatulia, hadi anataka kujishikisha mimba kwa ajili mje mfunge ndoa...........mhhhhhhh!! Mie ananitia mashaka mbona ana kihere here sana cha kuolewa?Ila mwenyewe umesema hapo ndipo moyo wako ulipo hivyo mkaka wewe mwenyewe chagua pumba na mchele hapo.

......Huyu wa 34 nahisi mtulivu japo umri umekwenda lakini hakupigii kelele za ndoa, na wewe ndio unamfahamu vizuri unasema hana makuu na anajiheshimu........umri sioni tatizo sana kama kweli umempenda, japo inapendeza mwanaume kumzidi mwanamke kiumri.Huyu wa 34 naona kama anafaa japo wewe naona kama humpendi kivileeeeeee!!

Hebu jarbu kuwa mkweli kwa hao wadada, kama mtu huna future naye nafuu tu umwambie ukweli mapema kuliko kumpotezea mtu bahati yake utakuta anapendwa na wengine huko lakini wewe unamletea mizengwe na wakati huna future naye.

I am in agreement with you Pretty....

Inaonekana mapenzi na huyu demu wa kwanza anafanya kwa kujificha kwa sababu demu anamzidi umri, anataka young blood.... kwa hiyo hawezi kumuoa huyu dada wa kwanza... Ni Bora amwambie kuliko kumpotezea wakati...
 
Pole sana ......Ni kweli umeamua kuoa au unatania???
Ngoja nipate B/fast nitarudi hapa baadae
 
26 ni muda mzuri wa kuolewa na ndio maana huyu anatamani kuolewa ila huyu wa 34 kwako wewe 29!!!! penzi lenu litakuwa la muda mfupi, baadae utaanza kukumbizana na dogodogo tuuu
hayo ni maoni yangu tu ila uamuzi wa mwisho unao wewe mwenyewe.
 
hili ni tatizo la wanaume wengi sana...wanakuwa kwenye mahusiano na wanawake wengi,wanawapotezea muda na mwisho wa siku anamwambia kuwa basi amepata mwingine.ushauri wangu ni huu
!> huyo wa kwanza,yawezekana unachofeel kwake si mapenzi,kama ulivyosema,mmekua wote na mlichukuliana kama kaka na dada,na ndio maana mlipokuwa S.A. mlikuwa jirani mno,na kama ilivyo kawaida,mwanaume na mwanamke hawawezi ishi pamoja bila kuwa na phyisical attraction sexually,ukizingatia sio ndugu yako,na ndicho kilichotokea hapo.mkajikuta mnakula tunda la ndoa...lakini kwa kweli sidhani kama ur real in love,hata huyo msichana anachokihisi kwako si real love,ni ukaribu tu.atakuja jua baadae.

2>huyo wa pili nafikiri is where ur heart belongs...na kama umesema tangu high school ulikuwa unampenda,na kwa kuwa kwenu karibu U.S ndio kumewafanya mkaingia mapenzini motomoto.kuhusu swala la kutaka mtoto,sidhani kama ni tatizo.wasichana wengi hawako secure kwenye relationship,wanafikiri wanaume wanawadanganya,hasa kama she is real in love,she can do anything to have u,na ndicho kinachotokea kwa huyu msichana.anafikiri unaweza kupata msichana mwingine ukamwoa(hajui kuwa unae tayari,lol!).sasa ili ahakikishe kuwa unabaki kuwa wake anataka apate ujauzito...au huenda umemwonyesha dalili za kutokuwa mwaminifu.

3>asikudanganye mtu,umri matters,hasa kwa waafrica...na hasa kama ana umbo kubwa...baada ya muda,yeye ataanza kujiona mtu mzima zaidi,na mataanza kupishana kwa mambo mengi sana,ni vyema ukaoa mtu ambae umemzidi umri...ningeweza kumshauri huyu dada,hata yeye ningemshauri asiolewe na wewe kwa sababu ya umri!nakwambia ukweli,italeta shida baadae,huwezi kuona sasa hivi sababu ya hicho unachokiita mapenzi,ingawa bado nina wasiwasi.

ungekuwa unampenda kweli huyu wa kwanza,usingethubutu kuwa na huyu wa pili,lakini kwa vile upendo wenu ni ule wa kaka na dada ndio maana ikawa rahisi kuwa na huyu wa pili ambae alikuvutia tangu mapemma.uwe mwangalifu sana na uamuzi wako...either way,waambie ukweli wote wawili,na uchague mmoja,najua ataumia atakae achwa lakini ni afadhali kuliko kubaki kkimya.
 
kitanzi cha maisha huja taratibu sana
unakurupuka, mara yakikushinda ndo unaanza kuomba ushauri.
deep down in your heart umeamua kuoa?

usipokiwa makini utakuwa mtu wa kunung'unika maisha yako yote, kaa chini tafakari kwa kina juu ya hatima ya maisha yako
 
pole sana, ni kweli umejitakia hayo mwenyewe kwa kuwa na wapenzi wawili na kuwapa matumaini ya ndoa wote.

kwa maelezo yako huyo mchumba mkubwa ndie anaekufaa, na umeshampotezea muda mwingi na bahati nyingi kwani kama ulivyosema ametulia hana makuu anakusubiri wewe.

kwa upande mwingine huyu dogo inaelekea hukumpenda kwa dhati bali kwa umri wake mdogo atakua anakufanyia vile vitu ambavyo huyu mkubwa hajafanya au anakupagawisha ndio maana unafikiri umempenda sana. hebu jaribu kumwambia huko tayari kwa ndoa sasa hivi uone kama atakuwa nawe tena. tena mwambie sasa hivi kabla hajaja huko kuchukua mimba!

usichukue umri kama kisingizio, nina rafiki yangu ambae wazazi wake baba ni mdogo na mama ni mkubwa kiumri lakini ndoa yao ya miaka zaidi ya 40 natamani yangu ingekua na upendo au ustaarabu kama yao.

Mshirikishe Mungu katika maamuzi yako kwani mke mwema ni zawadi kutoka kwa Mungu. kila la kheri
 
Sijajua wakati unafanya hayo ulikuwa unawaza nini hatima yake ...umeyakoroga
Cha msingi hapo ni wewe na moyo wako ndio mwamuzi tunaweza kuongea mengi na kuandika page zaidi ya kumi mwisho wa siku uamuzi wako ndio muhimu katika future yako.
Katika uchaguzi wako usiangalie umri kuna watu wanajipenda sana unamkuta ana 40 yrs ukadhani 30 ni mambo ya kujimake tu.
Ila hako katoto ka 26 kanakotaka mimba kabla ya ndoa kana hatari kweli.
1. Ni dhambi kwa mungu
2. Kakibeba hiyo mimba kisha usikaoe itakuwaje ?
Kuwa muwazi na mkweli kwa hao kina dada
Piga magoti mshirikishe mungu wako jibu utalipata .....
 
jamani naona peke yangu au hii kitu iko kinyume nyume?!

sioni jamaa alipochukua jukumu la kufika hapo alipo .................lawama zote kazivurumisha kwa PENZI.

ati alipendana na wa kwanza, kisha akampenda wa pili........

sidhani kama wewe uko tayari kuoa ....
 
jamani naona peke yangu au hii kitu iko kinyume nyume?!

sioni jamaa alipochukua jukumu la kufika hapo alipo .................lawama zote kazivurumisha kwa PENZI.

ati alipendana na wa kwanza, kisha akampenda wa pili........

sidhani kama wewe uko tayari kuoa ....

Huyu ni MTONGOZAJI na sio MUOAJI
 
Back
Top Bottom