Habarini wana jamvi?Naitwa Nicholas naishi morogoro,nashughulika na biashara na ufugaji.Kifupi ni kwamba nimepata tatizo katika kuku wa nyama niliowachukua kutokakampuni ya interchick kupitia wakala wao hapa morogoro ambao ni duka la madawa linaitwa Imuka.Yaani hadi sasa bandani kwangu kuku zaidi ya 50 wanakufa ovyo na hao kuku nimejaribu kuwachunguza sijaona ugonjwa wowote.
Ilinibidi niende duka nililochukulia vifaranga wao wanachonijibu ni kuwa inaonekana batch tuliochukua haikuwa sawa kwani tayari kuna wenzangu zaidi ya watano wameripoti tatizo kama hilo.Mimi nilichukua tarehe 25 mwezi wa nane yaani hadi leo hao kuku wana wiki mbili... Nitaendelea kesho.
Naendelea, Sasa nahitaji kupata angalau namba ya hawa jamaa wa interchick kwani nikiwapigia kwa simu yao ya ttcl hawapokei na hii hali si mimi peke yangu kuna wafugaji wenzangu wengi wameathirika na tatizo hili.Nachoshangaa ni kuwa kwa nini tatizo linalotokana na kampuni lituathiri sisi wafugaji hasa sisi ambao ni wadogo.?
Hadi sasa bandani kwangu tayari kuku 123 pamoja na wale 50 wa mwanzo na nilichukua kuku 150.Kwa stahili hii tutafanikiwa kupigana na umaskini na kuenda na kasi ya maendeleo tunayoyataka?
Ninachoomba cha ziada ni ushauri wa nini cha kufanya kuhusiana na hili au kama kuna muwakilishi wa kampuni hii tuwasiliane kwa namba hii 0719974886
Ilinibidi niende duka nililochukulia vifaranga wao wanachonijibu ni kuwa inaonekana batch tuliochukua haikuwa sawa kwani tayari kuna wenzangu zaidi ya watano wameripoti tatizo kama hilo.Mimi nilichukua tarehe 25 mwezi wa nane yaani hadi leo hao kuku wana wiki mbili... Nitaendelea kesho.
Naendelea, Sasa nahitaji kupata angalau namba ya hawa jamaa wa interchick kwani nikiwapigia kwa simu yao ya ttcl hawapokei na hii hali si mimi peke yangu kuna wafugaji wenzangu wengi wameathirika na tatizo hili.Nachoshangaa ni kuwa kwa nini tatizo linalotokana na kampuni lituathiri sisi wafugaji hasa sisi ambao ni wadogo.?
Hadi sasa bandani kwangu tayari kuku 123 pamoja na wale 50 wa mwanzo na nilichukua kuku 150.Kwa stahili hii tutafanikiwa kupigana na umaskini na kuenda na kasi ya maendeleo tunayoyataka?
Ninachoomba cha ziada ni ushauri wa nini cha kufanya kuhusiana na hili au kama kuna muwakilishi wa kampuni hii tuwasiliane kwa namba hii 0719974886