Nini siri ya baadhi ya watu kutozeeka mapema?

Nini siri ya baadhi ya watu kutozeeka mapema?

Nilipata muda wa kwenda kutembea katika moja ya shule nilizosoma ambapo ni takriban miaka 9 sasa toka niondoke hapo.

Kuna watu nimewakuta hapo ambao niliwaacha walinishangaza sana, wamebadilika miaka tu lakini kimuonekano wako vile vile kama nilivyowaacha miaka 9 nyuma na kuna wengine wamezeeka na mvi kibao.

Nilipata shauku ya kutaka kujua siri iliyopo ila muda haukuwa rafiki kwangu hivyo nimeona sio mbaya kuuliza kwenu wakuu sababu ni nini, ni vitu vya kurithi ama kuna namna mtu anaweza ishi ikamfanya awe hivyo?
Kila m2 ana kaumbwa kwa udongo wake!!! kama wewe udongo wako umetolewa kando ya mto utai kuzeeka manke ni teketeke!!!! kama udongo wako ni mfinyanzi utachelewa kidogo kuzeeka,lakini kama udongo wako umetolewa kwenye kichuguu kama MIMI au PUTIN!! hauzeeki kamwe!!
 
Kuna huyo babu toka miaka ya 1998 nipo katoto yuko vile vile mpaka leo, sasa mama yangu ambae ana miaka 50+ anakwambia huyo babu yupo hivyo hivyo toka wao bado wadogo. Mpaka leo hajabadilika chochote na anatembea vizuri tuu kweli Mungu kweli wa ajabu na kambariki sana.
Vp na bakora bado anatembeza?
 
Nadhani stress inachangia sana kuzeesha!
Wazaramo na wakwere wana lifestyle flani simple sana, yani hawajali chochote .nimewaona wengi wakipata umri mkubwa bila kubadilika miili wala kupata mvi.
 
Acheni kuwadanganya watu. Mtu asile wanga ale nini nchi hii ? Hizo mboga za majani unazoshobokea ni kemikali tupu ! Ule wanga, usile kufa utakufa tu.
Ukiamua kula kemikali ni ww na uzembe wako,
 
Vp na bakora bado anatembeza?
Kwa hilo sijui mkuu, ila toka miaka hiyo sijawahi kujua kama ana mke wala mtoto huwa tunamwona yeye tuu. Sijui story of his life ila i hope ana familia yake.
 
Mkuu usikubali kujenga nyumba bila kuacha eneo Kwa ajili ya organic garden,wenzako mboga na matunda tuliacha kununua.
Je, hilo eneo lako la bustani linaweza stawisha matunda yote ? Maana matunda huenda kwa msimu kama mnyororo, kuna msimu wa maembe, msimu wa machungwa, msimu wa nanasi, msimu wa tikitimaji. Je, matunda yote unayo kwenye bustani yako ?
 
Jana nlipanda bodaboda, nikamwamkia boda,, akaanza kulalama ye bado mdogo anamiaka 32,
Nikamshangaa sana, muonekano wake anaonekana yuko 40+

Akanisimulia kwamba alipata stroke,, nikampa pole,, leo sijamwamkia nimempa habar ya asubuh chief,, kafurai sana [emoji23]

Anavaa na kofia mda wote, nahisi ana mvi pia,,
 
Je, hilo eneo lako la bustani linaweza stawisha matunda yote ? Maana matunda huenda kwa msimu kama mnyororo, kuna msimu wa maembe, msimu wa machungwa, msimu wa nanasi, msimu wa tikitimaji. Je, matunda yote unayo kwenye bustani yako ?
Bustani yangu Ina mboga karibia 70%ya mboga zinazopatikana sokoni,Nna miti ya maembe,miparachichi na mipapai,na migomba,Matunda mengine ikitokea nayahitaji basi nayanunua!mfano mapasheni,matunda damu Huwa nanunua.
Ukiwa na bustani Yako unapunguza kiwango Cha Kula makemikali na sumu.
 
img_1_1692036340389.jpg
 
Jana nlipanda bodaboda, nikamwamkia boda,, akaanza kulalama ye bado mdogo anamiaka 32,
Nikamshangaa sana, muonekano wake anaonekana yuko 40+

Akanisimulia kwamba alipata stroke,, nikampa pole,, leo sijamwamkia nimempa habar ya asubuh chief,, kafurai sana [emoji23]

Anavaa na kofia mda wote, nahisi ana mvi pia,,
[emoji3][emoji3]
 
Acheni kuwadanganya watu. Mtu asile wanga ale nini nchi hii ? Hizo mboga za majani unazoshobokea ni kemikali tupu ! Ule wanga, usile kufa utakufa tu.
Panda Bustani kwa sámadi,njoo uchagani tukufundishe[emoji3] au tembelea makazi yoyote ya mchaga popote kama utakosa Bustani
 
Panda Bustani kwa sámadi,njoo uchagani tukufundishe[emoji3] au tembelea makazi yoyote ya mchaga popote kama utakosa Bustani
Umembiwa sina bustani baba. Ndiyo tatizo lako rafiki yangu huwa unakurupuka sana. Hata hivyo unavyo huko uchaggani lakini auishi huko. Unasubiri ufe ukazikwe huko. Si ajabu muda huu uko Lindi au Simiyu
 
Back
Top Bottom