Nini maana ya mchamaago?

abrisalim

Member
May 17, 2011
35
7
kuna msemo usemao
"Mchamaago hanyele huenda akwiya tena"
Msemo huu wa kiswahili unatumika tokaenzi ya mababu namababu lakini wengi wetu hatujui maana ya maneno yaliyotumika. Nawaombeni wakuu mtueleze maana ya maneno yafuataya:
Mchamaago,
Hanyele,
Akawiya.
Naomba kila neno litungiwe sentensi ili tujue vipi kulitumia.
 
Wengine husema MCHAMAAGO HANYELE HWENDA AKAWIA PAPO..............
maana : anaehama /anaendoka sehemu asitukane (kufanya mambo mabaya) pengine atarudi tena papo hapo
 
kuna msemo usemao
"Mchamaago hanyele huenda akwiya tena"
Msemo huu wa kiswahili unatumika tokaenzi ya mababu namababu lakini wengi wetu hatujui maana ya maneno yaliyotumika. Nawaombeni wakuu mtueleze maana ya maneno yafuataya:
Mchamaago,
Hanyele,
Akawiya.
Naomba kila neno litungiwe sentensi ili tujue vipi kulitumia.

Mimi ninvyojua ni "Mchama ago hanyeli,huenda akauya papo".

Mchama ago (msafiri aliyeweka kambi mahala fulani katika safari yake) hanyeli (hanyi hapo kambini kwa sababu anaondoka - i.e. hafanyi mabaya) huenda (kuna uwezekano) akauya (akarudi) papo (hapo hapo kwenye kambi aliyoweka mwanzo).
 
Mimi ninvyojua ni "Mchama ago hanyeli,huenda akauya papo".

Mchama ago (msafiri aliyeweka kambi mahala fulani katika safari yake) hanyeli (hanyi hapo kambini kwa sababu anaondoka - i.e. hafanyi mabaya) huenda (kuna uwezekano) akauya (akarudi) papo (hapo hapo kwenye kambi aliyoweka mwanzo).

Haya maneno yana falsafa kubwa sana, wanyamwezi nao wanamsemo kama huo igogo lya hakaya likashenyentelegwa ikiwa na maana karibu sawa na hiyo.
 
Mimi ninvyojua ni "Mchama ago hanyeli,huenda akauya papo".Mchama ago (msafiri aliyeweka kambi mahala fulani katika safari yake) hanyeli (hanyi hapo kambini kwa sababu anaondoka - i.e. hafanyi mabaya) huenda (kuna uwezekano) akauya (akarudi) papo (hapo hapo kwenye kambi aliyoweka mwanzo).
Asante mkuu SMU.umetufafanulia vizuri sana.
 
Mkuu Ecoli kama ulivosema: Haya maneno yana falsafa kubwa sana, wanyamwezi nao wanamsemo kama huo igogo lya hakaya likashenyentelegwa ikiwa na maanakaribu sawa na hiyo.
 
Mimi ninvyojua ni "Mchama ago hanyeli,huenda akauya papo".

Mchama ago (msafiri aliyeweka kambi mahala fulani katika safari yake) hanyeli (hanyi hapo kambini kwa sababu anaondoka - i.e. hafanyi mabaya) huenda (kuna uwezekano) akauya (akarudi) papo (hapo hapo kwenye kambi aliyoweka mwanzo).

Daah!! Ahsante sana mkuu, hii methali imenisumbua tangu muda mrefu sana kuitafsiri .
Leo nimeipata.
 
Mchama ago: anaeondoka ktk kambi au maeneo aliyokaa kwa muda na yakamsitiri nakumsaidia, HANYELE hapadharau au hapanyei kwakua ameshakidhi mahitaji yake, HWENDA AKAWIAPAPO: Huenda akarudi palepale pakamsitiri kuliko mwanzo,msemo huu unamaana kubwasanasanasana.nitafafanunua zaidi baadae.
 
Mimi ninvyojua ni "Mchama ago hanyeli,huenda akauya papo".Mchama ago (msafiri aliyeweka kambi mahala fulani katika safari yake) hanyeli (hanyi hapo kambini kwa sababu anaondoka - i.e. hafanyi mabaya) huenda (kuna uwezekano) akauya (akarudi) papo (hapo hapo kwenye kambi aliyoweka mwanzo).

wapendwa,

hii methali nimewahi kuifafanua kwenye thread fulani. ufafanuzi wa SMU ni sahihi kabisa, ila naomba nifafanue vizuri zaidi hapo kwenye wino mwekundu.

kuchamaa = kuchuchumaa
ago= mahali pafinyu (mfano pangoni ama chini ya mti mkubwa ulioinama) ambapo huwezi kusimama wima ama kujibanza ila kwa kuchuchumaa tu. mfano wa mtu aliyekumbwa na mvua kubwa akiwa porini aweza kukimbilia kwenye kapango kadogo kaliko karibu uli kujibanzxza pale na kujihifadfhi dhidi ya mvua hiyo kubwa.

sasa huyu aliyejibanza hapo pangoni kwa kujikunyata ama kuchuchumaa tu kutokana na ufinyu wa nafasi hapo pangoni, iwe ni kwa kujikinga na mvua, jua, baridi , wanyama wakali ama kulala wakati wa usiku nk, ndiye anayeitwa mchamaa ago! na ndiye tunayeambiwa hawezi kunya hapo maana huenda siku moja akapatwa na dharura nyingine na kujikuta akirudi kujihifadhi palepale.

mbarikiwe sana wapendwa.

Glory to God!
 
wapendwa,

hii methali nimewahi kuifafanua kwenye thread fulani. ufafanuzi wa SMU ni sahihi kabisa, ila naomba nifafanue vizuri zaidi hapo kwenye wino mwekundu.

kuchamaa =
kuchuchumaaago= mahali pafinyu (mfano pangoni ama chini ya mti mkubwa ulioinama) ambapo huwezi kusimama wima ama kujibanza ila kwa kuchuchumaa tu. mfano wa mtu aliyekumbwa na mvua kubwa akiwa porini aweza kukimbilia kwenye kapango kadogo kaliko karibu uli kujibanzxza pale na kujihifadfhi dhidi ya mvua hiyo kubwa.

sasa huyu aliyejibanza hapo pangoni kwa kujikunyata ama kuchuchumaa tu kutokana na ufinyu wa nafasi hapo pangoni, iwe ni kwa kujikinga na mvua, jua, baridi , wanyama wakali ama kulala wakati wa usiku nk, ndiye anayeitwa mchamaa ago! na ndiye tunayeambiwa hawezi kunya hapo maana huenda siku moja akapatwa na dharura nyingine na kujikuta akirudi kujihifadhi palepale.

mbarikiwe sana wapendwa.

Glory to God!

MCHAMA _ago, ni maneno mawili tofauti.
KUCHAMA ndio asili ya neno, maanayake ni kuhama na Ago ni kambi kama walivyoeleza wengine hapo juu.

MCHAMA NI KIWAKILISHI CHA MTU lakini neno hasa lilikua Kuchama.
 
Back
Top Bottom