Nini kitatokea endapo jua litazima/ litapotea?

Nini kitatokea endapo jua litazima/ litapotea?

Kwa hakika itakuwa giza muda wote na hapo ubinifu utaongezeka maradufu na mianga itagunduliwa.
 
Kaka jaribu kuelewa nilichokiandika,naposema huwezi kuona kilicho nyuma yako,hakuhitaji shule hapo ni kwamba hapo hapo ulipo kaa na ulipo elekea huwezi kuona kilcho nyuma yako.

Pili unajengea hoja juu ya movie huku ni kufikiri kimakosa. Nini asili ya movie ni maigizo kama maigizo mengine hupunguza katika ukweli na huongeza katika ukweli,kwahiyo hii si hoja dhidi ya kile nilicho kiandika.

Tuandike ukweli na uhalisia
..Wewe ndio hujaelewa naposema huu uzi ni wa ku-provoke critical thinking! Kufikiri, sky is the limit, kutenda kuna mipaka. Msingi wa hoja yako ni kwamba kuna mipaka ya kufikiri, mimi nimekupinga. Suala la kuona kilicho nyuma, iliposemekana haiwezekani kuona kama udaivyo, WALIFIKIRI na kuja na njia za kuweza kuona nyuma in real time.
 
Habari zenu.
Mimi mi mpenzi sana wa mambo ya intelligence. Ni mgeni kidogo humu jf upande wa kuwa member. Jukwaa hili ndio limenishawishi niweze kuwa member kamili ili niweze shiriki vizuri jukwaani.

Hivi ktk ulimwengu wetu huu, jua kama ndio chanzo cha gravity, nishati nk, ikatokea limezima ghafla, ulimwengu utakuwaje? Haswa hapa ktk dunia yetu, ni nini kitatokea?

Asanteni.
Jua likizima sasa hivi paap.

Hutakuwa na uwezo wa kujua hilo mpaka takriban dakika 8 na sekunde 20 zipite.

Utaendelea kuliona jua linawaka kwa dakika 8 na sekunde kama20 bila kuona tofauti yoyote.

Kwa sababu, huo ndio muda unaouchukua mwanga kusafiri kutoka kwenye jua mpaka kwenye jicho lako.

Ukiliangalia jua sasa hivi, hulioni kama jua lilivyo sasa hivi, unaliona jua kama lilivyokuwa dakika 8 na sekunde 20 zilizopita.

Kwa hiyo, muda wowote, hatuna uhakika kama jua lipo na linawaka, au limezimika.

Tunaweza kuwa na uhakika jua lilikuwepo na liliwaka takriban dakika 8 na sekunde 20 zilizopita tu.
 
Mitandaoni kuna maarifa mengi sana....lakini bahati mbaya vijana wetu wanasoma ili kufaulu mitihani
Kila kinachoandikwa ktk hili jukwaa (intelligence) kipo mitandaoni, unafikiri kwa nini hili jukwaa bado limewekwa hapa licha ya kuwa watu wanaweza wakaenda jichotea maarifa kimya kimya?
 
1. Wanasayansi watalikarabati au watatengeneza jua lingine.
Hii ni kwa mujibu wa watu wasiotambua uumbaji wa Mungu mwenyezi.
Kwamujibu wa tunaemwamini Mungu,
2. Jua haliwezi kufa wala kuharibika maana Mungua alilitrngeneza lituletee mwanga kuotesha mimea nk, hadi siku ya mwisho wa dunia ambapo Mungu atuondoa duniani na kwenda kuishi naye kwake mbinguni.
Chagua jibu moja hapo juu.
Bwana Yesu asifiwe.
 
Unaona kinachotokea North Pole kule ambapo miale ya jua haipafikii kwa sana basi iwapo jua litazima basi tegemea dunia nzima kuwa vile!. Kila kitu kitaganda na kwa kuwa Jua ndio chanzo cha uhai basi hakuna maisha yatakayo endelea kuwepo popote pale!.
Mwanga toka kwenye Jua kufika duniani unatumia dakika 8 na sekunde 19 ina maana kwa makadirio nayoona Jua likizimika ghafla ndani ya siku 3-5 Dunia itakua kimya yote!!..
Jua kuzima ghafla ni kitu kisichowezekana kabisa, Lakini labda likizimika tuwape moyo wachina watutengenezee copy ya Jua lao 😀🙂
View attachment 837457
Ingawa kwa maendeleo ya sayansi ya binadamu, wenzetu huko walishaweza kutengeneza kitu chenye mwanga (artificial sun) ingawa sio na nguvu kama Jua (ni kazi kulifikia joto lile ukasurvive lakini kina nguvu kuikaribia jua!).
View attachment 837460View attachment 837461
Scientists just switched on the world's largest 'artificial sun'
Hii artificial sun ikiwashwa inacover umbali gani?
 
..Wewe ndio hujaelewa naposema huu uzi ni wa ku-provoke critical thinking! Kufikiri, sky is the limit, kutenda kuna mipaka. Msingi wa hoja yako ni kwamba kuna mipaka ya kufikiri, mimi nimekupinga. Suala la kuona kilicho nyuma, iliposemekana haiwezekani kuona kama udaivyo, WALIFIKIRI na kuja na njia za kuweza kuona nyuma in real time.
Kaka bado hujaelewa mzee. Kupinga kwako kuwepo kwa mipaka ya kufikiri ni uchache wako wa elimu na maarifa.
 
Kaka bado hujaelewa mzee. Kupinga kwako kuwepo kwa mipaka ya kufikiri ni uchache wako wa elimu na maarifa.
Nimeelewa, tatizo ni wewe kutaka nifikirie kama wewe KUWA KUNA MIPAKA YA KUFIKIRI. Hii haiwezekani, nitabaki na msimamo wangu kuwa hakuna mipaka. Cha msingi ni logics, ila nimekuelewa.
 
Kwangu jua likizima, kitacho tokea ni kiza na mwanga hafifu na baridi isiyo pungua
Tukumbuke kuna chakula, ni mmea ule. Na mmea unahitaji mwanga wa Jua ili kujitengenezea chakula chake. Jua likitoweka mimea itashindwa katika ukuaji na itakufa, ikifa Hamna chakula.

Satellite nazo zitashindwa kufanya kazi, nguvu kazi yake inatokana na mionzi ya Jua.

Baridi itakuwa ni kubwa sana fikiria nchi kama Urusi,Korea kaskazini, Canada, sijui wataishije. Na baridi kwa ujumla wake ikitanda mfumo wa upumuaji wa binadamu unashindwa kufanya kazi vizuri. Watu wengi sana tutakufa kwa baridi, fikiria kama Makambako hali itakuaje. Dunia yote itakuwa ni barafu.
 
there will be no photosynthesis anymore, kwahiyo kutakua na mlundikano wa carbon dioxide na kutozalishwa kwa oxygen, hence death of living organisms will occur very fast due to lack of oxygen.
 
Itachukua kama dk 8 kabla watu hawajagundua kua jua halipo na itategemea hilo jua litapotea Kwa njia ipi na kama likitoweka basi kunauwezekano wa mabadiriko makubwa katika mwendokasi wa Dunia pia nafasi yake katika mzunguko.Refer universal law of gravitation kipi kitatokeo kama force itakuwa sawa na zero!?Dunia itaangukia anga za mbali kama haitogongana na sayari au magimba mengine pia inawezekana tukaishia kuvutwa na black bodies au tukajikuta kwenye solar system nyingine maana jua ni nyota na nyota zipo nyingi na kuna zero chance ya kiumbe yeyote kusalia kama hilo litatokea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom