Naona umeamua kubishana tu haya ngoja twende sawa
Kwa nyakati tofauti ndani ya east africa marais wa nchi hizi hasa uganda na kenya hawakuhi kusafiri kwenda nje wakati nchi zao zilipokuwa kwenye mchakato mgumu kabisa wa katiba ila hapa kwetu since mchakato huu uanzishwe rais kama amri jeshi mkuu kasafiri zaidi ya mara 10 na hilo nyie makada hamjaliona wala kulikemea kisa na mkasa kwa vile mmemeza kadi za uanachama
Rais alitangaza kuazisha mchakato wa katiba na pia alipaswa kuusimamia kiunaga ubaga ndani ya mda aliotutajia ila leo yu wapi?
Leo bunge la katiba limegawanyika si wabunge wa upinzani tu waliotoka hata wa ccm/cuf/tlp,201/ na kibaya zaidi mwanasheria mkuu wa znz na waziri wa katiba wa zanzibar hawamo hapo kuna katiba kweli kama sio uhuni?
Turudi kwenye hoja ya msingi,tuchukulie mbowe kaenda SA kutibiwa au kibiashara,kuna lolote lililo badilisha msimamo wa wanachama wa chadema?
Mbowe kama mwenyekiti wa chama anawatu wanaosimamia majukumu,yupo katibu mkuu,yupo makamu mwenyekitu bara pro safari na jana katoa msimamo maandamano yapo pale pale,labda kama una shida na mbowe personal