Wanasemaga hata Yesu alikuja kwa ajili ya wenye dhambi, na hakuna binadamu mkamilifu. Na hakuna dhambi kubwa kuishinda nyingine,kama ulimuona huko ni jambo jema, binafsi namuunga mkono. Ni jambo jema mwanadamu kujitafakari, ukiona unakosea mahali unajirekebisha, na kama ulikosea na unatubu/kuomba msamaha kwa imani yako. Kuomba msamaha siyo jambo la fedheha, ni jambo jema na ni ukomavu.
Kwa nafasi aliyohudumu ilikuwa kubwa na iliyogusa wengi. Kukoseana ni kawaida, hivyo kuomba msamaha na kujutia mabaya ulitotenda siyo fedheha ni ujasiri, kama ilivyo kujipingeza ufanyapo mazuri/mema, vivyohivyo kujutia mabaya na kutubu au kuomba msamaha. Kuomba msamaha isitafsiriwe kama unyonge au Ujinga. Tuone ni ujasiri, kama ambavyo mtu unaweza kujiuzuru unapoona umeshindwa kudeliver au umekosea sana na ukawapisha wanao weza.
Imani yake na imponye na kila la kheri kwake.