Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,876
- 2,740
Katika tamthiliya inayoendelea, mengi nayo yanaendelea kuibuka kutokana tu na kile kinachodaiwa kuwa ni mbinu za kampeni. Katika mchakato huu tunaambiwa kuwa daktari wa Nyerere aliamua kumpuuza na kumtelekeza na kumwachia Dr. Malima jukumu la kumtibu Mwalimu. Bila shaka kutakuwa na sababu ya msingi ya kufanya hayo hasa tukichukulia nafasi ya Mwalimu katika Taifa hili. Heshima ya kiafya anayoipata Mandela alistahili kuipata Mwalimu.
Wajuzi mtueleze kinagaubaga, ikawaje Mwakyusa hakutimiza wajibu wake na 'wito' wake kama ambavyo serikali iliyoko madarakani inataka madaktari kutimiza wito wao?
Nawasilisha.
Wajuzi mtueleze kinagaubaga, ikawaje Mwakyusa hakutimiza wajibu wake na 'wito' wake kama ambavyo serikali iliyoko madarakani inataka madaktari kutimiza wito wao?
Nawasilisha.