Nini ilikuwa dhamira ya gazeti la MWANANCHI?

kivyako

JF-Expert Member
Feb 2, 2012
14,341
12,045
Gazeti letu pendwa na huru la mwananchi limekuwa likiripoti habari ya mke wa kigogo wa polisi kuwatapeli vijana bila kutaja jina la huyo kigogo wala la mke wake (yalikuwa yakihifadhiwa) ila leo baada ya kesi kubadili uelekeo ndo majina yametajwa, 'kuwa mke wa chagonja awapeleka vijana polisi kwa kumtapeli' Mi nauliza ndg zangu nini ilikuwa dhamira ya hawa jamaa kuyahifadhi hayo majina mpaka kusubiri upepo wa kesi ubadilike?
 
Mkuu kwenye masuala kama haya wanaogopa kupelekwa mahakamani kwa udhalilishaji iwapo itakuja kujulikana kuwa issue sio kweli
Ndo maana wanapenda sana kuficha majina
Ila baada ya issue kwenda mbali na kujulikana kwenye vyombo vya juu haina haja ya kuficha tena majina
 
UNajua implication ya kutaja jina la mtu kwenye tuhuma kabla ya uthibitisho?

mkuu, umemuelewa mtoa mada?, nadhani anahoji muelekeo na muendelezo wa habari kubadilika: nadhani alitamani gazeti lingekamilisha stori kwanza- kuwa " mke wa kigogo awatapeli vijan", na wangekamilisha story kwa kutaja jina la muhusika. Kinyume chake wametaja jina la kigogo ambaye mke wake ametapeliwa. Hili ndo gogoro la mtoa mada na gazeti, na namuunga mkono GT. These could be two different stories kama siyo muendelezo wa manyanyaso yanayofanywa na watawala wa sasa.
 
Ninasoma hapa gazeti la mwananchi nimechanganyikiwa kila siku walikuwa wanariport kuwa mke wa kigogo katapeli akishirikiana na bwana anayeitwa Baraka nashangaa leo wamebadilisha na kuandika kwamba eti huyo mke wa kigogo ni miongoni wa waliotapeliwa!! najiuliza kama mwanzo walisema nafasi zinapatikana kupitia kwa kigogo wa polisi je kulikuwa na sababu ya yeye kumuamini Baraka? si angepitia kwa mumewe? je polisi wanataka kumuexonorate kwenye liability ili asishtakiwe? kwa nini mwananchi hawakukanusha habari ya kwanza? je mwananchi wanatumiwa au wanapotosha uma? is tido aware au kaingia mwananchi kupunguza umakini wa gazeti? napata kizunguzungu ngoja nikanywe chai
 
Ninasoma hapa gazeti la mwananchi nimechanganyikiwa kila siku walikuwa wanariport kuwa mke wa kigogo katapeli akishirikiana na bwana anayeitwa Baraka nashangaa leo wamebadilisha na kuandika kwamba eti huyo mke wa kigogo ni miongoni wa waliotapeliwa!! najiuliza kama mwanzo walisema nafasi zinapatikana kupitia kwa kigogo wa polisi je kulikuwa na sababu ya yeye kumuamini Baraka? si angepitia kwa mumewe? je polisi wanataka kumuexonorate kwenye liability ili asishtakiwe? kwa nini mwananchi hawakukanusha habari ya kwanza? je mwananchi wanatumiwa au wanapotosha uma? is tido aware au kaingia mwananchi kupunguza umakini wa gazeti? napata kizunguzungu ngoja nikanywe chai

wahi ndugu yangu ukapate chai, mwenzio saa hizi napoza machungu ya tumbo kwa paya la NOAH, tamu hilo, harafu husikii njaa kutwa nzima.
 
Gazeti letu pendwa na huru la mwananchi limekuwa likiripoti habari ya mke wa kigogo wa polisi kuwatapeli vijana bila kutaja jina la huyo kigogo wala la mke wake (yalikuwa yakihifadhiwa) ila leo baada ya kesi kubadili uelekeo ndo majina yametajwa, 'kuwa mke wa chagonja awapeleka vijana polisi kwa kumtapeli' Mi nauliza ndg zangu nini ilikuwa dhamira ya hawa jamaa kuyahifadhi hayo majina mpaka kusubiri upepo wa kesi ubadilike?

Mwananchi gazeti la Kenya, bongo wamekuja kusaka mkwanja. Majina yalikuwa yanafichwa kwa cash
 
1.Kimaadili waandishi hutakiwa kuhifadhi majina mpaka baada ya kuthibitishwa na vyombo husika hivyo walichofanya Mwananchi ni right.
2. Mke wa Chagonja naye ametapeliwa Sh.1.5 kwa ajili ya mwanae na nduguze wawili.
3. Kuna uwezekano Mke wa Chagonja naye aliwatonya rafiki zake nao wakawatonya rafiki zao na chain ikaendelea kama upatu, hivyo wote walio tapeliwa kwenye chain ya Mke wa Chagonja kudhania tapeli ni mke wa Chagonja kumbe sivyo bali na yeye ametapeliwa!.
4. Kwa vile mpango mzima sio tuu unahusisha utapeli bali ni rushwa ya wazi, mtoaji na mpokeaji wote ni wala rushwa, hivyo baada ya kukamilika uchunguzi wa kesi ya utapeli, wahusika wote wafunguliwe mashitaka ya kesi ya kutoa rushwa!.
5. Mke wa Chagonja athibitishe source yake ya fund, kama hana kazi yoyote ya maana au biashara yoyote ya maana, ya kumpatia Sh. 1.5 lump sum, inamaanisha source ya fund ni mumewe Chagonja, hivyo Afisa Polisi ametoa fedha ili kumpa mkewe huku akijua wazi zitatumika kwa rushwa, nalo ni kosa kisheria hivyo litamcost mumewe kazi yake under morals na sio legal.
6. Kwenye jinai, kila mtu anasimama kama yeye hivyo baada ya kujulikana ni mke wa Changonja, sasa atajwe kama Mrs. Chagonja na sio tena kumtaja kigogo wa polisi ni kumchafulia jina lake bure, Chagonja hahusiki kwa lolote hata kama ni yeye alimpa mkewe fedha hizo za rushwa!.
7. Sheria zetu za jinai zinatoa kinga kwa mume au mke hawezi kutumiwa na mahakama kutoa ushahidi au utetezi unamhusu mwenza wake, hivyo Chagonja haguswi kwa namna yoyote na nyendo zozote za kijinai za mkewe wala hatakiwi kuchunguzwa kijinai bali ni jukumu la jeshi la polisi kumchunguza ki morals kama kiongozi!.
8. Chagonja anaweza kulishitaki Gazeti la Mwananchi kwa kesi inayoitwa "defamation by innuendo" kwamba kosa ni la mkewe, kitendo cha gazeti hilo kushadidia "Mke wa Kigogo wa Polisi" na kigogo huyo ni yeye by implication anayechafuliwa jina ni yeye na sii mkewe!.
9. Enzi za Nyerere, Chagonja angekwenda na maji kwa kuitumia ile formular ya "Mke wa Kaisari".
Pasco.
 
Tatizo kubwa ni kwamba, wahalifu ni polisi, wapelelezi wa kesi ni polisi, na waendesha mashtaka ni polisi, lazima tu haki haitakuwepo
 
1.Kimaadili waandishi hutakiwa kuhifadhi majina mpaka baada ya kuthibitishwa na vyombo husika hivyo walichofanya Mwananchi ni right.
2. Mke wa Chagonja naye ametapeliwa Sh.1.5 kwa ajili ya mwanae na nduguze wawili.
3. Kuna uwezekano Mke wa Chagonja naye aliwatonya rafiki zake nao wakawatonya rafiki zao na chain ikaendelea kama upatu, hivyo wote walio tapeliwa kwenye chain ya Mke wa Chagonja kudhania tapeli ni mke wa Chagonja kumbe sivyo bali na yeye ametapeliwa!.
4. Kwa vile mpango mzima sio tuu unahusisha utapeli bali ni rushwa ya wazi, mtoaji na mpokeaji wote ni wala rushwa, hivyo baada ya kukamilika uchunguzi wa kesi ya utapeli, wahusika wote wafunguliwe mashitaka ya kesi ya kutoa rushwa!.
5. Mke wa Chagonja athibitishe source yake ya fund, kama hana kazi yoyote ya maana au biashara yoyote ya maana, ya kumpatia Sh. 1.5 lump sum, inamaanisha source ya fund ni mumewe Chagonja, hivyo Afisa Polisi ametoa fedha ili kumpa mkewe huku akijua wazi zitatumika kwa rushwa, nalo ni kosa kisheria hivyo litamcost mumewe kazi yake under morals na sio legal.
6. Kwenye jinai, kila mtu anasimama kama yeye hivyo baada ya kujulikana ni mke wa Changonja, sasa atajwe kama Mrs. Chagonja na sio tena kumtaja kigogo wa polisi ni kumchafulia jina lake bure, Chagonja hahusiki kwa lolote hata kama ni yeye alimpa mkewe fedha hizo za rushwa!.
7. Sheria zetu za jinai zinatoa kinga kwa mume au mke hawezi kutumiwa na mahakama kutoa ushahidi au utetezi unamhusu mwenza wake, hivyo Chagonja haguswi kwa namna yoyote na nyendo zozote za kijinai za mkewe wala hatakiwi kuchunguzwa kijinai bali ni jukumu la jeshi la polisi kumchunguza ki morals kama kiongozi!.
8. Chagonja anaweza kulishitaki Gazeti la Mwananchi kwa kesi inayoitwa "defamation by innuendo" kwamba kosa ni la mkewe, kitendo cha gazeti hilo kushadidia "Mke wa Kigogo wa Polisi" na kigogo huyo ni yeye by implication anayechafuliwa jina ni yeye na sii mkewe!.
9. Enzi za Nyerere, Chagonja angekwenda na maji kwa kuitumia ile formular ya "Mke wa Kaisari".
Pasco.

Pasco, umajitahidi kutoa ufafanuzi wa kumpunguzia uzito wa kosa mke wa Chagoja; hapo sikuungi mkono, mimi habari za uhakika nilizonazo ni kuwa mke wa afande chagonja ndiye aliyeanzisha dili la kuwadanganya watu kuwa anaweza kuwapa mchongo wa PCCB na UWT, wewe unateteta tu. Lakini jiulize; hivi nke wa afisa mwandamizi wa serikali hawezi kudhiridhisha juu ya uwepo wa nafasi katika taasis nyeti ya serikali?!, mpaka atapeliwe na wapita njia?, kwa uelewa wangu hilo haliwezekani.
 
Ninasoma hapa gazeti la mwananchi nimechanganyikiwa kila siku walikuwa wanariport kuwa mke wa kigogo katapeli akishirikiana na bwana anayeitwa Baraka nashangaa leo wamebadilisha na kuandika kwamba eti huyo mke wa kigogo ni miongoni wa waliotapeliwa!! najiuliza kama mwanzo walisema nafasi zinapatikana kupitia kwa kigogo wa polisi je kulikuwa na sababu ya yeye kumuamini Baraka? si angepitia kwa mumewe? je polisi wanataka kumuexonorate kwenye liability ili asishtakiwe? kwa nini mwananchi hawakukanusha habari ya kwanza? je mwananchi wanatumiwa au wanapotosha uma? is tido aware au kaingia mwananchi kupunguza umakini wa gazeti? napata kizunguzungu ngoja nikanywe chai
Nimeacha siku nyingi kusoma magazeti ya Tanzania kwa sababu wao wanaandika HABARI ili wauze GAZETI na sio WANAANDIKA HABARI ILI KUHABARISHA UMMA! Ndio maana mara nyingi hawaandiki ukweli au uhalisia wa jambo. Na mara nyingine wanaweza kuandika vitu visivyohusiana kabisa... Mkuu, hivi ulidhani kuwa Tido akiwa kule ndio kutabadilika?

Nilipata kusema YEYOTE MWENYE ASILI YA MAGAMBA HUWA HABADILIKI HATA AKIJIGAMBUA MAGAMBA KWA SABABU HIYO NI ASILI. NA ASILI NI KAMA MAJI, UTAYACHEMSHA NA BAADA YA MUDA YATARUDI KATIKA UHALISIA WAKE.

UKITAZAMA VEMA HATA HAO TUNAOWASIFIA LEO KUWA WANATUFAA ASILI YAO NI MAGAMBA! TUNAHITAJI KIZAZI KIPYA AMBACHO HAKIKUPATA KUWA KWENYE JAMII YA MAGAMBA KATIKA NYANJA ZOTE ILI TUENDELEE....
 
Madhara ya kuwapa nafasi wake wa viongozi kufungua vituo vya polisi, kupokea mafungu ya fedha ili eti kuwafundisha watanzania kunawa mikono (kwa hisani ya watu wa marekani)

Watoto wa viongozi tumewapa heshima za baba zao. Oneni rizimoko anavyotutenda.
Hii ni nchi ya michongo, imepaswa tuchukue hatua.
 
Ndugu zangu inaonyesha huyo mama ni tapeli kwa sababu
1.yeye ni mke wa mmoja wa maafisa waandamizi wa jeshi la polisi kwa nini asingejiridhisha kwanza na huo utaratibu hata kwa kumuuliza mumewe taratibu zikoje kabla ya kutoa hongo ili hao watu wake wapate kazi
2.kwa cheo alichonacho changonja mumewe ilikuwa ni rahisi kuwatafutia kazi hao watu wake(kama kweli wana sifa) kupitia mumewe kuliko kutoa hongo sehemu nyingine

3.hata ukiangalia huu utapeli umefanikiwa kwa sababu watu wengi walimwamini kuwa wangepata kazi kwa sababu yeye ni mke wa chagonja ndo mana ikawa rahisi kwa watu kumwamini
 
Back
Top Bottom