Mremaaa
JF-Expert Member
- Jul 1, 2015
- 293
- 325
Wasalam wana Jamvi!
Ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya tukimalizia weekend yetu murua kabisa!!
Niweke mada mezani bila kupoteza muda!
Siku ya leo nimefanya kitendo ambacho sikuwahi kufikiria kukifanya katika maisha yangu. Tumepishana kauli na mke, sasa huwa nikiwa na hasira nina desturi ya kukaa kimya na kuondoka, na Mara zote huwa naepusha ugomvi kwa namna hiyo, ndugu zetu akina mama wamejaliwa kuongea sana tofauti na sisi wanaume, hasa mimi yaani sipendi kelele kabisa kama kuna issue tusemeshane taratibu tuongee tumalize sio kelele
Ilikuwa majira ya saa mbili na nusu asubuhi ya leo, wakati tumetoka tu kanisani ibada ya Alfajiri.
Issue ni ndogo sana, mimi naandaa nguo zangu kwa ajili ya safari yangu siku ya kesho, sasa kuna baadhi ya mashati yangu aliyatunzaga kabatini nikawa namwagiza anipatie, kidogo majibu yake hayakuwa mazuri ukizingatia ni mke wangu sio hawara, na mimi alivyonijibu ilikuwa kwa dharau flani au anamjibu mdogo wake au mtoto kiukweli sikupendezwa, nikamuuliza unamfanyia nani hayo? Ikaanza kelele wewe, nikamwambia sikuelewi !! Ahaa bhana niache huwezi kuchukuaa mwenyewe, nikawa mpole nikamwambia sipendi kelele inatosha, ikaanza mada nyingine ambayo haihusiani, kuhusu maswala ya fedha na aseti ikawa kelele zaidi nikamwambia haya nimekuelewa inatosha, ehee mwenzangu hanisikii wala haelewi, nikamwambia basi toka chumbani mimi sitaki sharii, ahaa sitokiii!! Kelele ikawa kubwa sana!! Nikashindwa kujizuia kiukweli nikampiga! Tangu hiyo asubuhi hatujasemeshana kabisa, wala kumwona sijamwona, maana nyumba ina vyumba vingi vingine siwezi ingiwa sababu ni vya wasaidizi wetu wa kike !! Ila naisikia sauti humu humu ndani!!
Baada ya hayo kutokea nikaenda kwenye mizunguko yangu nikarudi saa Tisa, aliyenitengea chakula ni shemj yangu yaani mdogo wake wa kiume ambaye pia tunaishi naye hapa!!
Jionii hii pia chakula nimekula na huyo shemj yangu yeye sijamwona!!
Sijui pia hali yake ikoje mpaka sasa!
Naombeni ushauri juu ya-:
1) Nimwombe msamaha kwa kitendo hicho?
2) Au nikae tu kimya ?
3) Kesho nisafiri kama nilivyopanga ?
4)Na ushauri mwingine wowote nipo tayari kuupokea!!
Nawasilisha karibuni kwa ushauri na michango mbalimbali!!
Ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya tukimalizia weekend yetu murua kabisa!!
Niweke mada mezani bila kupoteza muda!
Siku ya leo nimefanya kitendo ambacho sikuwahi kufikiria kukifanya katika maisha yangu. Tumepishana kauli na mke, sasa huwa nikiwa na hasira nina desturi ya kukaa kimya na kuondoka, na Mara zote huwa naepusha ugomvi kwa namna hiyo, ndugu zetu akina mama wamejaliwa kuongea sana tofauti na sisi wanaume, hasa mimi yaani sipendi kelele kabisa kama kuna issue tusemeshane taratibu tuongee tumalize sio kelele
Ilikuwa majira ya saa mbili na nusu asubuhi ya leo, wakati tumetoka tu kanisani ibada ya Alfajiri.
Issue ni ndogo sana, mimi naandaa nguo zangu kwa ajili ya safari yangu siku ya kesho, sasa kuna baadhi ya mashati yangu aliyatunzaga kabatini nikawa namwagiza anipatie, kidogo majibu yake hayakuwa mazuri ukizingatia ni mke wangu sio hawara, na mimi alivyonijibu ilikuwa kwa dharau flani au anamjibu mdogo wake au mtoto kiukweli sikupendezwa, nikamuuliza unamfanyia nani hayo? Ikaanza kelele wewe, nikamwambia sikuelewi !! Ahaa bhana niache huwezi kuchukuaa mwenyewe, nikawa mpole nikamwambia sipendi kelele inatosha, ikaanza mada nyingine ambayo haihusiani, kuhusu maswala ya fedha na aseti ikawa kelele zaidi nikamwambia haya nimekuelewa inatosha, ehee mwenzangu hanisikii wala haelewi, nikamwambia basi toka chumbani mimi sitaki sharii, ahaa sitokiii!! Kelele ikawa kubwa sana!! Nikashindwa kujizuia kiukweli nikampiga! Tangu hiyo asubuhi hatujasemeshana kabisa, wala kumwona sijamwona, maana nyumba ina vyumba vingi vingine siwezi ingiwa sababu ni vya wasaidizi wetu wa kike !! Ila naisikia sauti humu humu ndani!!
Baada ya hayo kutokea nikaenda kwenye mizunguko yangu nikarudi saa Tisa, aliyenitengea chakula ni shemj yangu yaani mdogo wake wa kiume ambaye pia tunaishi naye hapa!!
Jionii hii pia chakula nimekula na huyo shemj yangu yeye sijamwona!!
Sijui pia hali yake ikoje mpaka sasa!
Naombeni ushauri juu ya-:
1) Nimwombe msamaha kwa kitendo hicho?
2) Au nikae tu kimya ?
3) Kesho nisafiri kama nilivyopanga ?
4)Na ushauri mwingine wowote nipo tayari kuupokea!!
Nawasilisha karibuni kwa ushauri na michango mbalimbali!!