Clearly Nchi imemshinda, anaonekana kuhaha, hana maamuzi, hajui cha kufanya, kiujumla nchi imemshinda kabisa, ni aibu kubwa kwa rais wa nchi kama Tanzania kukosa maamuzi, inatia kichefuchefu.
KIPIMO CHANGU CHA NCHI KUMSHINDA:
1. Huyu bwana hajui hata yanayoendelea ndani ya serikali yake:
Kipindi flani mwaka huu, akihutibia wananchi katika viwanja vya jangwani, akiwemo mama Tibaijuka, alipiga kelele kuhusu ujenzi wa uzio wa mabati katika ujanja huo, akamuagiza mama tibaijuka kuwaondoa hao "jamaa, wanaojenga hapo mara moja" maana uwanja wa jangwani ni sehemu ya wazi inayotakiwa kuhifadhiwa. Chaa jabu kabisa, huo ulikua ni ujenzi wa kituo cha mradi wa mabasi yaen dayo kwa kasi.
Aibu kubwa zaidi, hivi majuzi mwaka huu yeye mwenyewe akaenda kufungua mdari huo wa mabasi yaendayo kwa kasi..aibu gani hii..
Inamaana waziri wa ujenzi, na waziri wa ardhi hawakumpa mzee taarifa kuhusu ujenzi huo hapo jangwani??
Kikwete hakuona umuhimu wa kuuliza kabla ya kuota maamuzi??? Inamaana Rais anaweza kwenda mahali asiwe na taarifa muhimu kuhusu eneo analokwenda??
Huu udhaifu na aibu kubwa kama hii, imetokana na nani??? UONGOZI wake ama watendaji wake????
Kwa hili ni kupimo tosha kuwa kikwete , hii nchi imemshinda, hajui afanyalo, jiuzulu tu baba, upishe tufanye uchaguzi.