Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,702
- 36,132
Wiki ijayo tunapokea ndege nyingine ya fedha nyingi sana ambayo itaungana na ndege zingine za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).
Ununuzi wa ndege za mabilioni si tatizo, tatizo ni pale tumeruka hatua muhimu. Tulipaswa kutatua masuala ya maji, umeme, elimu, na afya kwanza kabla ya kufikiria kununua ndege.
Inafika wakati ambapo viongozi na waalikwa katika sherehe za kupokea ndege wanafananishwa na watu wasio na akili. Shule nyingi zina madarasa yanayoonekana kama maghala au mabanda ya kuhifadhi mkaa.
Vyoo na madarasa ambayo serikali inajivunia mtandaoni ni msaada wa COVID-19. Ni vipi tunafanya mambo muhimu kwa msaada halafu pesa zetu zinanunua ndege za mabilioni?
Choo cha shule kinajengwa kwa msaada. Je, unajenga choo kwa msaada na bado unataka sifa mara tatu? Leo hii, matibabu ya wazee na watoto ni bure lakini wanapata tu vipimo na wanapewa Panadol na Aluu, halafu wanatakiwa kununua dawa nyingine dukani.
Hali hii itaendelea hadi lini?
Kwa sasa, tuache masuala ya ndege kwa mashirika binafsi. Tutatue kwanza suala la vyoo shuleni na katika zahanati. Kuna choo kimoja karibu na mahakama, kinafunguliwa na msimamizi, ukiona unahitaji kwenda, lazima ulipe.
Bei ya Boeing 737-9 Max sokoni ni kubwa sana. Fedha hizo zingeweza kutumika kujenga madarasa ya kisasa bila kikomo. Watoto wakiwa darasani, wanaweza kufikiria wako chooni. Madarasa ni mabovu, na ofisi za walimu katika shule za umma zina mashimo ya kutosha.
Ununuzi wa ndege za mabilioni si tatizo, tatizo ni pale tumeruka hatua muhimu. Tulipaswa kutatua masuala ya maji, umeme, elimu, na afya kwanza kabla ya kufikiria kununua ndege.
Inafika wakati ambapo viongozi na waalikwa katika sherehe za kupokea ndege wanafananishwa na watu wasio na akili. Shule nyingi zina madarasa yanayoonekana kama maghala au mabanda ya kuhifadhi mkaa.
Vyoo na madarasa ambayo serikali inajivunia mtandaoni ni msaada wa COVID-19. Ni vipi tunafanya mambo muhimu kwa msaada halafu pesa zetu zinanunua ndege za mabilioni?
Choo cha shule kinajengwa kwa msaada. Je, unajenga choo kwa msaada na bado unataka sifa mara tatu? Leo hii, matibabu ya wazee na watoto ni bure lakini wanapata tu vipimo na wanapewa Panadol na Aluu, halafu wanatakiwa kununua dawa nyingine dukani.
Hali hii itaendelea hadi lini?
Kwa sasa, tuache masuala ya ndege kwa mashirika binafsi. Tutatue kwanza suala la vyoo shuleni na katika zahanati. Kuna choo kimoja karibu na mahakama, kinafunguliwa na msimamizi, ukiona unahitaji kwenda, lazima ulipe.
Bei ya Boeing 737-9 Max sokoni ni kubwa sana. Fedha hizo zingeweza kutumika kujenga madarasa ya kisasa bila kikomo. Watoto wakiwa darasani, wanaweza kufikiria wako chooni. Madarasa ni mabovu, na ofisi za walimu katika shule za umma zina mashimo ya kutosha.