Ninatafuta mpenzi/mume nipo serious

Ninatafuta mpenzi/mume nipo serious

Mmh kwa jinsi visichana vinavyosumbua.. Naona nijiweke kwako tufurahie maisha japo nina mtoto mmoja
 
Dah.... Masharti mengi sana....
Ya kawaida tu kama unajua maana ya maisha. Uzoefu umenifanya kuweka hivyo. Ndiyo maana huoni vitu kama sura, umbo, kabila, elimu n.k kwenye andiko langu.
 
Toka alhamisi hadi leo jumamosi nadhani mstahiki keshajitokeza kuwania nafasi

Kuomba unachokihiitaji ni jambo moja na kupata unachokitaka ni jambo la pili...Mungu akusimamie
Asante. Kitu kizuri hakina haraka. PM wamekuja wengi shida vigezo. Akipatikana nitarudi hapa kufunga thread.
 
Mmh kwa jinsi visichana vinavyosumbua.. Naona nijiweke kwako tufurahie maisha japo nina mtoto mmoja
Mtoto mmoja si tatizo hata ungekuwa nao kumi. Cha msingi ni vigezo nilivyoweka tu kuanzia umri na kuwa huna mke ni muhimu zaidi.
 
Duh!! Kweli utu uzima dawa na wisdom!! Visichana kama atoto wala havifahamu kwamba mwanaume aliyefiwa na mke ni deal!!
 
Watu wengine huwa wanakosa wapenz wazuri sio kwa bahati mbaya ila ni kwasababu ya misimamo miingi kama hii yako ambayo kwa kiasi kikubwa umetawaliwa na umimi (ubinafsi). Hivi ni mtu gani anayejitambua utamwambia nataka ufate hiki, kile mara usiniingilie kwenye hiki na kile halafu naye akubali tu na kunywea kama vile sio binadamu mwenye hisia na mapendeleo?
Nakushauri tu, mahusiano yoyote (hata yasiyo ya kimapenzi) it's about compromise of what you believe kwa kiasi flani. Usipolikubali hilo utaendelea kuwa mpweke milele au kupata kampani za watu wenye malengo ya muda mfupi kama hao uliotangulia kuwa nao.
 
Mimi ni mwanamke mwenye miaka 47. Nina watoto watatu. Tulitengana katika ndoa baada ya kutendwa na kutelekezwa na mume. Nilikwazika na kukata tamaa sana ya mahusiano. Nilikaa muda mrefu sana bila mahusiano. Nikajaribu kuruhusu ya aliyejiita mlokole kumbe ilikuwa gear ya kuficha maovu.

Nikaangukia pua kwa mara ya pili na kuamua kuishi tena muda mrefu bila mahusiano. Kwa sasa basi ninahitaji kumpata mwanamume ambaye ana mapenzi ya dhati hasa uaminifu. Sihitaji kuolewa au niseme kuishi na mwanamume tena ila ninataka company tu. Na kupitia kampany nitaweza kujifunza kwa undani kama kweli mwanaume yuko siriazi au la. Ninachohitaji kwa sasa ni upendo wa dhati, nimerudia hapo.

Sitaki wababaishaji wa mahusiano na hapa atakayejitokeza awe mtu wa uhakika ambaye:

- Ni mgani i.e aliyefiwa na mkewe kwa misingi hii kama una baba yako hapa alifiwa na mama niunganishe tu. Au kaka yako ambaye amefiwa na mke niunganishe tu.

- Akubali kupima HIV

- Asiwe mume wa mtu au mwanaume ambaye hajao ila ana wanawake ambao ana connect nao. Hii imenigusa sana baada ya kukutana na mwanaume ambaye alizaa na several women kumbe ni mtu ambaye hana future kabisa kimaisha ya familia. Nilimpenda sana ila changamoto za wanaume kama hawa ni kubwa sana. Ni kujitakia presha.

- Anipe uhuru wa kufanya mambo yangu ya kiuchumi kwa kuwa nina watoto na ninahitaji wasiishi maisha ya tabu . Sitaki kuwa tegemezi hapa. Nimejifunza sana.

- Awe ananithamini mimi kama mpenzi wake na asinilazimishe ndoa mpaka pale nitapona kuwa kweli ni mtu wa kuzeeka naye.

- Awe ni mtu anayejituma katika kuzalisha mali, either ameajiriwa/kujiajiri au anafanya biashara zake.

- Awe ni mtu anayependa familia kwa kuanzia na watoto wake mwenyewe iwe ni priority kwake kabla hajawapenda wanangu mimi.

- Awe tayari kuandikiana pre-nuptial agreement kama itafikia mahali tuamue kuishi pamoja. Ninasema hivi kwa kuwa atakuwa na mali zake na wanawe ambao atataka kuwapa urithi na mimi nina wanangu na chochote kidogo nilichoweza kuhangaikia kwa miaka yangu hivyo sitaki ugomvi wa mali hata kidogo.

-Asiwe Mlevi au Mvuta sigara.

- Awe mkristu. Sibagui ila mimi ni mkristu na wangu pia hivyo itakuwa shida kidogo hapa. Nimekuwa mkweli msinielewe vibaya.

- Awe na miaka kati aya 47-50.

Ninasema sasa kwa mwanaume ambaye anaona anaweza kujaribu kuanzisha mahusiano na mimi karibu PM. Ukiona utatoa lugha mbovu isiyo na staha ninaomba upite taratibu.

Angalizo.
Nipo serious, ninaomba sitaki lugha za matusi ua mitaani mimi ni mtu mzima. Wanaume serious tu na wenye umri niliotaja wani Meseji (PM].
Huwezi kuandika mbele za watu wasome unachotaka alafu uwazuie mawazo yao na lugha watakazotumia kukujibu dhidi yako,kiufupi MUNGU pekee ndo mwenye majibu yako na huleta mtu pasi hata wewe kujua siku wala saa,lakini kuja hapa kutafuta mume ni kuendelea kumpa shetani nafasi akuletee tena wale wale,wewe unapaswa kufundishwa hekima kwanza.
 
Asante. Kigezo kigumu ni kipi hapo? Nisaidie ili kama vipi nikiondoe.
Loeli a.k.a Bundimkubwa salamu.

Mojawapo ya kigezo ambacho naamini kinakwaza wengi ni hiki cha mlengwa shurti awe amefiwa na mwenza.....

Unaweza niambia ni kitu gani hasa kimekufanya umfikirie mfiwa zaidi na si mwinginewe??
 
Huwezi kuandika mbele za watu wasome unachotaka alafu uwazuie mawazo yao na lugha watakazotumia kukujibu dhidi yako,kiufupi MUNGU pekee ndo mwenye majibu yako na huleta mtu pasi hata wewe kujua siku wala saa,lakini kuja hapa kutafuta mume ni kuendelea kumpa shetani nafasi akuletee tena wale wale,wewe unapaswa kufundishwa hekima kwanza.
Asante sana kwa ushauri. Kila MTU mwenye mke au mume wanayeishi vizuri wana historia ya jinsi walivyokutana. Vigezo vyangu Mimi ni rare ndiyo maana ni lazima nijiongeze njia ya kupata.
 
Kumpata mwanaume wa vigezo ulivoweka ni ngumu sana. Mwanaume wa aina hiyo anaonekana haraka sana na kuwahiwa na wanawake wenzako hata kama alifiwa na mkewe. Ukizingatia umri umeekukata kidogo huwezi pata unachokitafuta mama, cha msingi achana na mapenzi kuwa bize na watoto tafuta mtu mzima mwenye mke uwe mchepuko wake kwa siri mambo yataenda sio kutafuta mtu wa kummliki wewe.
NB. Kadri binadamu anavoongezeka umri kwa mwanamke thamani yake inaporomoka(deceleration) sana ila kwa mwanaume thamani inapanda(acceleration)
 
Mimi ni kijana umri miaka 25 sina kazi yoyote mision town! Yaani kula kulala siwazi saaana maisha ya hapo baaadae nawaza leo tu nitakula nini na nitalala wapi..... (same text missing)
 
Back
Top Bottom