Self Improvement and Personal Real Life Achievement
Hali si shwari ndani ya Ccm kwa ujumla. Hali tete imejitokeza ghafla na Sasa ni vikao kila kona, tunasubiri
*********************************************
************************************
Kikao cha dhalura chaitishwa Kamati kuu: sumaye atikisa chama na Sasa mpango mkakati waundwa, tutawajuza kinachojiri huko Lumumba.
Ipo hatari ya mtu kung'ang'ania Ikulu:
Fundi Mkuu Anasema
Patamu sana, Sumaye wa Mkapa, Lowassa wa Kikwete, hakuna siri tena hapo, Mwandosya atatueleza kuhusu IPTL, kuna hatari mtu kung'ang'ania ikulu hapa, Maanake akiachia tu madaraka kisutu inamhitaji.
Yericko Nyerere anasema Wakijichanganya tu, ataweka siri zote za wizi wa Simba trust uliofanywa na familia ya Mzee huu mwaka mtamu, Torongey Mathayo hii ndiyo nafasi kuwaumiza.Ngoja tuone hapo.
Kwakweli kunahaja kubwa ya kumtunuku Mbowe cheo cha heshima cha kitaifa kutambua mchango wake, Leo ameweza kuwaunganisha makundi yote hasimu na mengineyo, Leo sumaye na Lowasa waliokuwa maadui wanacheka pamoja?
Aaah Mbowe nakupa cheo cha Rafidainian Order First Class, ROFC, Hiki ni cheo cha juu kwa jasusi mwenye taaluma zote ndani ya idara ya ujasusi duniani, yaani mpanga mikakati, na mtekeleza mikakati ikiwemo uwezo mkubwa wa wa diplomasia ya kijasusi. Nawiwa na furaha na kuona taifa jipya la Tanzania likizaliwa mikononi mwa Mbowe.
Nakupa saluti kubwa sana ya Ukombozi Kamanda Mbowe, Navutiwa kuona Mbowe unakuwa Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa nchini Tanzania baada tu ya kulikomboa taifa hili, naamini utafanya mapinduzi makubwa sana ya Idara hii nchini;