Ninahitaji Mwanamke Tasa (Mwanamke asie na uwezo na kushika mimba na kuzaa)

Ninahitaji Mwanamke Tasa (Mwanamke asie na uwezo na kushika mimba na kuzaa)

Arch Barrel

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2024
Posts
533
Reaction score
1,225
Naenda moja kwa moja kwenye maada.

Nina miaka 33, kabila langu (siri), kazi yangu (siri) na mkoa ninaoishi kwa sasa (siri) ingawa ni kanda ya ziwa.
Nina watoto wanne, wakiume wawili na wakike wawili pia. Watoto watatu nimepata kwa mama mmoja na mmoja nimepata kwa mama mwngine.
Mzazi mwenzangu mwenye watoto watatu tumetengana rasimi zaidi ya mwaka sasa na aliamua kuniachia watoto na kwenda kuanzisha maisha yake zaidi ya mwaka sasa, awali nilitegemea kuwa huyu mama mwenye mtoto mmoja angeweza kuwatunza na kuwajali hawa watt watatu lakini imekuwa tofauti. Lakini pia amekuwa akilazimisha na yeye awe na watoto watatu kama mwenzie jambo ambalo kwangu limekuwa gumu. kiufupi siwezi kuongeza watoto zaidi ya hawa wanne niliojaliwa wanatosha. Huyu mzazi mwenye mtoto mmoja nae ameamua kuondoka nae tumetengana rasimi kwa sababu matakwa yetu yametofautiana na yeye pia ameacha mtoto kwangu.
Hivyo kwa sasa nina watoto wanne ndani ya nyumba yangu. Miaka 8 mmoja, miaka 6 mmoja na miaka 2.5 wawili.

Baada kutafakari sana, nimefikiria vitu mhimu viwili
Kwanza kuwalea na kuwatunza hawa watoto kama ilivyo dhamira yangu toka awali bila kupitia changamoto yoyote
Pili, mimi mwenyewe kupata rafiki, mfariji na mshauri ambae muda mwingi atakuwa pembeni yangu. Hapa tendo la ndoa ni mhimu sana kwangu maana kuna wakati linapunguza makasiriko.

Sharti moja pekee nililonalo kwa mwanamke huyu nje sharti la kwanza la kuwa tasa, nahitaji awe mama mlezi, awapende na kuwajali watoto wangu (ingawa najua hii ni ngumu sana ila naomba Mungu anisaidie iwezekane), umri wake uwe chini miaka 30 ila asipungue 24.

Jukumu na malengo yangu niliyojiwekea sasa yametimia, lengo la kwanza ilikuwa kupata watoto, lengo la pili sasa naanza kutafuta hela.

Naweka angalizo kwa mwanamke alie tayari, sihitaji mtoto tena.

Kama una ndugu, dada, rafiki au jirani naomba karibu sana kwenye DM yangu.

Lakin pia nakaribisha ushauri kutoka kwenu wanajukwaa.
Mwisho
 
Pole sana, ila unaweza kuwa na mwanamke mwingne yoyote ambye anaweza kukubaliana na matakwa yako... Sio lazima awe tasa
 
Lakini pia amekuwa akilazimisha na yeye awe na watoto watatu kama mwenzie jambo ambalo kwangu limekuwa gumu.
- Timiza mahitaji yake; Ikiwezekana sio watatu tu; Fanya kumi kabisa (Joking); Kama mdau hapa chini
1750308685900.jpeg
 
Sharti moja pekee nililonalo kwa mwanamke huyu nje sharti la kwanza la kuwa tasa, nahitaji awe mama mlezi, awapende na kuwajali watoto wangu (ingawa najua hii ni ngumu sana ila naomba Mungu anisaidie iwezekane), umri wake uwe chini miaka 30 ila asipungue 24.
Mungu atakusaidia, utapata mwenza anayekidhi vigezo. ( Sorry kwa post iliyotangulia ina kautani kidogo)
 
Toa ofa ya kulea watoto wako umeandaa kiasi gani?

Unataka mwanamke wa kwenda kumtomb@ tu sio wa kukuzalia nakushauri tafuta wasichana wa kazi walee watoto wako na wewe mwenyewe tafuta mwanamke hata awe mdangaji wa kulipa kei bila kubeba mimba yako.(Au usimmwagie ndani)
 
Utamlipa bei gani?

Unaonekana mbinafsi sana, na umeachana nao wote wawili kwa sababu ya ubinafsi. Wakati wenzio wanataka win-win situation wewe unataka win-loose. Hata ukimpata mwingine mtashindwana mapema tu kama hutofanya reforms kwa upande wako.

Hakuna wa kukuvumilia alee wanao wanne yeye asizae hata mmoja. Ajiri housemaid.

Anyway, ningekusonteshea x wangu ila kwa mfumo wako huo utamtesa tu anilaumu nami nijutie. Kwanza ndo kwanza yupo 24 yrs na hajakata tamaa hivyo akija kwako atahitaji mtafute tiba azae. Umri huo ulioutaja (24-30) wengi bado wanapambana hawajakata tamaa, na wengi wao huwa wanafanikiwa kuzaa. Wewe nawe unalenga kuua mapambano yao! Hamtoelewana. Tafuta jimama lililofikia menopause.


NRNE.
 
Wanawake wa sasa hawapendi shida,akisikia una watoto wanne na yeye hazai anajua unaenda kumfanya beki 3 hawawez kukubali
 
Wanawake wengi waliozaliwa Mwezi wa 10 uwa wanashida ya kuuzaa, ni vyema ukajikita na hao.
 
Back
Top Bottom