NINA MASHAKA NA UAMUZI HUU ULIOFANYWA NA Mh Mbowe:

peoples powerrrrrrrr!!!!!!!!
Mamndenyi kitu ambacho hawa magamba hawakijui ni kwamba Chadema tunaamini kwamba maisha na uhai wa watanzania ni muhimu sana kuliko kitu chochote sembuse hii bajeti yao mbovu ya sigara, pombe na soda?


Wabunge wa Chadema ni wawakilishi wa wananchi na kwakuwa wananchi wa Arusha wamekumbwa na msiba mkubwa basi ni muhimu wawakilishi wao wajumuike nao katika kipindi hiki cha majonzi na maombolezo. Kuna watu wengi bado wako hospitali wanahitaji msaada wa hali namali hivyo kuhitaji watu kuwa nao karibu kufuatilia hali zao.

Kama ccm ina wabunge zaidi ya 200 ukiongezea na ndugu zao wa cuf ambao wako zaidi ya 30, kwa idadi hiyo ya wabunge takribani 300 ni wengi sana na wanaweza kuijadili bajeti mbovu ya magamba.

Hiki kilio cha magamba kuwataka wabunge wa Chadema kuwepo Dododma kujadili bajeti yao kinadhihirisha kuwa wabunge wa Chadema ndio wenye uwezo na akili ya kuijadili na kuiboresha bajeti hiyo na hao wa ccm na mshirika wao cuf ni maamuma na hawawezi ku-add value katika bajeti hiyo.
 
mkuu hebu fikiri picha gani itajengeka kwa wananchi hasa wanachama wa chadema kama wabunge wangeendelea kuwepo bungeni nakuchangia kama kawaida wakati kuna tukio kubwa kama hili la watu kufa kwaajili ya chama,bila shaka wabunge na chadema kwa ujumla wangeonekana ni wasaliti wakubwa na wasiopenda kushirikiana na wananchi wao,mimi nasuport uamuzi wa mbowe
 
Sikutegemea kwa mtanzania mwenye akili timamu kama wewe uandike ----- kama huu...hiyo bajeti ni ya nani? na waliokufa ni kina nani? ifike mahala tuache fikra za ajabu ajabu

Bora mkuu umeshamwambia maana nilisha m-devaluate baada ya kuun huu uzi. Mud mwingine tuweke siasa pembeni na kuangalia ukubwa wajambo lililotokea pale Arusha.
Naona watu kama mtoa mada wanaanza kuzoea mapema matukio yanayohusu urushwaji w mabomu kwenye halaiki ya watu, kitu ambacho watanzania hawajakizoea. Je huu ni mkakati maalumu wa kuanza kuonesha kinachoenda kutokea katika uchaguzi mkuu au baada ya matokeo kutangazwa 2015?
 
Revocatus una mawazo mazuri katika ulimwengu wa watu wa aina yako! Hivi wewe ungekuwa ni mkeo(kama una bahati ya kuwa nae) kapatwa na ugonjwa au anahitaji kwenda kutibiwa utamuacha na kwenda kazini? Au wewe ni mmoja wa wale wanao delegate nyumba zao? Angalia usije ukawa umetumwa na Mashaitwan wa kijani kuanzisha hii thread!
 
Nina wasiwasi na akili yako inajaa matope kwakuwa CHADEMA sio chama cha kutoana kafara ni cha kuwatumikia wananchi je nikuulize wewe ambae ni mpuuzi na pungufu wa mawazo utakuwa na raha gani kutumika au kufanya kazi angali mmoja wa familia yako amefariki???? CHADEMA ni chama cha kutetea wanyonge na ninahisi wewe sio miongoni mwao maana hata akili yako imeshindwa kucharge... TAFAKARI NA UWE NA MANENO NA SENTENSI ZENJE MAANA...
 
Wewe ni nape with fake ID. Tokea ulipoanza kuangalia bibi kiroboto na ze comedy yake lini uliona kambi ya upizani inatoa maoni na yanafuatwa?

Lakini sikushangai kwamba hata chembe ya fikra huna, watu wamepotea kwenye mkutano wa chadema sasa ulitaka chadema waonesheje kuguswa na tukio walilofanyiwa na nyinyi kwa hao mliowatesa?

Kama nakumbuka vizuri mtwara hakufa mtu lkn bunge zima liliahirishwa mbona hukujitokeza kutoa uhalo wako hapa.

Achana na unafiki kajenge nchi yako. Ila cku umeingiza. Big up
 
kuna sehemu nimenukuu,
'Hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kuungana na mtu kama MBOWE au MAPROSOO aka MZINZI au PADRE FEKI ( SLAA )?

kwanza ni mwizi ,tapeli ,mzinzi na mtu asiyejuwa uongozi kwa sababu amejaaliwa kipimo kidogo sana HEKIMA na BUSARA.

Ndio maana hata uongozi mdogo mtu wa ngazi ya familia ambao ndio kipimo cha busara ya mtu umemshinda.

Hali inayosababisha mtu mzima wa miaka karibu sabini anaonekana hadharani eti ana mchumba kwa zaidi ya miaka mitano ina maana anazini.

Wahoji ; anatumia kigezo gani kushindwa kuoa

1) hana hela ?
2) ameshindwa kupata ridhaa ya wazazi wa mke ?
3) anogopa mtu mzima kuonekana kaoa mwanawe ? au
4)anaogopa kuoa kwa kuwa anaogopa amezoea kuacha akiacha tena itakuwa kashfa kubwa kuliko sasa ?

Walalamikia viongozi wao kukosa uadirifu. Wahoji unawezaje kuendelea kuiunga mkono CHADEMA wakati Una maswali yote haya kichwani unanishawishi vipi kumchagua SLAA na MBOWE yupo nae jirani yote hayo anayaona anapotezea au wote wale wale ?

Inasikitisha sana kwa namna CHADEMA inavyoendesha ni kama NGO's na baadidhi ya watu wakijaribu kuhoji ndio hawa wanaoitwa wasaliti na kutimuliwa ktk chama sasa haya ndio matokeo yake .R.I.P CHA DE MA'
 
Wabunge wote wa Chadema ni mateka wa Mbowe na Dr Slaa.

Maneno haya yangekuwa ya mtu mwingine ningeshangaa, lakini Ritz; kusema hivyo ni sawa. Lakini labda nikuulize, hujaona tusi lingine la kuwatukana wabunge wa CHADEMA mpaka. Ukatumia hilo?
 
Kwa hiyo unataka kutuambia na kutuaminisha kuwa mkutano wa bunge kuahirishwa kwa matukio ya maandamano Mtwara na mlipuko wa bomu kanisani Arusha pia ulikwa ni upuuzi...?

Kwa maoni yangu tukio hili halina tofauti na lile la kanisani Arusha so means spika pia alipaswa kuahirisha bunge kwa siku ya leo ili baadhi ya wabunge waje kutoa pole pia Arusha...!!

basi wavunje bunge tujue moja,kama kila kitu kinachotokea bunge linaahirishwa lini watajadili mambo yanayohusu taifa.
 
Sikutegemea uamuzi mbovu kama huu unaweza kufanywa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni-KUB ya kuwalazimisha wabunge wote wa CHADEMA wasitishe kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti vinavyo endelea na kwenda jijini Arusha kuhudhuria maziko ya wananchi waliofariki kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea kwenye Mkutano wa CHADEMA.

Kuna haja gani ya wabunge wote kwenda Arusha na kukaa kusubiria maziko ambayo hayaeleweki yanafanyika lini?? Bila shaka huu ni mtaji wa kisiasa unatafutwa kupitia vifo vya watanzania wenzetu. Mh Mbowe yawezekana kasahau kabisa kazi ya Kambi ya Upinzania Bungeni-KUB?? Au ndiyo kusema wenzetu mmelidhishwa na bajeti hii iiyosomwa bungeni?? Kwa hili sisiti kutamka wazi wazi huu uamuzi ni wa kipuuzi na hauna tija kabisa mbele ya watanzania, waacheni wabunge wafanye kazi zao za kibunge kwa kuhakikisha wanawatetea na kuwatumikia watanzania waliowapa fursa ya kuingia bungeni.

KWA HAYA NAANZA KUONA UMUHIMU WA WAGOMBEA BINAFSI HAPA NCHINI AMBAO HAWATAPELEKESHWA NA VIONGOZI WAO

Tangu nijiunge hapa jamii forum kwa mara ya kwanza kabisa naona kumbe kuna watu wapuuzi kama wewe, nani aliyesema CHADEMA wakiwepo bungeni ndo mambo yatabadilika wakati Godfrey Dhambi anafikiria jinsi ya kupata mgawo wake na sasa amekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa mmoja wapo hapa Tanganyika nawatahadharisha Halmashauri mnatakiwa kutenga fedha nyingi za kumgawia maana jamaa hataki mchezo. Ubinadamu na uatamaduni wa kitanzania ni kwamba inatakiwa mtu akifariki azikwe ndo muendelee na shughuli zenu. Watu wamefariki katika mkutano wa CHADEMA ulitaka waendelee na shughuli zingine? Gaidi Mwigulu anafanya sherehe baada ya kufanikiwa kutekeleza ugaidi aliojifunza CHINA.
 
Sikutegemea uamuzi mbovu kama huu unaweza kufanywa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni-KUB ya kuwalazimisha wabunge wote wa CHADEMA wasitishe kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti vinavyo endelea na kwenda jijini Arusha kuhudhuria maziko ya wananchi waliofariki kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea kwenye Mkutano wa CHADEMA.

Kuna haja gani ya wabunge wote kwenda Arusha na kukaa kusubiria maziko ambayo hayaeleweki yanafanyika lini?? Bila shaka huu ni mtaji wa kisiasa unatafutwa kupitia vifo vya watanzania wenzetu. Mh Mbowe yawezekana kasahau kabisa kazi ya Kambi ya Upinzania Bungeni-KUB?? Au ndiyo kusema wenzetu mmelidhishwa na bajeti hii iiyosomwa bungeni?? Kwa hili sisiti kutamka wazi wazi huu uamuzi ni wa kipuuzi na hauna tija kabisa mbele ya watanzania, waacheni wabunge wafanye kazi zao za kibunge kwa kuhakikisha wanawatetea na kuwatumikia watanzania waliowapa fursa ya kuingia bungeni.

KWA HAYA NAANZA KUONA UMUHIMU WA WAGOMBEA BINAFSI HAPA NCHINI AMBAO HAWATAPELEKESHWA NA VIONGOZI WAO


Laiti ungekuwa umelipuliwa wewe au mwanao au mkeo au mumeo na kufa na hilo bomu, labda usingekuwa na nafasi ya kutoa hoja ya kipuuzi kama hii!!.

After all BUDGET inajadiliwa nadhani kwa zaidi ya wiki moja,problem iko wapi kutenga siku moja au mbili kumshukuru MUNGU kwa wokovu wake kwa sisi tuliopona ktk tukio hilo baya lililotendwa na MAHAYAWANI pamoja na kuwapa faraja baba,mama,kaka,dada na rafiki zetu waliofiwa pamoja makumi ya majeruhi wanagugumia na maumivu hospitalini?

Kwako wewe bajeti is more important kuliko UHAI wa watu wa3 waliokufa hapo ARUSHA
siyo?

Hivi tutakosea tukisema you are among wa washiriki wa kupanga na kutekeleza mauaji haya sasa mmekaa pembeni na kuanza kutusanifu na kutuletea kejeli kama hii!!?????


 
Revocatus unaoneshd ni jinsi gani usivyopenda maisha ya watanzani wenzako. Tena mimi nilidhani wabunge wote ukiacha utofauti wa vyama wataungana na wenzao wa CHADEMA katika hili kwa kwenda kuwatembelea wahanga na kutoa matamko makali ya kupinga lililofanyika.
Ila kwa jinsi ulivyo na level yako ya kufikiri na kufanya maamuzi unaona Mh. Mbowe amekosea dah.
Kama nusu ya watanzania wanafikiri kama wewe, basi maendeleo kupatikana Tanzania itakuwa taabu sana. Ila naimani dhama hizi watu kama wewe watakuwa wachache sana.
 
Naomba jibu maswali yafuatayo kwa ufasaha.

Una umri gani?

Una elimu kiwango gani?

Ulikunywa pombe aina gani jana?

Unafanya shughuli gani kujipatia kipato?

Je wewe ni mtanzania?

Na je kuna ndugu yake yeyote aliyeathiriwa na tukio lile?
 
Masikini kameachwa chenyewe ataishije sasa bila tegemeo lake jamani na alaaniwe aliyefanya kitendo hiiki
 
Back
Top Bottom