NINA MASHAKA NA UAMUZI HUU ULIOFANYWA NA Mh Mbowe:

Jospina

JF-Expert Member
Apr 19, 2013
2,421
1,387
Sikutegemea uamuzi mbovu kama huu unaweza kufanywa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni-KUB ya kuwalazimisha wabunge wote wa CHADEMA wasitishe kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti vinavyo endelea na kwenda jijini Arusha kuhudhuria maziko ya wananchi waliofariki kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea kwenye Mkutano wa CHADEMA.

Kuna haja gani ya wabunge wote kwenda Arusha na kukaa kusubiria maziko ambayo hayaeleweki yanafanyika lini?? Bila shaka huu ni mtaji wa kisiasa unatafutwa kupitia vifo vya watanzania wenzetu. Mh Mbowe yawezekana kasahau kabisa kazi ya Kambi ya Upinzania Bungeni-KUB?? Au ndiyo kusema wenzetu mmelidhishwa na bajeti hii iiyosomwa bungeni?? Kwa hili sisiti kutamka wazi wazi huu uamuzi ni wa kipuuzi na hauna tija kabisa mbele ya watanzania, waacheni wabunge wafanye kazi zao za kibunge kwa kuhakikisha wanawatetea na kuwatumikia watanzania waliowapa fursa ya kuingia bungeni.

KWA HAYA NAANZA KUONA UMUHIMU WA WAGOMBEA BINAFSI HAPA NCHINI AMBAO HAWATAPELEKESHWA NA VIONGOZI WAO
 
Taifa stars japokuwa jana imefungwa lakini ilicheza vizuri sana.
Juhudi zinahitajika kuzidi kuiunga mkono Taifa Stars.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia na kutuaminisha kuwa mkutano wa bunge kuahirishwa kwa matukio ya maandamano Mtwara na mlipuko wa bomu kanisani Arusha pia ulikwa ni upuuzi...?

Kwa maoni yangu tukio hili halina tofauti na lile la kanisani Arusha so means spika pia alipaswa kuahirisha bunge kwa siku ya leo ili baadhi ya wabunge waje kutoa pole pia Arusha...!!
 
Sikutegemea kwa mtanzania mwenye akili timamu kama wewe uandike ----- kama huu...hiyo bajeti ni ya nani? na waliokufa ni kina nani? ifike mahala tuache fikra za ajabu ajabu
 
Idadi ya Tembo wa Tanzania imepungua sana.
Ujangili unaofanywa na Kinana na makada wenzie wa CCM imechangia sana kumaliza tembo wetu.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia na kutuaminisha kuwa mkutano wa bunge kuahirishwa kwa matukio ya maandamano Mtwara na mlipuko wa bomu kanisani Arusha pia ulikwa ni upuuzi...?

Kwa maoni yangu tukio hili halina tofauti na lile la kanisani Arusha so means spika pia alipaswa kuahirisha bunge kwa siku ya leo ili baadhi ya wabunge waje kutoa pole pia Arusha...!!
Jamani mie nawaambia kuwa hawa jamaa wa buku 7 waacheni wajitekenye na kucheka wenyewe. Wameshasahau matukio yaliyotokea majuzi tuu ambayo hata mtoto wa darasa la pili angekumbuka. Bure kabisa hawa 7thou
 
Mkuu, siyo kweli wanakwenda kuomboleza msiba. wanaenda kuongeza nguvu na kutaka huruma ya wananchi ili waichague chadema kwenye uchaguzi wa udiwani ulioahirishwa. hawataomboleza msiba bali watatumia nafasi watakazopewa kuongea kwenye msiba kufanya kampeni za uchaguzi
 
Endeleeni na bunge lenu la Ndiyooooo,pitisheni bajeti yenu ya kukusanya kodi ya bia!kwa kuwa bomu halikulipuka kanisani au msikitini wana ccm hamna uchungu wala mlichopoteza
 
Sikutegemea kwa mtanzania mwenye akili timamu kama wewe uandike ----- kama huu...hiyo bajeti ni ya nani? na waliokufa ni kina nani? ifike mahala tuache fikra za ajabu ajabu

Kwani wewe unafikiri mzima huyo? Akili zake zimepeperushwa na bendera ya kijani.
 
Na ccm ni mali yako ndio maana watoto wa viongozi wa ccm ndio wenye madaraka na maamuzi nchi hii wanyonge hawana nafasi ccm.

mkuu, wanyonge gani ambao unawasema kuwa hawana nafasi katika nchi hii. mbona mie wazazi wangu ni wanyonge lakini natoa mchango mkubwa kwa taifa hili.
 
Alichosema mbowe ni. Sa hihi kabisa kwamba lile tukio lilipangwa na si bahati mbaya amesema pia kama ccm hawawezi kumudu mfumo wa vyama vingi waufute
 
naona mmeamua kujitengenezea post ya chai, hivi wewe una akili za kufikiria au za kuvuka kwenye mataa barabarani? huo uamuzi unaouona wewe wa kipuuzi ni vyema uuache kisha fanyeni wenu na wabunge wa ccm, sidhani kama jambo hili mtalipenda nyie ccm, maana mnaweza kujua muvi yote.
 
Kwani wewe unafikiri mzima huyo? Akili zake zimepeperushwa na bendera ya kijani.

mkuu, mtu akifa kinachoendelea ni mazishi. pia mtu amekufa peke yake lakini bajeti inaathiri taifa zima na ina madhara makubwa kama haitajadiliwa kiumakini kuliko hata hilo bomu
 
I knew tungeishia hapa.. lile bomu wa plan .. huku wakijua kuna vikao muhimu vya bunge na kama wasipohudhuria sababu ya msiba .. spotlight itageuka kwao ...

Watanzania sio wapumbavu Mbowe.. even a primary school kid anaweza ku connect dots....
 
Usipotezee watu muda wa kusoma mada kama hizi ambazo naamini hata wewe mwenyewe muanzishaji unajua nafsini mwako kwamba hazina maana yoyote.
 
Sikutegemea uamuzi mbovu kama huu unaweza kufanywa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni-KUB ya kuwalazimisha wabunge wote wa CHADEMA wasitishe kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti vinavyo endelea na kwenda jijini Arusha kuhudhuria maziko ya wananchi waliofariki kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea kwenye Mkutano wa CHADEMA.

Kuna haja gani ya wabunge wote kwenda Arusha na kukaa kusubiria maziko ambayo hayaeleweki yanafanyika lini?? Bila shaka huu ni mtaji wa kisiasa unatafutwa kupitia vifo vya watanzania wenzetu. Mh Mbowe yawezekana kasahau kabisa kazi ya Kambi ya Upinzania Bungeni-KUB?? Au ndiyo kusema wenzetu mmelidhishwa na bajeti hii iiyosomwa bungeni?? Kwa hili sisiti kutamka wazi wazi huu uamuzi ni wa kipuuzi na hauna tija kabisa mbele ya watanzania, waacheni wabunge wafanye kazi zao za kibunge kwa kuhakikisha wanawatetea na kuwatumikia watanzania waliowapa fursa ya kuingia bungeni.

KWA HAYA NAANZA KUONA UMUHIMU WA WAGOMBEA BINAFSI HAPA NCHINI AMBAO HAWATAPELEKESHWA NA VIONGOZI WAO

mkuu, ndo kusema leo hatutakuwa na malalamiko ya kambi ya upinzani kuhusu bajeti ya serikali?
 
Acha u.mbulula CDM ni lazima waonyeshe kwa vitendo kuwa wamechukizwa na kitendo hicho
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom