NINA MASHAKA NA UAMUZI HUU ULIOFANYWA NA Mh Mbowe:

Kwa sababu huwezi hata siku moja kusifu mawazo ya Mbowe, basi utaendelea kupinga. Safari ya Mbowe na wabunge wote wa CHADEMA Arusha ni ya muhimu sana kuliko hata hilo bunge. Pale bungeni hoja za upinzani hata siku moja zinapingwa na hivyo hata wao kukaa pale ni jambo la kupoteza muda. Hivi ushaona wapi mchango wa wabunge wa maana ukabadilisha au ukaboresha bajeti ya serekali? Au unataka uendelee kudanganywa kuwa tumeongeza hela kwenye bajeti ya maji alafu mwaka unapita hela iliyotengwa kwa ajili ya wizara ya maji imetolewa chini ya 50%.

Bomu limetokea wakati wa mkutano wa CHADEMA na hivyo wabunge wa CHADEMA lazima waonyeshe solidarity na sympathy kwa watu wa Arusha. Au unadhani hao waliofariki si wamaana kuliko wale waliofariki kule Mtwara wakati bajeti ya wizara ya madini na nishati ikisomwa?

MImi kwa kweli nina mashaka na uzalendo wako pamoja na fikira zako
 
Kwaiyo ulitaka cdm wakae bungeni wakati wakipulizwa kiyoyozi uku wananchi wasio na hatia wanauwawa kule Arusha? Ulitaka CDM wasifanye chochote tu watulie kimyaaaa?!!?wewe waluokutuma kawambie hata muendele kuuwa wananchi kulipua makanisa na kutisha wandishi wa habari ni lazima mtang'oka tu mwisho wenu umekaribia kabidhini vijiti.Mshazeeka hamna jipya.Cdm ni chama cha kutetea wanyonge waliilipuliwa juzi na maskiskiem.Hamna hata aya eti mnaunda tupe ya uchunguzi ya nini sasa wakati hamna atakayekamatwa na mtuhumiwa alisaidiwa na jeshi la polisi kutoroka baada ya wananchi kumuona na kuanza kumkimbiza alafu polisi wakawazuia wananchi kwa kupiga risasi hewani zen jamaa akasepa zake.Ila siku ipo hata mandela alipigwa sana mwisho akashika Dola
 
Hata nabii eliya aliwaua manabii wa baali kwa upumbavu kama huu unaofanya leo, watu wamekufa alafu mnalazimisha nyekundu iwe njano, Huu ni ujinga haukubaliki... Sht..

sasa wewe unamfuata elia au unamfuata yesu?
Yesu alisema muwasamehe wanaowakosea,akasema ukipigwa shavu la kushoto ugeuze na la kulia.ndo maana nakuuliza mkuu kwakua ulisema humu kuwa unatoka family ya kilokole na wewe ni mlokole mzuri tu,na walokole ni wafuasi wa yesu ambae kasema muwe wasamehevu,nikashangaa kuona lugha unayotumia,kwani mbowe na yesu nani kati ya hao unaemtii zaidi ya mwingine?
 
Sikutegemea kwa mtanzania mwenye akili timamu kama wewe uandike ----- kama huu...hiyo bajeti ni ya nani? na waliokufa ni kina nani? ifike mahala tuache fikra za ajabu ajabu

Ndugu yangu, nani kakwambia huyo Kashaga ana akili, hamna kitu hapo!!!! Huyo naye ni book 7 mkomavu. Ukiisha kuwa book 7, wewe inabidi uimbe tune ya Nape na kibaka Mwigulu basi, hakuna kufikiri.

Tiba
 
Cdm kwenye mikutano A, Kupiga kura C, Kushinda D. Ccm mikutano C, kupiga kura A, kushinda B.
 
aisee kumbe enh!!
so wataka kuniambia IDI azani atayajua matatizo ya kahawa ya wananchi wa MULA na KISIKI huko HAI?? Hadi ayasemee??
ishu sio idadi ya wabunge ishu ni uwakilishi.

Cha msingi hapa ni kuvumiliana.Wabunge wa CHADEMA wamekwenda kwenye msiba na msiba ni sehemu mojawapo ya mapito ya kila mtu.Wakikosa bungeni siku mbili au tatu siyo mwisho wa uwakirishi wao bungeni pia wapiga kura wao ni waelewa wameshaelewa kuwa wabunge wao hawakwenda huko kucheza disco bali wamekwenda kwenye matatizo na bila hivyo wawakirishi wa wananchi wasinge kwenda huko.wa kulaumiwa hapa ni aliye sababisha yote haya ni yule muuaji.
 
sikutegemea uamuzi mbovu kama huu unaweza kufanywa na kiongozi wa upinzani bungeni-kub ya kuwalazimisha wabunge wote wa chadema wasitishe kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti vinavyo endelea na kwenda jijini arusha kuhudhuria maziko ya wananchi waliofariki kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea kwenye mkutano wa chadema.

kuna haja gani ya wabunge wote kwenda arusha na kukaa kusubiria maziko ambayo hayaeleweki yanafanyika lini?? Bila shaka huu ni mtaji wa kisiasa unatafutwa kupitia vifo vya watanzania wenzetu. Mh mbowe yawezekana kasahau kabisa kazi ya kambi ya upinzania bungeni-kub?? Au ndiyo kusema wenzetu mmelidhishwa na bajeti hii iiyosomwa bungeni?? Kwa hili sisiti kutamka wazi wazi huu uamuzi ni wa kipuuzi na hauna tija kabisa mbele ya watanzania, waacheni wabunge wafanye kazi zao za kibunge kwa kuhakikisha wanawatetea na kuwatumikia watanzania waliowapa fursa ya kuingia bungeni.

Kwa haya naanza kuona umuhimu wa wagombea binafsi hapa nchini ambao hawatapelekeshwa na viongozi wao

kama unanufaika na ccm kwa mawazo yako ni sawa lakini kama huo ndo upeo wako wa kuelewa na kujenga hoja ni hasara kubwa mno kwako na vizazi vyako, pole !
 
Sikutegemea uamuzi mbovu kama huu unaweza kufanywa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni-KUB ya kuwalazimisha wabunge wote wa CHADEMA wasitishe kuhudhuria vikao vya bunge la bajeti vinavyo endelea na kwenda jijini Arusha kuhudhuria maziko ya wananchi waliofariki kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea kwenye Mkutano wa CHADEMA.

Kuna haja gani ya wabunge wote kwenda Arusha na kukaa kusubiria maziko ambayo hayaeleweki yanafanyika lini?? Bila shaka huu ni mtaji wa kisiasa unatafutwa kupitia vifo vya watanzania wenzetu. Mh Mbowe yawezekana kasahau kabisa kazi ya Kambi ya Upinzania Bungeni-KUB?? Au ndiyo kusema wenzetu mmelidhishwa na bajeti hii iiyosomwa bungeni?? Kwa hili sisiti kutamka wazi wazi huu uamuzi ni wa kipuuzi na hauna tija kabisa mbele ya watanzania, waacheni wabunge wafanye kazi zao za kibunge kwa kuhakikisha wanawatetea na kuwatumikia watanzania waliowapa fursa ya kuingia bungeni.

KWA HAYA NAANZA KUONA UMUHIMU WA WAGOMBEA BINAFSI HAPA NCHINI AMBAO HAWATAPELEKESHWA NA VIONGOZI WAO

angekufa baba yako ,au mama yako au mtoto wako. . . .ungeandika huu uha.ro wako hapa?
Mbona matukio ya Olasiti na mtwara bunge lilipoahirishwa hukuja kuha.ra hapa jukwaani?
Watu wamefiwa kikatili ,wanauchungu hebu acheni siasa zisizokuwa na tija kwenye uhai wa watu.
 
Lakini yote haya watu watakuja kujua tu ukweli ulipo na chadema sijui kama wanaweza kujitenga sana na suala hili siamini kama kwenda kwenye misiba na kuoneka kwa watu ni njia sahihi ya kukomesha uovu huu.
 
Back
Top Bottom