Nina hakika ujinga sasa umevuka mipaka

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,074
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa upumbavu ni sifa sawa na ilivyo ufupi au urefu; yaani huwezi kuubadili. Ina maana, kwa tafsiri ya Mwalimu Nyerere, mpumbavu huwezi kumbadilisha akawa mwerevu.

Pole sana ndugu zetu wa Hanang kwa janga hili kubwa lililowapateni.

Wananchi tuliposikia Rais anaenda Hanang tuliamini kuwa anaenda kuwapa faraja waathirika, sawa na baadhi ya wengine wanavyostahili kufanya.

Lakini kwa bahati mbaya inaonekana Serikali na ikulu imejaa watu wa ajabu, ambao wamevuka hata ule mstari wa ujinga. Badala ya kuifanya ziara ya Rais kuwa ni ziara ya kuwapa faraja waathirika, wao wakaigeuza ziara hiyo kuwa ya uchawa. Yaani ziara ya kumsifia na kumpamba Rais.

Hawa watu ambao kwa kweli wamevuka hata kiwango cha ujinga, walishindwa kumtafutia mahali sahihi Rais wakampambe kwa uchawa wao wa kinafiki mpaka wakatumie misiba ya watu wa Hanang? Wakaandaa mpaka vikundi vya sanaa, ambavyo badala ya kuwafariji waathirika, wao kàzi yao ikawa kumsifu na kumwabudu Rais.

Hivi kweli nchi hii tuna watu wenye upeo mdogo kiasi hiki? Siamini na wala sishawishiki kuamini kwamba Rais alikuwa anayatarajia hayo.

USHAURI
Mambo kama haya ya hovyo, yanampa ujumbe Rais kuwa ndani ya Serikali yake amejaza watu wa hovyo wasioelewa hata kitu gani kifanyike wakati gani!!
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa upumbavu ni sifa sawa na ilivyo ufupi au urefu; yaani huwezi kuubadili. Ina maana, kwa tafsiri ya Mwalimu Nyerere, mpumbavu huwezi kumbadilisha akawa mwerevu.
...
Vyeo walivyonavyo wamevipata kutokana na vitendo vyao vya kujikomba, kujipendekeza na kusifia kwa unafiki. Je, wataachaje kufanya vitendo hivyo wakati ndivyo vinawapatia shibe yao ya kila siku???
"Mtumikie kafiri ili upate mradi wako."
 
Cha kushangaza ujinga huu unazidi kushika Kasi hapa nchini. System imefanya makosa makubwa sana kuruhusu chama kimoja kukaa madarakani muda mrefu, tena kwa shuruti. Sifa za kijinga zinazidi kushika kasi baada ya kuwa na uhaba wa mafanikio tarajiwa. The worse is yet to come.
 
Cha kushangaza ujinga huu unazidi kushika Kasi hapa nchini. System imefanya makosa makubwa sana kuruhusu chama kimoja kukaa madarakani muda mrefu, tena kwa shuruti. Sifa za kijinga zinazidi kushika kasi baada ya kuwa na uhaba wa mafanikio tarajiwa. The worse is yet to come.
Kwa nchi zilizostaarabika na kuendelea, mtaji mkubwa kabisa kwa Serikali ni ELIMU KUBWA walizonazo Wananchi wao. Lakini kwa nchi ambazo hazijastaarabika na zilizo duni kwa maendeleo, mtaji mkubwa kabisa kwa Serikali ni UJINGA MKUBWA ULIOTOPEA walionao wananchi wake.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa upumbavu ni sifa sawa na ilivyo ufupi au urefu; yaani huwezi kuubadili. Ina maana, kwa tafsiri ya Mwalimu Nyerere, mpumbavu huwezi kumbadilisha akawa mwerevu...
Bams, tuna taifa la watu wa ajabu sana. Wanafurahia kufanya siasa kwenye maafa!!! Kwa maana nyingine serikali ya CCM inaombea maafa mengine yatokee ili wapate nafasi ya kufanya siasa. Cha ajabu wamezuia vyama vingine visiende na viongozi wa Chadema wamezuiriwa kuingia Hanang. Hivi kweli tunabaguana hadi kwenye misiba?? Hivi wanadhani wananchi ni wapumbavu kiasi hicho
 
Inaonekana huyo mama ndio zake hizo anapenda kusifiwa hata upepo ukivuma anataka apongezwe kwa upepo mzuri! Sasa hata maafa yakitokea anataka apongezwe pia, haya hongera bibie kwa mafuriko ya Hanang!
 
Ukweli ulio wazi ni kwamba,watu wanao mzunguka Rais Honorable causa ni reflection ya Raisi mwenyewe,hivyo basi hakuna haja ya kumtafuta mchawi kwa kumung'unya maneno wakati mchawi yupo dhahiri kabisa.

Nelson Mandella kasha wahi sema "ni vema viongozi wajao wa kiafrika kuwa na akili zaidi kuliko sisi wapigania uhuru maana yajayo yanahitaji akili na ujasili"

Sasa hawa tulio nao ni wapumbavu.
 
Cha kushangaza ujinga huu unazidi kushika Kasi hapa nchini. System imefanya makosa makubwa sana kuruhusu chama kimoja kukaa madarakani muda mrefu, tena kwa shuruti. Sifa za kijinga zinazidi kushika kasi baada ya kuwa na uhaba wa mafanikio tarajiwa. The worse is yet to come.
Mkuu Tindo,Tanzania hakuna Cha system bali kundi la wahuni wafaidika na mfumo huu wa utawala,Kuna hitajika nguvu ya umma kuleta mageuzi ndani ya taifa hili.
 
Mkuu Tindo,Tanzania hakuna Cha system bali kundi la wahuni wafaidika na mfumo huu wa utawala,Kuna hitajika nguvu ya umma kuleta mageuzi ndani ya taifa hili.
Kweli kabisa, huwa nasema bila machafuko au mapinduzi ya kiheshi tusitegemee mabadiliko yoyote ya maana.
 
Mkuu Tindo,Tanzania hakuna Cha system bali kundi la wahuni wafaidika na mfumo huu wa utawala,Kuna hitajika nguvu ya umma kuleta mageuzi ndani ya taifa hili.
"Katika nchi za Afrika hakuna Serikali, bali kuna magenge ya watu walioshika silaha na kupora rasilimali za nchi ili kujinufaisha wao wenyewe binafsi pamoja na vibaraka wao."
Jonas Savimbi, aliyekuwa Mwanasiasa na Mwanamapinduzi wa nchini Angola.
 
Yaaani porojo zako zote ulizo piga hapa ni kwa kuwa tu mh Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania anapongezwa kwa kazi nzuri na maelekezo yake watendaji wa serikali kwa ajili ya kuwasaidia wahanga na majeruhi wa mafuriko ya Hanang eneo la kateshi. Kinachokutesa wewe siku zote ni chuki zako binafsi kwa mh Rais na li roho lako baya lililojaa wivu hasa baada ya kuona mh Rais akiendelea kuchanja mbuga katika mioyo ya watanzania.
 
Ukweli ulio wazi ni kwamba,watu wanao mzunguka Rais Honorable causa ni reflection ya Raisi mwenyewe,hivyo basi hakuna haja ya kumtafuta mchawi kwa kumung'unya maneno wakati mchawi yupo dhahiri kabisa.

Nelson Mandella kasha wahi sema "ni vema viongozi wajao wa kiafrika kuwa na akili zaidi kuliko sisi wapigania uhuru maana yajayo yanahitaji akili na ujasili"

Sasa hawa tulio nao ni wapumbavu.

Upo sahihi.

Nina hakika kama Rais asingekuwa anapenda huu upuuzi wa sifa za kinafiki, lazima ungekoma.

Mwalimu Nyerere, wakati wa uongozi wake walitokea watu wanafiki wakawa wanajikomba kwake, wakamwita ni Musa wa Tanzania. Mwalimu alichukia, aling'aka hadharani. Akasema lile kuniita mchongameno nimekubali, lakini hili la Musa, sitaki, sitaki kabisa kulisikia. Hakuna aliyemwita tena kwa jina hilo.

Kuna watu kwa kutaka kujipendekeza kwa mwalimu, wakawa wanabwagiza kwenye mikutano kwa kusema, 'zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM', mwalimu akang'aka, akawauliza, yaani zidumu fikra za mwenyekiti hata zisipokuwa sahihi? Ndipo wakabadilisha wakawa wanasema, zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa CCM.

Mara baada ya uhuru, wapo walioanza kumwita Mwalimu Nyerere, Mheshimiwa, Mwalimu akakemea na kusema kuwa waheshimiwa ni wananchi. Akawaambia wamwite 'ndugu', kama hawataki kumwita ndugu, wamwite Mwalimu.

Lakini haya ya sahizi, tena mengine hayana hata heshima kabisa, yanang'ang'ania yaitwe "mheshimiwa".

Siku zote matendo ya wasaidizi huashiria hulka za mkubwa wao. Kama Rais asingekuwa anapenda kusifiwa na kutukuzwa, kusingetokea tena mtu wa kumfanyia hayo.
 
Yaaani porojo zako zote ulizo piga hapa ni kwa kuwa tu mh Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania anapongezwa kwa kazi nzuri na maelekezo yake watendaji wa serikali kwa ajili ya kuwasaidia wahanga na majeruhi wa mafuriko ya Hanang eneo la kateshi. Kinachokutesa wewe siku zote ni chuki zako binafsi kwa mh Rais na li roho lako baya lililojaa wivu hasa baada ya kuona mh Rais akiendelea kuchanja mbuga katika mioyo ya watanzania.

Wewe bila shaka ni punguani. Niwe na chuki na Rais, kwani nina ugomvi naye wa kitu gani. Kwani kuna chochote ninachoshindania naye? Kwanza ninyi machawa wajinga ndio mnaomfanya Rais wakati mwingine asemwe vibaya.

Wewe endelea kuweka namba yako ya simu hapa ukiamini Rais hana uwezo wa kuwatambua watu wanafiki.
 
Upo sahihi.

Nina hakika kama Rais asingekuwa anapenda huu upuuzi wa sifa za kinafiki, lazima ungekoma.

Mwalimu Nyerere, wakati wa uongozi wake walitokea watu wanafiki wakawa wanajikomba kwake, wakamwita ni Musa wa Tanzania. Mwalimu alichukia, aling'aka hadharani. Akasema lile kuniita mchongameno nimekubali, lakini hili la Musa, sitaki, sitaki kabisa kulisikia. Hakuna aliyemwita tena kwa jina hilo.

Kuna watu kwa kutaka kujipendekeza kwa mwalimu, wakawa wanabwagiza kwenye mikutano kwa kusema, 'zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM', mwalimu akang'aka, akawauliza, yaani zidumu fikra za mwenyekiti hata zisipokuwa sahihi? Ndipo wakabadilisha wakawa wanasema, zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa CCM.

Mara baada ya uhuru, wapo walioanza kumwita Mwalimu Nyerere, Mheshimiwa, Mwalimu akakemea na kusema kuwa waheshimiwa ni wananchi. Akawaambia wamwite 'ndugu', kama hawataki kumwita ndugu, wamwite Mwalimu.

Lakini haya ya sahizi, tena mengine hayana hata heshima kabisa, yanang'ang'ania yaitwe "mheshimiwa".

Siku zote matendo ya wasaidizi huashiria hulka za mkubwa wao. Kama Rais asingekuwa anapenda kusifiwa na kutukuzwa, kusingetokea tena mtu wa kumfanyia hayo.
Mtu mwenye akili timamu siku zote,huwa hapendi sifa za kijinga ambazo mwisho huutweza utu,lakini kwa mtu mpumbavu sifa huwa sehemu ya maisha yake ili kuficha udhaifu au madhaifu yake.

Na pale wanapo tokea watu wa objective truth,huonekana kama tishio kwa wapenda sifa na watoa sifa.Hata huu Uzi wako muda sio mrefu utavamiwa na waimba mapambio ili kuonesha kiwango Chao kidogo Cha fikra.
 
Back
Top Bottom