Nimuache au nimuoe huyu msichana?

Nimuache au nimuoe huyu msichana?

Mudundo

Member
Joined
Apr 3, 2014
Posts
38
Reaction score
9
Hamjambo wadau?

Namuomba ushauri wenu wa busara. Mimi kuna msichana ambaye nilimpenda sana. Juzi nilipomwambia bayana yangu kwake kuhusu MAPENZI kwa sababu nataka kumuoa alinipatia masharti mawili la kwanza aliniambia nimnunulie Simu ya tachi sharti la pili anipeleke kwa wazazi wake.

Sasa na hisi kuwa hajanipenda bali anamathamanio ya vitu vya kidunia zaidi kuliko mapenzi ushauri wenu kwangu ni mununulie hiyo simu au niachane naye? Nisaidieni wadau huyu msichana ananiumiza kimawazo.
 
Mnunulie kwani simu tsh ngapi na imani hajaomba iPhone 7 hivyo mnunulie ya bei rahisi. Labda anataka kuboresha mawasilano baina yenu. Lakini kwanza mpime dhamira yake kama ni mkweli
 
Tena mwambie kwa mapenzi yote kuwa mpenzi wangu kwa sasa sina hiyo pesa ila nakuahidi mwisho wa mwezi huu nitakununulia nipe muda nakupenda sana mpenzi wangu naahidi nitakupa chochote kilicho ndani ya uwezo wangu. Kama binti anakupena na ana malengo na wewe atakuvumilia.
 
Kwan simu Shiling Ngapi Mkuu......

Hayo masharti ndio yanayokupa stress Au una kingine ......

Uwe na maamuz kwenye Vitu vidogo kama hivi
 
Mnunulie mpendwa huoni aibu wewe una simu za tach umpendae ana tochi???

Acha tu shoga mimi niliwahi kuwa na bf ana drive ndinga kali mjini ana gari za kifahari kama Range, discovery lakini mpenzi wake hata ka vits nilikuwa sina. Vitu vingine wanaume muwe mnajiongeza nilimuacha sababu niliona huyu hakuwa na mimi kwa malengo.
 
Yaani umeombwa simu tuu unakuja kulalamika humu khaaaa ....... tatzo mademu zenu wanawaendekezaga saanaa
 
Acha tu shoga mimi niliwahi kuwa na bf ana drive ndinga kali mjini ana gari za kifahari kama Range, discovery lakini mpenzi wake hata ka vits nilikuwa sina. Vitu vingine wanaume muwe mnajiongeza nilimuacha sababu niliona huyu hakuwa na mimi kwa malengo.


Wakati mwingine ni heri kuwa mwenyewe kulikoni kugandana na watu kama hawa
 
Mkuu usikilize moyo wako unasemaje halafu changaya na mawazo ya wadau utoe uamuzi wako.

Ukiona moyo unamkubali zaidi unaweza kumfanyia hayo yote ingawa angekuwa na akili angetanguliza suala la kukupeleka kwa wazazi wake hayo mengine badae.

Maana siku hizi vijana tuko tofauti sana siyo waoaji bali tunapenda kutandika papuchi na kukimbia.

Ila dalili niliyoiona hapo ipo siku utaambiwa kama unataka papuchi yangu naomba uninunulie gari baada ya kuwa umemueka ndani.
 
Nawaza tu Kama uwezi kumpa mpz wako sim bila hata kuomba ushauri kweli kuna siku utawaza kumpa gari? Watu wengine wabahili by nature anaona bora anywe pombe
 
Acha tu shoga mimi niliwahi kuwa na bf ana drive ndinga kali mjini ana gari za kifahari kama Range, discovery lakini mpenzi wake hata ka vits nilikuwa sina. Vitu vingine wanaume muwe mnajiongeza nilimuacha sababu niliona huyu hakuwa na mimi kwa malengo.

Hebu na nyie msiwe na mawazo tegemezi! Kwa vile jamaa anaendesha basi na wewe akununulie gari? Ndio maana mnanyanyasika! Kama hizo gari ni za dingi wake je? Pambaneni kivyenu, mtakuwa huru zaidi!
 
Hebu na nyie msiwe na mawazo tegemezi! Kwa vile jamaa anaendesha basi na wewe akununulie gari? Ndio maana mnanyanyasika! Kama hizo gari ni za dingi wake je? Pambaneni kivyenu, mtakuwa huru zaidi!

Kwa hiyo wewe ndio unamjua sana kuliko mimi niliekuwa mpenzi wake au ??
 
Ninatatizika kidogo, hiyo simu ya touch ni sehemu ya mahari au ni sehemu ya awali ya masharti ya kukubaliwa? Maana naona kama kuna utoto fulani hivi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom