Mimi ni mtumishi wa serikali ngazi ya mshahara TGTS D,nimeolewa na nina mtoto mmoja, pia ninaishi na watoto wengine wawili ambao tunawasomesha secondari. Kwa ujumla maisha ni magumu ukilinganisha kipato na hiyo extended family.
Tatizo langu ni kwamba nina mdogo wangu wa kiume ambaye alimaliza form six mwaka jana akapata division three masomo ya arts, kutokana na hiyo division na nature ya masomo na jinsia yake, kupata mkopo wa kujiunga na chuo kikuu si rahisi hivyo nikamshauri akasomee kwanza diploma ya ualimu ambayo hata mie mlezi wake nitamudu kumlipia ili angalau apate kazi.
Tangu mwanzo kijana hapendi kusikia neno ualimu, anataka kusikia kazi zile zenye mapesa mengi lakini kutokana na economic background inakuwa ngumu kumlipia ada kwenye kozi anayotaka. Hivyo tulijitahidi kumshauri na kumpa mifano hai na baadaye akakubali. Lengo la kumshawishi akasomee ualimu ni kwamba ataweza kupata ajira kirahisi na pia kujiendeleza ni rahisi na pia pesa atakayolipwa itamsaidia kujiendeleza mwenyewe kwenye profession aitakayo. Nikajitahidi kumtafutia chuo cha serikali kikapatikana na nikalipa ada na mtumizi mengine.
Sasa baada ya TCU kutoa majina alipata chuo kikuu kama alivyotaka ila kwa bahati mbaya hakupata mkopo kitu ambacho na mie nilimdokezea toka mwanzo kwamba kupata mkopo si rahisi. Lakini kijana aliamua kuacha mafunzo ya ualimu na kwenda huko IFM bila hata ya kuniambia mimi dada yake toka mwaka jana 2010,mwezi wa 11 . Amefuatilia mkopo mpaka amechemka sasa ndo anatuma ujumbe eti hajapata mkopo nimtumie pesa.
Jamani kama mnavyoyajua maisha ya chuo, accommodation, stationery, meal, na vingine vingi. kwa uwezo wangu kamwe siwezi kulipa hata kama nitasema tutakula majani ili kijana asome, Mbaya zaidi kule chuoni kwenye diploma alitoroka na hawawezi kumpokea tena. Mpaka aombe upya mwakani.
Nategemea mawazo kutoka kwenu, source ni mimi mwenyewe!
Tatizo langu ni kwamba nina mdogo wangu wa kiume ambaye alimaliza form six mwaka jana akapata division three masomo ya arts, kutokana na hiyo division na nature ya masomo na jinsia yake, kupata mkopo wa kujiunga na chuo kikuu si rahisi hivyo nikamshauri akasomee kwanza diploma ya ualimu ambayo hata mie mlezi wake nitamudu kumlipia ili angalau apate kazi.
Tangu mwanzo kijana hapendi kusikia neno ualimu, anataka kusikia kazi zile zenye mapesa mengi lakini kutokana na economic background inakuwa ngumu kumlipia ada kwenye kozi anayotaka. Hivyo tulijitahidi kumshauri na kumpa mifano hai na baadaye akakubali. Lengo la kumshawishi akasomee ualimu ni kwamba ataweza kupata ajira kirahisi na pia kujiendeleza ni rahisi na pia pesa atakayolipwa itamsaidia kujiendeleza mwenyewe kwenye profession aitakayo. Nikajitahidi kumtafutia chuo cha serikali kikapatikana na nikalipa ada na mtumizi mengine.
Sasa baada ya TCU kutoa majina alipata chuo kikuu kama alivyotaka ila kwa bahati mbaya hakupata mkopo kitu ambacho na mie nilimdokezea toka mwanzo kwamba kupata mkopo si rahisi. Lakini kijana aliamua kuacha mafunzo ya ualimu na kwenda huko IFM bila hata ya kuniambia mimi dada yake toka mwaka jana 2010,mwezi wa 11 . Amefuatilia mkopo mpaka amechemka sasa ndo anatuma ujumbe eti hajapata mkopo nimtumie pesa.
Jamani kama mnavyoyajua maisha ya chuo, accommodation, stationery, meal, na vingine vingi. kwa uwezo wangu kamwe siwezi kulipa hata kama nitasema tutakula majani ili kijana asome, Mbaya zaidi kule chuoni kwenye diploma alitoroka na hawawezi kumpokea tena. Mpaka aombe upya mwakani.
Nategemea mawazo kutoka kwenu, source ni mimi mwenyewe!