Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,804
- 11,261
natoa shukrani kwa michango yenu yote na ningejaribu kumjibu mmoja mmoja lakini kama mnavyojua ttcl yetu hii na mitandao ya kudandia.
Naomba niseme tatizo si fedha zake kwani na mimi nina za kwangu na nina uwezo wa kuishi vizuri tu. Mwanzoni nilifikiri ni mtu wa urafiki tu lakini aliponipa hizo za kunidondokea ndio nimepata na utata. Hivi nikiamua kuanza kumchunia si atanielewa vibaya na anaweza kuanza kudai "yote aliyonifanyia" mimi na mwanangu?
Au niamue kumlipa "kiaina" yaishe huku nikijua siwezi kuwa naye? Lakini pia maisha ya kuishi single muda mrefu nayo si mazuri kwani Mungu alituumba wawili wawili.
Nimeuliza hapa si mimi tu kuna mabinti wengine ambao wao hawana hata watoto lakini wanajikuta na utata huu wa kutembea na waume za watu hasa hawa waheshimiwa wetu. Au na sisi tuingie kwenye haya ya kuwakamua tu na kuwachuna?
nadhani nitafikia uamuzi na asanteni sana. Bimkubwa, nashukuru kwa ushauri wako. Umenisaidia sana.
Asanteni.
natoa shukrani kwa michango yenu yote na ningejaribu kumjibu mmoja mmoja lakini kama mnavyojua ttcl yetu hii na mitandao ya kudandia.
Naomba niseme tatizo si fedha zake kwani na mimi nina za kwangu na nina uwezo wa kuishi vizuri tu. Mwanzoni nilifikiri ni mtu wa urafiki tu lakini aliponipa hizo za kunidondokea ndio nimepata na utata. Hivi nikiamua kuanza kumchunia si atanielewa vibaya na anaweza kuanza kudai "yote aliyonifanyia" mimi na mwanangu?
Au niamue kumlipa "kiaina" yaishe huku nikijua siwezi kuwa naye? Lakini pia maisha ya kuishi single muda mrefu nayo si mazuri kwani Mungu alituumba wawili wawili.
Nimeuliza hapa si mimi tu kuna mabinti wengine ambao wao hawana hata watoto lakini wanajikuta na utata huu wa kutembea na waume za watu hasa hawa waheshimiwa wetu. Au na sisi tuingie kwenye haya ya kuwakamua tu na kuwachuna?
nadhani nitafikia uamuzi na asanteni sana. Bimkubwa, nashukuru kwa ushauri wako. Umenisaidia sana.
Asanteni.
Kwanini hukumwambia hivi: Siwezi kuwa nawe k/sbb unae mke badala ya kumuuliza ulivyomuuliza? Kujiamini ndiko kunakupa msimamo, dada!
Nimepatwa na utata kidogo, sina mahali pengine pa kuuliza bila kujulikana na ninaomba ushauri wa kweli.
Mimi ni mama single, mwanangu ana miaka minne tu. Mimi na baba yake tuliachana kama mwaka mmoja na nusu baada ya yeye kuamua kuzaa nje ya ndoa yetu.
Nikajitutumua mimi mwenyewe na kwa kiasi kikubwa nimeweza kufanya mambo yangu mimi mwenyewe na maisha siyo mabaya sana. Hata hivyo karibu mwaka mmoja sasa nimekuwa nikijidedicate kumhudumia mwanangu na kuandaa maisha bora ya huko mbeleni na hasa kuamua kukaa single.
Nimekuwa nikiwatolea wengi nje kwa sababu najua wanachotaka ni kitu kimoja tu. Sasa tangia kikao cha februari kuna mheshimiwa mmoja ambaye amekuwa akinionesha ukaribu na ukarimu katika mambo mengine na tangu wakati huo hajagusia neno lolote la mapenzi kiasi cha kuanza kumuamini na pole pole nimeanza kujikuta ninavutwa kwake. Hata hivyo sikumtumia "signal" zozote za kuashiria ninavyojisikia.
Sasa wamekuja hii juzi na akanikaribisha DDM Hotel kwa chakula cha mchana na akanidondoshea hilo bomu kuwa ananitaka. Sasa tatizo ni kuwa huyu bwana ana mke na watoto (mmoja ameondoka majuzi kwenda US), na mke wake ni mtumishi pia serikalini. Anataka nimpe jibu kabla hawajaondoka na amenihakikishia kuwa ati nisiwe na wasiwasi mimi na mwanangu tutaishi vizuri tu.
Nilimuuliza kwanini anataka kuwa nami wakati ana mke? kasema ati mke wake yuko busy sana na hawezi kusafiri mara nyingi na majaribu mengi njiani anataka awe na "mtu" ambaye anamjali n.k
Kwa kweli, najua ni jambo la kipuuzi lakini mwenzenu nimetingwa. Naomba ushauri.
asanteni and I'm out.