Nimkubalie?


Kama walivyosema wengi jibu unalijua. Wewe ulishafanyiwa na unajua chungu yake sasa kwa nini unataka kujiingiza huko? Hauna haja ya kumchunia wala kumchukia maana yeye kama mwanaume yeyote katupa ndoana yake na kuna kupata na kukosa. Ukimtema, mteme kiungwana na kama ni muungwana kweli basi uhusiano wenu utakomaa zaidi maana mipaka itakuwa inajulikana kwa wote. Hawezi kukudai chochote maana alifanya yote kwa mapenzi yake. Na kudai kunaweza kumlipukia maana haitakuwa siri tena kuwa alitoa kwa malengo gani.

Ukiamua kumshukuru kiaina, ufanye ukijua kuwa na wewe utajulikana tu. Kama vile wewe ulivyomstukia mwenzio (au tatizo lilikuwa ni yeye kuzaa na sio kuwa na uhusiano nje?). Upete ukijua kuwa kama itatokea siku akatokea anayekutaka na yuko huru patakuwa na kazi! Jamaa dizaini hii ni ving'ang'anizi ile mbaya.

Lakini nina wasiwasi. Is this for real? Maana kwa simulizi zako kama jamaa anapitia humu atakuwa ameishajijua!

Asante.
 

Uamuzi wa Busara ni kumsamehe na kumrudia Mzazi mwenzako au kuamua kuishi kama mseja. Kuwa hawara ni kujidhalilisha na kupata UKIMWI.
 
Mwambie mkapime ngoma kama mambo yatakua mazuri wewe zuka nae.
 
Bwana wasikutishe,we kama unaamua kumpa Tunda we toa kama unaona gozi piga chini kwani hadi sasa utakuwa unajua nini ni nini.Kana ka nsungu aligusia mambo ta Sex na Love so hapo inabidi upime je wewe una nia gani na huyo jamaa..kama masilahi yako yakifikiwa basi you can go on...
 
After climbing a great hill, someone only finds there are more hills to climb onwards..
 
Nashindwa kuelewa mantiki ya huyu bibiye anaeuliza swali hili. Anadai aliachana na mumewe kutokana na tabia ya mume huyo kutembea nje ya ndoa. Sasa kuna faida gani kuachana na mume aliyetembea nje ya ndoa, na sasa unataka ukatembee nje ya ndoa na mwanamume mwingine anayetembea nje ya ndoa? Kulikuwa na mantiki gani ya kumwacha mume yule?
 
Mama, kama uliachana na mumeo kwa sababu ya kuzaa nje na ukuweza kumsamehe iweje sasa uwaletee wenzio shida. Unafikiri huyo mke wake akisikia kuwa mumewe anakidosho nje naye si atavunja ndoa yake na kwa hiyo tatizo la kuvunjika kwa zoa kuongezeka. Kama ulivyochukizwa kwa kitendo cha mumeo hivyohivyo usiwafanyie na wenzako hivyo
 
... dada hilo ni kanya boya achana na hilo dude na kama ameshakwambia ana mke na watoto sioni nafasi ya kupendwa sana sana unatafutwa kurogwa na mwenye mume. Tulia omba mungu utapata kitu cha kweli na cha uhakika hayo ma-advertise ya kusafiri na yuko busy yatakurudia siku moja. Si ujanua wanaume akila mzigo anatambaa na moto wake!!!
 
Kwa mtazamo wangu mi naona "mchane mbavu"..huyo anataka kukutumia tu pale anapojisikia na vile vile ana mke na watoto!Hakuna future hapo.. subiri ambaye hajaoa au kama jasiri na unaona unataka kuondoa upweke kwa kuolewa tafuta wa kukuoa..
 
Wewe ni mtu mzima, unajua kila kitu, kwani unataka kutuambia kwamba hukuwahi kutembea na mwanaume yeyote ila mme wako tu? Je kama ulishawahi unatuuliza nini, tumia mbinu ile ile unayotumia kwa wanaume wako wengine.
 
Kwanini hukumwambia hivi: “Siwezi kuwa nawe k/sbb unae mke” badala ya kumuuliza ulivyomuuliza? Kujiamini ndiko kunakupa msimamo, dada!

Watu wengine hawapendi maendeleo ya wengine. Kuwa na mke haijalishi my friend. Watu huoa hata wanne ebo?

Wewe sister kama mmeachana na jamaa fresh angalia tu usawa wa mbele. Huyu aweza kuwa mchumba.Labda kama hutaki mchumba aliyeoa. Ila ninahisi kumpata fresh itakuwa ngumu. Labda umpate aliyeachika , japo hata mimi ningeachika ningechagua msichana .
 
dadangu, inategemea utaamua kutumia akili au utashi au hisia kufanya maamuzi.
Kama uliwakatalia wote hao kabla, huyu kakupa nini? Lazima kuna cha zaidi.
mi navyoona unahitaji company wakati kama huu wakati akili yako inapopingana nguvu za vishawishi.
Hivi ulikuwa unafikiri kumkataa mwanaume ni kishawishi? La hasha dada!!
Kishawishi ni kumkataa mwanaume ambaye unamtamani. Mwili wote unauma, kila kitu anachosema unaona kama ukweli na kizuri, hapo ndio uko kwenye kishawishi manake unashawishika.
Sasa kama wewew huwezi kushinda vishawishi basi ndio hivyo tena. Endelea tu.
Lakini kama unataka support ya upweke na liwazo wakati unapigana na kishawishi tupo wakina dada JF.
Nakuusia tu, kuwa unaweza kuvishinda, ni kuamua tu, msaada ni kukaa mbali na kishawishi, mwili hauna nguvu sana, hivyo tumia akili kaa mbali, futa namba ya simu. badili vitu vyote vinavyowakutanisha.
Anyway, kama ukikuwa unadhani inawezekana ukwa nae comfortably kwa zaidi ya miaka 10, si kweli, uhusiano utakwisha mapema tu na utabaki mpweke.
 
Unajua kwanini anakutaka?? kwa kuwa kipya hakinyemi......,baadaye akikupata atalelkea kwenye kipya kingine .Kumbuka kwa kuwa huna ndoa naye utakuwa ndio basi tena afadhali ya mkewe wa ndoa akienda anrudi tena!!!! utaumizwa tena kisha uchukie wanaume kweli kweli !!! achana na huo ujinga !!!
 
mkuu mwanakijiji sasa ruksa kuchangia baada ya walio wengi kuchemsha
 
Mpe tu tundi lakini tumia kinga! Usikubali kuwa wa kudumu lakini mchune kisawasawa maana hawa waheshimiwa wanakula hela zetu bila kuzifanyia kazi. Akipatikana wa kuwachuna, mie naona ni bora ili wazipunguze kidogo. This advise is nonetheless without prejudice, and is given without any fiducial commitment!
 

Kuna mtu aliniambia kuwa adui ya mwanamke siyo mwanaume bali mwanamke mwenzake.
Ukimkubali halafu akakupa miwaya, usije ktk baraza kuomba ushauri jinsi ya kupona.
Angalia maisha ya mwanao (Innocent) kwanza kisha mengine yatafuata.....

......May be you look attractive, can i see you?????
 
Mimi ningekushauri u-make up na mume wako kama mlikuwa mmeoana. Of course, kama anajutia kwa dhati kosa alilolifanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…