Hope Kwema bandugu?
Straight kwenye mkasa, tupo marafiki watatu let's say A,B,C. A na B sisi ni mabachelor ila C ana mke na watoto 2. Mm A na C tumepanga nyumba yenye geti moja ila ndani kuna nyumba tatu hivyo kila mmoja ana getto lake na B anakaa kama mwendo wa dk 15 kwa miguu kutoka hapo kwetu na urafiki wetu sote ni kama 5 yrs HV na zaidi kwan ni toka nimehamia mkoa huu kikazi na apart from utani wa kawaida WA kirafiki ni watu ambao tulikuwa tunaheshimiana na kusaidiana sana kama ndugu, ila kama wiki tatu nyuma nilikuwa na tatizo ambalo lilinifanya niombe ruhusa kazini, hvyo nililala sana mpaka mida ya SAA 4 siku ya tukio, ile nakurupuka usingizin nataka kutoka nje nikasikia sauti ya mke wa C akiongea na mtu kwa ukali kama amekereka na jambo " hivi una akili ww mm Mali ya MTU jiheshimu" na huyo mwingine ni kama ananongoneza hata cmsikiii vizuri ikabidi nisifungue mlango
kwanza niende dirisha kuchungulia kwenye upenyo wa pazia, believe it or not Duh sikuamini ni B, macho yakanitoka, hasira kama yule ni mke wangu, akili kama sio zangu nashika mswaki narudisha ila baada ya muda kama dk 5 akaondoka na neno la mwisho niloskia kutoka kwa B ni NARUDI, kweli akatoka akili ikaniambia c huyu mwanamke afunge geti kwa ndani ila bwana ya shetani nayo Mengi hiyo akili haikumuingia (cjui ila hakulifunga) zaidi ya kumuona ni kama ana hasira za kuchukizwa na kilichotokea na chai aliyokuwa anakunya kwa pale nje ni kama haitaki tena. Kweli bhana Mara jamaa akarudi (nahs alienda kusoma ramani kwa nje) na kulianzisha tena "oh VP sasa.." Kabla hajamalisha nikasikia mke wa C akisema "Katafute wanawake wakotongoza huko nje na unikome" na mitusi kama 1000, baada ya kuona kawa mkali duh B speed getini katoka huku namuona kwa mbali anajichekesha. Yule wife wa C alikaa sana lile eneo ni kama anamawazo sana ikabidi nitoke maana hakuwa na dalili za kuamka pale huku nikijifanya nimetoka usingizini kwa kukunja sura na miayo kama 1000. Tukapeena hi nikawa natoka namuona nikama kuna kitu anataka kusema ila inajishauri mwisho wa siku akaniambia kama siendi mbali nimchulie azam kule nje. Mkasa ukaishia hapo. Ila toka cku hiyo huyu B staki mazoea nae akipiga cpokei akiniambia nipo na C venue zetu za kupata siendi na nataka nikate mazoea kabisaa pasipo C kujua kwa Nn maana huyu C najua hatamuelewa jamaa akijua. Ushauri wenu ndugu ... B na C wanafanya biashara zao (sio waajiliwa) hvyo wapo vizuri kidogo financial.
Note: True story na Mm ndo mhusika A.