Nimevamiwa na nyoka aisee ni hatari

Nimevamiwa na nyoka aisee ni hatari

litutumbwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
731
Reaction score
1,376
Jamani wanajamvi wazima? Hapa kwangu ninaishi na baadhi ya mifugo,nimewajengea mabanda maalumu uani...

Sasa jana jioni tu kuku wangu alishambuliwa mno,na ndiyo nilikuta nyoka ameshaingia bandani.

Yaani alikuwa ameshamuua jogoo sasa anamnyofoa nyama anakula. Nilikuta kashamla robo tayari na anaendelea kumega mapande ya minofu.

Ama kwa hakika nyoka ni hatari,tulimuua kwa msaada wa kerosene pia. Mkoani nyoka wengi sana... Mabaki ya kuku tukayafukia.

Kuweni makini jamani. Na nasikia nyoka aina ya kobra huwa wanatembea mume na mke, mkewe tulishamuua na huyu ni mumewe.

Huwa anaweza kuingia hata kupitia upenyo mdogo wageti.kuweni makini mno

NB:nyoka huyu alikua anatafuna kabisa minofu aliyonyofoa kwenye mwili wa kuku. Hii inaonesha ata mtoto mdogo anaweza kumla. Tuwe makini
 
Kuna eneo linaitwa Nala, Dodoma. Nilimkanyaga huyu nyoka Dec 31 usiku. Nikagundua kumbe binaadamu tunaweza kupaa basi tu uzembe wetu😅
Cobra
IMG_20221214_104530_4.jpg

 
Kuna eneo linaitwa Nala, Dodoma. Nilimkanyaga huyu nyoka Dec 31 usiku. Nikagundua kumbe binaadamu tunaweza kupaa basi tu uzembe wetu😅
Cobra
View attachment 2603894
😂 Pole sana.
 
🤣🤣🤣🤣 Unamaanisha, ulijibika umalaika Kwa muda mfupi
Acha tu yaani niliruka juu height kubwa sana nadhani hata masai niliwashinda.
Lakini hili tukio lilinifanya nigundue Mungu fundi sana kwenye upande wa response towards stimulus/Vichochezi.

Yaani ilinichukua muda wa 0.01second kuchukua hatua ya kuruka juu baada ya kumkanyaga. Nilivyomkanyaga mwili ukasisimka nikajiuliza nini hiki nimekanyaga kilaini hivi nikaruka. Yaani ndani ya muda mfupi sana. Nikawa nimefanya practical ya Topic ya Coordination
 
Acha tu yaani niliruka juu height kubwa sana nadhani hata masai niliwashinda.
Lakini hili tukio lilinifanya nigundue Mungu fundi sana kwenye upande wa response towards stimulus/Vichochezi.

Yaani ilinichukua muda wa 0.01second kuchukua hatua ya kuruka juu baada ya kumkanyaga. Nilivyomkanyaga mwili ukasisimka nikajiuliza nini hiki nimekanyaga kilaini hivi nikaruka. Yaani ndani ya muda mfupi sana. Nikawa nimefanya practical ya Topic ya Coordination
Nacheka kama mazuri🥺😂, pole sana .. mimi huwa sijawahi kuona hao viumbe kabisa vikiwa hai na naomba Sana Mungu nisiwaone maana dah sijui itakuwaje 😢
 
Kuna eneo linaitwa Nala, Dodoma. Nilimkanyaga huyu nyoka Dec 31 usiku. Nikagundua kumbe binaadamu tunaweza kupaa basi tu uzembe wetu
Cobra
View attachment 2603894


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha tu yaani niliruka juu height kubwa sana nadhani hata masai niliwashinda.
Lakini hili tukio lilinifanya nigundue Mungu fundi sana kwenye upande wa response towards stimulus/Vichochezi.

Yaani ilinichukua muda wa 0.01second kuchukua hatua ya kuruka juu baada ya kumkanyaga. Nilivyomkanyaga mwili ukasisimka nikajiuliza nini hiki nimekanyaga kilaini hivi nikaruka. Yaani ndani ya muda mfupi sana. Nikawa nimefanya practical ya Topic ya Coordination
🤣🤣🤣🤣🤣
 
Acha tu yaani niliruka juu height kubwa sana nadhani hata masai niliwashinda.
Lakini hili tukio lilinifanya nigundue Mungu fundi sana kwenye upande wa response towards stimulus/Vichochezi.

Yaani ilinichukua muda wa 0.01second kuchukua hatua ya kuruka juu baada ya kumkanyaga. Nilivyomkanyaga mwili ukasisimka nikajiuliza nini hiki nimekanyaga kilaini hivi nikaruka. Yaani ndani ya muda mfupi sana. Nikawa nimefanya practical ya Topic ya Coordination
 
Nacheka kama mazuri, pole sana .. mimi huwa sijawahi kuona hao viumbe kabisa vikiwa hai na naomba Sana Mungu nisiwaone maana dah sijui itakuwaje
Nyoka anatisha bwana

Miaka mingi kidogo nilikaa kwenye kibaraza mbele ya nyumba umeme umekatika, Sina hili wala lile

Ghafla nikahisi kitu chenye joto kinateleza kwenye nyayo zote za miguu, sielewi ilikuwaje ila nilisogeza miguu taratibu sana nikawasha tochi ya simu...Kuangalia nyoka ndio alikuwa anajiweka vizuri pale aiseeee niliruka hatari ile speed sijawahi kuwa nayo tukamuua

Siku tatu mbele nipo bafuni naoga nyoka kama yule yule ukubwa ule ule rangi ile ile namuona pembeni nashukuru nilikuwa sijavua nguo sijui ingekuwajenikatoka mbiiioooo na sikuoga Tena Kwa muda ule

Aiseee mama akaanza kulia wachawi wanamfuata mwanaeeti nyoka yule yule kafufuka..

Siku kadhaa mbele tukaua mwingine ila huyo alionwa na mwingine sio Mimi.

Tukahisi wamezaliwa pale ila hatukuwahi kumuona mama Yao wala baba yao
 
Nilikanyaga nyoka ,bahati nzuri nilikanyaga upande wa kichwani,niligundua alipoanza kujinyonganyonga mwili na kujiviringisha mguuni,akili ya haraka ikanijia kwamba kwakuwa mwili umeshajifunga mguuni nikiinua kuachia kichwa ataning'ata,nikakandamiza kiatu na kubana kichwa ardhini hadi alipojinyoosha kuashiria amekufa ndio nikamuachia,nikamfungua mguuni kwa mkono nikamtupia mbali.
 
Nyoka anatisha bwana

Miaka mingi kidogo nilikaa kwenye kibaraza mbele ya nyumba umeme umekatika, Sina hili wala lile

Ghafla nikahisi kitu chenye joto kinateleza kwenye nyayo zote za miguu, sielewi ilikuwaje ila nilisogeza miguu taratibu sana nikawasha tochi ya simu...Kuangalia nyoka ndio alikuwa anajiweka vizuri pale aiseeee niliruka hatari ile speed sijawahi kuwa nayo tukamuua

Siku tatu mbele nipo bafuni naoga nyoka kama yule yule ukubwa ule ule rangi ile ile namuona pembeni nashukuru nilikuwa sijavua nguo sijui ingekuwajenikatoka mbiiioooo na sikuoga Tena Kwa muda ule

Aiseee mama akaanza kulia wachawi wanamfuata mwanaeeti nyoka yule yule kafufuka..

Siku kadhaa mbele tukaua mwingine ila huyo alionwa na mwingine sio Mimi.

Tukahisi wamezaliwa pale ila hatukuwahi kumuona mama Yao wala baba yao
Jamani😢, mimi huwa nikiona tu kwenye TV vile anatembea mwili unasisimka vibaya mno, ila maandiko yanasema pia yamethibitisha binadamu na nyoka ni maadui wakubwa sana☹️
 
Back
Top Bottom