Lowasa unapaswa kuonyesha ubora wowote alionao katika hili. Umekuja CHADEMA baada ya kuona kiko safi na imara na kwamba kinakubalika ili udandie muunganishe nguvu. Wewe lengo lako likiwa ni kuiua ccm na kuwa raisi, huku ukitambua uwezo wako mdogo wa kujenga chama na hivyo ukitambua umahiri wa dr. Slaa katika kujenga chama na taifa imara.
Ukiona uliowakuta wanakukimbia, ujue wanakimbia na mchango wao katika kufanikisha azma yako pia. Hutaenda ikulu kwa mteremko wa CHADEMA uliyoikuta bila Dr. Slaa. Na sasa bila Dr. Slaa unaonekana wewe ni laana, umeleta laana CHADEMA kitu ambacho unapaswa kukikataa.
Ninakushauri kwamba umwombe Mungu sana akuondolee kiburi na hasira, pamoja na roho ya visasi uliyonayo.
Pili unatakiwa kuita press comference uruhusu maswali yote kutoka kwa waandishi ambayo wana maduku duku nayo juu ya histori yako iliyojaa maswali. Kuwajibu watu kwa kejeli kwamba mwenye ushahidi aende mahakamani, ni kashfa kwasababu ukweli unaujua.
Tatu sina imani na upenzi wako juu ya ChADEMA kama chama,ila katika ufahamu wangu naona unakipenda chaddema kama mtumbwi wa kukupeleke ikulu. Na hivo imani yetu kwako bila viongozi waliotufikisha hapa, haipo. Peke yako hukubaliki CHADEMA. Ili tujue chama chetu kinaendelea kuwa salama, na kwamba hata ukiwa Ikulu utaendeleza itikadi za CHaDEMa kwa ubora wake, tunataka uwarudishe viongozi wetu wanaokukumbia. Hao ndi tunaowaamini na siyo wewe kama wewe. Bila hivyo, hatukupeleki Ikulu Mheshimiwa kwa sasa. Tutahitaji kukaa na wewe miaka mitano ili tukufahamu rangi yako halisi juu ya uzalendo unaotaka tuuamini.
Nne, ninaomba Mungu uongee na wanasheria wa UKaWA juu ya maisha yako ukiwa ulikotoka ili wapime na kuona kama huna kosa la kuwekewa pingamizi tukakosa mgombea kwa ajili ya tamaa zako kumbe huna hata sifa.
Tano wafuasi wako, waambie wawe na adabu. Waache kukupigia debe kwa kumtukana Dr. Slaa wakidhani watamdhdoofisha iili upate nafasi ya bure usije kukatwa na huku. Tunawaelewa kwamba wengi ni wahuni tu hapa mitandaoni. Lakini wafahamu kwamba wanavyomtukana Dr. wanazidi kukuweka mbali na mioyo yetu. Ongea na watu wako uwaambie huku siyo ccm, hakuna cha kulilndana, wala kusimamia uovu.
Ukimrudisha Dr. Slaa, tutaungana kukupigia kampeni za nguvu tukiamini hujaleta laana ya mafarakano na kwa tamaa zako unaua CHADEMA.
Ninaomba Mh. Lowasa uingie kazini wala usikae kama mgeni ili ueleweke na upate Support ya CHADEMA ambayo ni muhimu sana kuliko madonda na vinyongo vilivyopo sasa dhidi yako.