yero
JF-Expert Member
- Mar 26, 2015
- 471
- 425
Wana JF hii kitu inaniumiza hasa kuna maneno nikisoma humu ndani, najisikia vibaya. Nampenda 'binti mkubwa' nahofia siku akijua atanichukuliaje, nawaza sana kama ataendelea hata kuongea na mimi, au nitamwambia kitu gani anielewe. Kiukweli nikiwa naye nikimwangalia usoni naumia sana nalazimisha kuwa kawaida mpaka kuna mda ananiuliza nina tatizo gani, namwambia hamna. Hadi chozi huwa linanilenga naamua kuzuga tu.
Mpenzi wangu nampenda sana, tunaongea kila siku kwenye cm, na ananitafuta kuliko hata mimi ninavyomtafuta. hajawahi kunifanyia chochote kibaya cha kulinganishia, kwa ninavyomjua siku akifaham ndio itakuwa mwisho wetu. Yupo mbali lakini naweza kuhisi mapenz yake kwangu kila tukiongea naye. Yan naweza kuwa huku nilipo na nikasema kwa ujasiri kuwa nina mpenzi.
Kubadilisha line, haitasaidia namba zote zipo kichwani.
Nikipotea kwenye ramani zao, nahisi nitaandamwa na mawazo na maradhi ya mawazo. Nikiwaambia, naogopa kuwapoteza. Nlivyokaa kimya bila kusema kitu ndo mawazo ya itakuwaje yananiandama usiku na mchana. Nawaza kama kuna siku haya mawazo yataisha na mimi kuwa huru bila kuwapoteza watu muhim kwenye maisha yangu.
Mwanzoni nilivyokusoma niliona chembe za sifa hivi, kumbe unaumia mkuu, pole sana. Hayo mawazo ukiyachukulia poa yatakuletea matatizo. Mpige chini 'bi mkubwa' haraka iwezekanavyo. Hao wawili endelea kuwachunguza utambue nani nafaa. M-block 'bi mkubwa' kwenye simu yako. Hama mtaa, halafu usiwaze sana taratibu utarudi kwenye hali ya kawaida