Hivi seriously wanaume hamuelewi kwanini mliambiwa muishi na sisi kwa akili? Nashangaaga baadhi ya wanaume wanatoa sababu zao ambazo hazina kichwa wala miguu wanaume mara nyingi mnatumia nguvu kwenye mambo yenu ila wanawake mara nyingi tunatumia akili kwenye mambo yetu
Labda nikuelezee kwanini nasema sisi tumewazidi akili ila ninyi mmetuzidi nguvu ngoja nitolee mfano labda katika swala la kuua mwanaume akitaka kuua atachukua silaha anayotaka kutumia kama ni bunduki au panga ataenda moja kwa moja kwa anayetaka kumuua atatekeleza mauaji halafu ataondoka
Ila mwanamke akitaka kuua anatafuta mazoea kwanza na huyo mtu halafu atajifanya rafiki yake na kumuweka karibu zaidi halafu pale ambapo huyo mtu kaanza kumuamini ndipo atatekeleza mauaji
Sasa najua kuwa wapo wanaume wanaoua kwa taratibu na wapo wanawake wanaoua kwa haraka sasa hizo ni exceptions tu na ni cases chache za hivyo na kama unabisha jiulize kwanini asilimia kubwa ya wanaoenda vitani ni wanaume halafu asilimia kubwa ya wanaotumika kwenye maswala ya ujasusi ni wanawake? Mind you kwenye vita kunahitajika nguvu nyingi kuliko akili na kwenye ujasusi kunahitajika akili nyingi kuliko nguvu
Kuna mfano mmoja ninao mwanamke alikuwa jasusi akatumwa na kitengo chao kuwa akatafute information za mwanaume fulani kitengo walikuwa wanazihitaji huyo mwanamke alijenga mazoea na huyo mwanaume wakaanzisha hadi mahusiano ya kimapenzi wakafunga ndoa wakazaa na watoto kumbe miaka yote hiyo mke hana mapenzi bali yupo kikazi tu
Mume kashamuamini mwanamke kwa asilimia mia moja na mke sasa anajua siri zote za mume wake ndipo mume anapokuja kugundua kuwa mke wake ni jasusi na taarifa za mume zote zishajulikana kitengoni basi wakafanya yao sasa niambie mwanaume anaweza kufanya hayo? Nina mifano mingi tu ya hivyo ila nimekupa huo mmoja sababu siwezi kuiandika yote hapa na ndo maana wanasema mwanaume asili yake ni ujasiri na mwanamke asili yake ni unafiki yaani mwanamke anakuua huku anakuchekea
Mungu aliposema muishi na sisi kwa sisi akili alimaanisha kwamba sisi tuna akili zaidi yenu yaani kwamba ninyi amewapa akili ila akili zenu hazijafikia za kwetu kwahiyo mnatakiwa mzipandishe zifikie za kwetu yaani ni sawa mtu akwambie binadamu uishi na simba kwa makini sana ni kwa sababu anajua simba kamzidi binadamu ujanja kwahiyo ujitahidi asikudhuru
Na Mungu aliliona hilo mapema sana na ndiyo maana akawaruhusu wanaume mtutawale wanawake halafu akatuambia sisi tuwatii alijua kuwa akimuachia mwanamke hii dunia aitawale basi wanaume mngekoma mara kumi zaidi ya sisi tunavyokoma kwenye huu mfumo dume hata ninyi wenyewe si mnaona kwenye huu mfumo dume tu bado wanaume mnakoma sasa fikiria dunia ingekuwa iko kwenye mfumo jike je? Najua na hapa utabisha ila sitashangaa maana wanaume hamkubaligi kushindwa mbele ya wanawake yaani hamtakagi kukubali kwamba kuna vitu wanawake tumewazidi wanaume hata Mungu anajua hilo ila ninyi mnadhani mmetuzidi kwa kila kitu