Nimepoteza fedha kwenye account yangu ya CRDB

Nimepoteza fedha kwenye account yangu ya CRDB

Crdb ni janga hadi naishangaa hii bank ...huduma zao mbofu pili usiombe mkopo kabisa yaan mkopo kwa mfanyakazi inachukua mwaka bora hata saccos
 
Crdb kuna wizi..Mimi pia pesa wangu tsh laki mbili hivi majuzi hyo hivyo wamenipiga..nakomaa nao kesho mpaka warudishe... Majibu wanayotoa ni ovyo na mepesi..ntawapeleka mahakamani wasiporudisha.
 
Kiresua,

Pole sana.
Nina rafiki ambaye alipoteza milioni nne na ilionekana ametoa laki nane nane Mumbai, India wakati huo yeye alikuwa hapa Tanzania. Hii ilikuwa takribani miezi miwili iliyopita.

Alifika benki, na kuandika maelezo pamoja na kutoa uthibitisho wa alipokuwa pamoja na ATM cards zake. Na kutaka kurudishwa kwa fedha. Pia akaunti yake ya zamani ya CRDB(iliyoibiwa fedha) ilifungwa na akafunguliwa akaunti mpya na pia taarifa kuthibitishwa na CRDB. Ninadhani fedha zaje zilirudishwa.
 
Last edited by a moderator:
Mi kuna mtu namfahamu alipoteza Milioni moja, karudishiwa laki tu, hizo zingine bado
 
Mi kuna mtu namfahamu alipoteza Milioni moja, karudishiwa laki tu, hizo zingine bado

Mabank yetu hayana wataalam wazuri wa kuzuia wizi wa mtandao. Watoto wa computer science wanaiba kirahisi sana. Tujiandae kuwakaba benki zetu tunapogundua maana wengi wetu hatujui tu
naibiwa.
 
Mbona mimi nilipoteza hela nikiwa nje ya nchi na wakanirudishia baada ya kuandika barua na kuuwasha moto? Waambie hayo majibu mepesi wakuandikie barua manake hujaelewa. Uende kwa branch na wakikuzingua uwaambie unataka kumuona meneja.

Ndiyo maana nilikuwa sikupati kwenye simu, kumbe ulikuwa overseas!
 
Jumamosi narudi, nilikuwa nataka waniambie kwa maandishi hizo assumtion zao maana huwezi kutoa majibu ya assumption kwa vit vinavyotaka facts (this is money business)

Halafu nitajua hatua stahiki za kuchukua..... nitaleta vita aisee wanipe ushahidi kuwa nilitoa mm! (a strange thing ni kuwa hakuna ATM charges kwenye hizi transactions) of which sio kitu cha kawaida, pia kama ni visa za atm za benki nyingine huwa inaandika VISACASH80....4NBC LTD/*location ya ATM. hapa hakuna kitu kama hicho ni (VISA Ubungo 220......44) tuu!

tutaona mbele ya sabari

Nashukuruni sana kwa mawazo Yenu! walionitia moyo, walionipa njia nawashukuru sana!
 
Iliwahi kunikuta hii....nimelala nyumbani napata alert kwenye simu kuwa...umetoa shs....kutoka atm blahh blahh...kama hauhusiki na muamala huu piga simu namba ......(landline, hivi landline baada ya saa moja usiku inapokelewa kweli?...iliita mpaka nilikaribia kuingia wazimu)....panic haijashuka inaingia alert nyingine....umetoa blah..blah....halafu walivizia wakati siku inapinduka ili kama limit ya siku imepita, nyingine itaangukia siku mpya....Nashukuru pesa yangu ilirudishwa na benki husika (sio CRDB) kwa wakati husika (reasonable).
 
Mi nadhani andika barua kiofisi, usikubali majibu ya dirishani omba majibu official ya maandishi, nakuhakikishia watarudisha pesa haraka sana wataogopa kukuzingua kwa maandishi, wakikuzingua kwa maandishi nenda na maandishi hayo kwa mwanasheria wako, atakushauri jinsi ya kufungua kesi na watakulipa vizuri tu, siyo laki nne tena, watakulipa na gharama zote za usumbufu, na mwanasheria watamlipa wao.
 
Nawamezea mate wananchi wa nchi zenye huduma bora za kibenki.
 
Kwanini Cases hizi nyingi zinahusu Local Banks kulinganisha na Banks nyingine?
Kuna KCB Bank ya jirani zetu hapo,mbona wao hawana cases nyingi za namna hii.Je ni kweli Watanzania wengi sio waaminifu anatoa data za wateja wao kwa Wataalam wa utapeli?

Ndio maana bado watu wanaweka pesa nyumbani kwa kuhofia hili,na wapo watu wengi wana accout banks karibia nne ili kuigawa pesa isije kutokea tatizo kubwa kama hayo.
 
Kama card yako ya ATM hukumpatia mtu siku hiyo, huenda ikawa ni tatizo la network(hizo debit and credit hafu ika debit tena) au ikawa ni ciber crime kuna bank zina EMV chip hizi ziko more secured so far najua EXIM ndo wanazo hizo cjajua other banks kama ni cover crime sijui utaratibu umekaaje pia watejaa tuwe makin unapokua kwenye ATM jaribu kuangalia ka hakuna vijicamera vimepachikwa coz majizi huwa wanategesha vijicamera
 
wandugu mnao poteza pesa zenu kwa njia ya cards au sim banking kuwen makini sana na hizi huduma, epuka sana kushare pin zako za atm au simu banking, pia mwatakiwa kujua kwa wale wanaotumia ATM CARDS ZA VISA, MASTERCARDS hapa tz hata kama una chip and pin card kua makini sana na kitu kinaitwa card skimming, lakini pia tambua hakuna kitu risk kama atm cards hasa visa au mastercards kwa kufanya online transactions, kuna baadhi ya websites za online payment haziitaji passwords kwa ajili ya ku-authorize transaction yoyote, hizi website zinahitaji only serial numbers za kadi mfano kuna namba 16 zz serial number huwa zipo kwenye uso wa kadi , na nyingine huwa zipo nyuma ya kadi , so kwenye online transactions unakuta ni only namba nne za mwanzo na namba nne za mwisho pamoja na zile namba za nyuma ya kadi, so ukisha ingiza namba hizo , basi mtu ANAweza fanya payment yoyote online kwa kutumia hizo number , kwahiyo hata mie leo nkiokota kadi yako au ukinipa kadi yako, nikifanikiwa kukopi namba nne za mwanzo na namba nne za mwisho, na za nyuma ya kadi, ninaweza fanya any online payment fraudulently na hakuna wa kunikama,

solution yake ni ipi?

nenda benk yako waambie wa-disable hiyo kadi ili serial numbers zisiweze fanya chochote kweenye akaunt yako, report issue yako makao makuu (hasa risk department) branch kuna longo longo nyingi, pia pin nimuhimu sana kuzuhifadhi kwa siri
 
Kama card yako ya ATM hukumpatia mtu siku hiyo, huenda ikawa ni tatizo la network(hizo debit and credit hafu ika debit tena) au ikawa ni ciber crime kuna bank zina EMV chip hizi ziko more secured so far najua EXIM ndo wanazo hizo cjajua other banks kama ni cover crime sijui utaratibu umekaaje pia watejaa tuwe makin unapokua kwenye ATM jaribu kuangalia ka hakuna vijicamera vimepachikwa coz majizi huwa wanategesha vijicamera

benk zote tz zilizopo kwenye NETWORK YA VISA AU MASTER CARDS kwa hapa tz zina chi and pin cards, ilikua imebakia nbc pekee nao wameanza badirsha kadi sasa nao wanatoa chip and pin cards. zipo safe hizi kadi ila not for online transactions
 
Iliwahi kunikuta hii....nimelala nyumbani napata alert kwenye simu kuwa...umetoa shs....kutoka atm blahh blahh...kama hauhusiki na muamala huu piga simu namba ......(landline, hivi landline baada ya saa moja usiku inapokelewa kweli?...iliita mpaka nilikaribia kuingia wazimu)....panic haijashuka inaingia alert nyingine....umetoa blah..blah....halafu walivizia wakati siku inapinduka ili kama limit ya siku imepita, nyingine itaangukia siku mpya....Nashukuru pesa yangu ilirudishwa na benki husika (sio CRDB) kwa wakati husika (reasonable).

nadhan ilikua nbc
 
Kwanini Cases hizi nyingi zinahusu Local Banks kulinganisha na Banks nyingine?
Kuna KCB Bank ya jirani zetu hapo,mbona wao hawana cases nyingi za namna hii.Je ni kweli Watanzania wengi sio waaminifu anatoa data za wateja wao kwa Wataalam wa utapeli?

Ndio maana bado watu wanaweka pesa nyumbani kwa kuhofia hili,na wapo watu wengi wana accout banks karibia nne ili kuigawa pesa isije kutokea tatizo kubwa kama hayo.

ndugu nipo kwenye banking kwa muda sasa, na moja kat ya shughuli nifanyazo ni fraud investigation, case kama hizi zipo benk takriban nying hapa tz na duniani kwa ujumla sema kwa vile hapa kwetu twaona ni mambo mapya, ila frauds in banks ni serious problem.....hasa kwenye ulimwengu wa sayansi na technologia. fraudsters wanatumia sayansi ya hali ya juu sana kufanikisha dhamira zao, so nijukumu la benk kuwa n robust systems zinazoweza punguza uwezakano wa majanga kama haya
 
Back
Top Bottom