Nimepigwa mzinga wa maana leo

Nimepigwa mzinga wa maana leo

fablo can

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2016
Posts
1,222
Reaction score
1,267
Hello wana wanabody habari za jioni

Niende moja kwa moja kwenye mada.
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu. Leo nilikuwa n.a. safari kwenda shule fulani maeneo ya mtoni mtongani (kwaazizially) kwa lengo la kuchukua order ya vifaa vya stationeries....!! Mimi ni supplier wa vifaa ivyo.
Wakati natoka hapo shuleni nikasema let me go to posta now. Nilipotaka kuvuka upande wa pili, ili nikapate usafiri kuelekea posta nikawaona wadada 2 warembo kweli kweli...nisiwe mnafiki hapa kwa kweli walikuwa wazuri siyo reception wala Tigo. Hakika waliumbwa wakaumbika.

Nikasema ngoja nivute faster niwasalimu kidogo. Nilipo wakaribia kumbe na wao walikuwa wananifanyia tyming. Na maongezi yetu yakawa ivi....!!!

Mimi: Mambo zenu watoto wazuri.....?
Wao: Nzuri
Moja kati yao akaniambia.....!!
Yeye: Kaka samahani. Naomba utusaidie elfu mbili ya nauli.
mimi: Nikamuuliza, mnaenda wapi?
Yeye: Tunaenda Kigamboni.
Mimi: mnatoka wapi....?
Yeye: Kwa Dada, anaishi Mtoni mtongani.
Mimi: Sawa. Though nikawa nawaza n.a. kutafakari iweje hawa wadada wazuri ivi wakose nauli tena elfu 1 na si elfu 2. Au ndiyo januari imekaza na kuvaa bukta nyeusi nini...? Manake from mtoni adi kigamboni ni elfu 1 kwa wawili. Baada ya kutafakari kwa kina nikatoa elfu 2. Nikawapatia kiroho safi tena bila kinyongo. Tukaagana n.a. kila mmoja akawa busy kusubiri usafiri wake.

Muda mfupi nikawaona wanashuka kituo kinachofata pembeni nikamuona yule Dada mwingine aliyekuwa nyuma pindi namwoji mwenzake...amemfesi kaka mmoja anamuomba nauli kwenda posta.
Nikashangaa n.a. kupigwa n.a. butwaa nikajisemea kimoyo moyo tayari nimeisha pigwa MZINGA tena asubuhi asubuhi...!!!.kwa kweli nilitamani kuwakimbiza wale wadada lakini nikasita na kujishauri wasije wakanigeukia hapa nikapata aibu ya mwaka. Kwani mjini mpango. Ingawa roho inaniuma.
Hivyo ndivyo nilivyopigwa mzinga siku ya Leo.
Ahsanteni naomba kuwasilisha
 
Wa maana “BUKU MBILI!!!” Watu bwana
 
Kweli akipendacho binti mwanaume lazima utanunua! Angekuwa mwanaume mwenzio kakuomba hela ya kula hakika angeondoka na matusi ya kutosha.
 
Ewe mwali kamlongele mwali mwanamwali mwali
 
Hello wana wanabody habari za jioni

Niende moja kwa moja kwenye mada.
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu. Leo nilikuwa n.a. safari kwenda shule fulani maeneo ya mtoni mtongani (kwaazizially) kwa lengo la kuchukua order ya vifaa vya stationeries....!! Mimi ni supplier wa vifaa ivyo.
Wakati natoka hapo shuleni nikasema let me go to posta now. Nilipotaka kuvuka upande wa pili, ili nikapate usafiri kuelekea posta nikawaona wadada 2 warembo kweli kweli...nisiwe mnafiki hapa kwa kweli walikuwa wazuri siyo reception wala Tigo. Hakika waliumbwa wakaumbika.

Nikasema ngoja nivute faster niwasalimu kidogo. Nilipo wakaribia kumbe na wao walikuwa wananifanyia tyming. Na maongezi yetu yakawa ivi....!!!

Mimi: Mambo zenu watoto wazuri.....?
Wao: Nzuri
Moja kati yao akaniambia.....!!
Yeye: Kaka samahani. Naomba utusaidie elfu mbili ya nauli.
mimi: Nikamuuliza, mnaenda wapi?
Yeye: Tunaenda Kigamboni.
Mimi: mnatoka wapi....?
Yeye: Kwa Dada, anaishi Mtoni mtongani.
Mimi: Sawa. Though nikawa nawaza n.a. kutafakari iweje hawa wadada wazuri ivi wakose nauli tena elfu 1 na si elfu 2. Au ndiyo januari imekaza na kuvaa bukta nyeusi nini...? Manake from mtoni adi kigamboni ni elfu 1 kwa wawili. Baada ya kutafakari kwa kina nikatoa elfu 2. Nikawapatia kiroho safi tena bila kinyongo. Tukaagana n.a. kila mmoja akawa busy kusubiri usafiri wake.

Muda mfupi nikawaona wanashuka kituo kinachofata pembeni nikamuona yule Dada mwingine aliyekuwa nyuma pindi namwoji mwenzake...amemfesi kaka mmoja anamuomba nauli kwenda posta.
Nikashangaa n.a. kupigwa n.a. butwaa nikajisemea kimoyo moyo tayari nimeisha pigwa MZINGA tena asubuhi asubuhi...!!!.kwa kweli nilitamani kuwakimbiza wale wadada lakini nikasita na kujishauri wasije wakanigeukia hapa nikapata aibu ya mwaka. Kwani mjini mpango. Ingawa roho inaniuma.
Hivyo ndivyo nilivyopigwa mzinga siku ya Leo.
Ahsanteni naomba kuwasilisha
Ulivyo boya yaan hata namba ya simu hukuchukua
 
Ulivyo tia mbwembwe sasa eti mzinga wa maana.... Mzinga wenyewe buku 2
 
Hii Michezo ni tokea enzi na enzi.

Mitaa ya KIJITONYAMA maeneo ya Shule ya MAPAMBANO ukivuka upande wa pili kuja Mitaa ya CCM (KIJITONYAMA) kulikuwa na MAMA Mmoja yeye alikuwa anapiga Virungu kwa njia ya kupungukiwa NAULI.

Kile ndio kilikuwa kipande chake kila siku, halafu alikuwa anajiweka Kiheshima na Msafi.

Yaani wala huwezi kujua kama ni mpiga VIRUNGU, wewe utadhani huyu MAMA kapungukiwa kweli na Nauli
 
UNGEwaitia taxi tu iwapeleke wanapotaka na kumpa pesa dereva
 
UNGEwaitia taxi tu iwapeleke wanapotaka na kumpa pesa dereva
Angekuwa kapigwa tu na.pia angekuwa kasababisha wengine huko kigamboni kupigwa, mzinga na hata dereva tax naye angeweza kupigwa mzinga kama angepewa ka darasi hiyo.
Hivyo kupelekea wote 3 kupigwa mzinga na.kikosi vha wabebez 2.
 
Back
Top Bottom