Elections 2010 Nimepiga kura, wewe je?

Nimetoka sasa hivi kupiga kura.
Kura ni siri lakini mimi nimepigia kura wagombea wa vyama vyote vitatu vikuu CHADEMA,CUF NA CCM,mpangilio nilivyotaja haufuati utaratibu wowote.
Pale kituoni watu wengi wa kata yetu nawafahamu kwamba ni CCM.Nikichanganya na mwenendo wa kampeni maeneo mengine nchini na kwenye vyombo vya habari na kwenye mitandao,dalili zote zinaonesha Jakaya Kikwete ndiye raisi anayemalizia awamu ya nne ya uongozi wa juu Tanzania.

Sasa natayarisha barua ya wazi kwa raisi huyu kutoka CCM.Nimeshaweka mezani vifaa vyote vya kuandikia isipokuwa maneno sijayapanga katika paragrafu zake.Kila nikijaribu nakuta sina maneno mengi na barua itakuwa fupi mno,haitopendeza.
Nawaomba wana JF tusaidiane vitu vya kujaza hii barua kwa Kikwete ili akiingia ikulu tu aikute barua yetu inamsubiri mezani kwake.

Rais JK usinichekeshe mie na mzazi wangu (ambaye ni kada wa zamani wa CCM), mke wangu na wadogo zangu na watu wanne mtaani kwetu tushaajiri rais mpya wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Sie ndio waajiri wakuu bwana JK na wewe subirini matokeo naenda kulala narudi baadae kwenda kulinda kura yangu pale kituoni hakuna kulala hapa leo.
 
Paragrafu yangu ya mwanzo nilitaka nimwambie kikwete
ACHANA NA MAFISADI
Ndugu raisi mafisadi nusura wakukoseshe kura katika kampeni za uraisi.Kwa hivyo............
 
Huyo Ami si alikuwa CUF amehamia lini CCM?????

Mimi ndugu yangu wala sijawahi kuwa na chama.Nimepiga kura kwa kufuata ushauri wa askofu Kakobe,Gamanywa na Sheikh Mkuu.Sikuchagua chama bali nimechagua wagombea kulingana na sera na kampeni zao.Ndio maana vyama vyote vitatu vimepata kura yangu.
 
Mama yangu Mzazi amekwenda kumpa kura yake Rais wetu mtarajiwa Dr. W Slaa. Kwa miaka yote amekuwa anaipigia CCM ila mwaka huu anasema mtazamo wake kwa kiti cha Uraisi umebadirika. Lakini anampigia CCM-kiti cha ubunge kwani bado anaimani na muwakirishi mpya katika nafasi hiyo hali kadhalika katika kiti cha udiwani. Namuunga mkono kwa uchambuzi wake na uhamuzi wake wa busara. Sisi tulio nje ya nchi tunafurahia kuona progress na muamko wa namna hii. N.B familia ya watu kumi wote wanampigia Dr. Slaa..MUNGU IBARIKI TANZANIA!!
 
Mungu amenisaidia nimekuwa mtu wa kwanza kituoni kwangu kupiga kura. Nilifika saa 11 na dakika 33 (05h33) na kituo kilifunguliwa saa 12 na robo (06h15) na nilipiga kura yangu saa moja na dakika nne asubuhi hii (07h04).

Pia nemefurahi kutimiza /kufikisha messages 1000 leo hii.

Utaratibu ni mzuri lakini inaelekea hata wasimamizi wa vituo mambo mengine hawayaelewi. Kwa kuwa nilikuwa wa kwanza kufika ilibidi niwasaidie watu wengine kutambua sehemu yao ya kupiga kura.

FFU wamejaa kwenye vituo na magari ya jeshi (JWTZ) ndio yanayosaidia usafari wa viti (nimeona kwa macho yangu) na vitu vingine.

Tatizo ni kwamba kura yangu sio siri (kunja kiganja na nyoosha vidole viwili huku vingine ukibaki umevikunja)

Mungu Ibariki Tanzania


Na mimi nimepiga kura na tayari nimesha mfukuzisha kazi jamaa wa MIPASHO na mama wa PATACHIMBIKA hapa Gonja SAME MASHARIKI. Inatia raha sana kwani vijana wamejitokeza kwa wingi ile mbaya kuanzia maeneo ya Ndungu, Gonja Mpirani, Gonja Maore. Vijana wameamua kumkoma nyani. Mipasho, patachimbika wote chaliiiiii, Napata msosi kidogo halafu twaoenda zetu kulinda kura zetu. Usiku wa leo, lazima mama apelekwe Mirembe. PEOPLEEEEE'S POWERRRRRRRRRRRRRRRRRRRR............!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom