PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,725
Paka Jimmy umepiga kura?
Broda mi(na familia yangu) sifanyi makosa...Tushamfuta kazi mtu tayari!
Paka Jimmy umepiga kura?
Nimetoka sasa hivi kupiga kura.
Kura ni siri lakini mimi nimepigia kura wagombea wa vyama vyote vitatu vikuu CHADEMA,CUF NA CCM,mpangilio nilivyotaja haufuati utaratibu wowote.
Pale kituoni watu wengi wa kata yetu nawafahamu kwamba ni CCM.Nikichanganya na mwenendo wa kampeni maeneo mengine nchini na kwenye vyombo vya habari na kwenye mitandao,dalili zote zinaonesha Jakaya Kikwete ndiye raisi anayemalizia awamu ya nne ya uongozi wa juu Tanzania.
Sasa natayarisha barua ya wazi kwa raisi huyu kutoka CCM.Nimeshaweka mezani vifaa vyote vya kuandikia isipokuwa maneno sijayapanga katika paragrafu zake.Kila nikijaribu nakuta sina maneno mengi na barua itakuwa fupi mno,haitopendeza.
Nawaomba wana JF tusaidiane vitu vya kujaza hii barua kwa Kikwete ili akiingia ikulu tu aikute barua yetu inamsubiri mezani kwake.
Huyo Ami si alikuwa CUF amehamia lini CCM?????
Mungu amenisaidia nimekuwa mtu wa kwanza kituoni kwangu kupiga kura. Nilifika saa 11 na dakika 33 (05h33) na kituo kilifunguliwa saa 12 na robo (06h15) na nilipiga kura yangu saa moja na dakika nne asubuhi hii (07h04).
Pia nemefurahi kutimiza /kufikisha messages 1000 leo hii.
Utaratibu ni mzuri lakini inaelekea hata wasimamizi wa vituo mambo mengine hawayaelewi. Kwa kuwa nilikuwa wa kwanza kufika ilibidi niwasaidie watu wengine kutambua sehemu yao ya kupiga kura.
FFU wamejaa kwenye vituo na magari ya jeshi (JWTZ) ndio yanayosaidia usafari wa viti (nimeona kwa macho yangu) na vitu vingine.
Tatizo ni kwamba kura yangu sio siri (kunja kiganja na nyoosha vidole viwili huku vingine ukibaki umevikunja)
Mungu Ibariki Tanzania