Nimependa msimamo wa Dr Slaa

Nimependa msimamo wa Dr Slaa

Kuna kundi limeibuka ghafla wakijifanya kuwa na uchungu sana na CHADEMA kumbe ni wanafiki, moyoni wako CCM. Wakati Magufuli anatangazwa kundi hilo hilo liliibuka na kuwashauri CHADEMA wakomae na ubunge. Ujio wa Lowassa umeonyesha rangi za baadhi ya watu. Sasa ni kama wamechanganyikiwa na kujifanya washauri wa CHADEMA.

Mimi nilikuwa mmoja wa watu niliyempinga Lowassa na kumuita mwizi wakati wa mchakato wa kura za maoni CCM ili asipitishwe sababu kubwa niliona upepo wake ulikumba hata wasiokuwemo. Nilijua wakimpitisha tu wapenda mageuzi tumekwisha kwani upepo wake ungepiga hadi kwenye majimbo ya upinzani, na badala ya kuongezeka yangepungua. Kuna wabunge wengi wa CCM walitegemea sana upepo wa Lowassa uwapitie. Sasa hivi wamechanganyikiwa wanaomba bora wangejitoa CCM mapema kabla kura za maoni CHADEMA hazijafanyika.

Ndugu zangu upepo wa wanasiasa ni mbaya sana kuna wabunge CHADEMA upepo wa Dr.Slaa uliwapitia hadi leo hawaamini kama wapo mjengoni. Lowassa upepo wake ni mbaya sana. Dr.Slaa angemsumbua Dr.Magufuli lakini asingemshinda. Vile vile kwenye UKAWA ujio wa Lowassa umeleta mshikamano zaidi. Ninaamini kuna wana CUF na NCCR wasingeweza kumpigia kura Dr.Slaa zaidi ya wabunge wao. Lakini Lowassa ni kama amekuja kuwaunganisha UKAWA. Zitabebwa kura nyingi sana hapa.

Hawo wasiomtaka Lowassa ni wale waliotaka wapinzani wawe wapinzani milele. Ndio wale utawaskia Urais CCM, Ubunge upinzani. Huo ni unafiki mkubwa. Tunahitaji CCM itoke kabisa. Sasa ujio wa Lowassa ni kama umewachanganya sana wamebaki kujifanya wanakishauri chama kumbe wanafki wakubwa. Lengo kuu la chama ni kushika dola kama kuna upenyo umetokea wa kukupeleka huko utumie ipasavyo. Muda ndio huu ukipita CCM itatawala milele.
Unajua kinachoshangaza watu ni kwamba, Je cdm wote hawakua bora kupata mgombea kwenye maisha yao yote ya kisiasa mpaka mtu alietoka upande wa wa pili aje awatetee kwenye nafasi hiyo?
 
Unajua kinachoshangaza watu ni kwamba, Je cdm wote hawakua bora kupata mgombea kwenye maisha yao yote ya kisiasa mpaka mtu alietoka upande wa wa pili aje awatetee kwenye nafasi hiyo?


Suala sio kupata mtu wa kuwatetea. Mbona 2005 na 2010 waliweka wagombea wakawatetea. Mwaka 2010 alipogombea Dr.Slaa unajua kilichotokea? Sasa hivi kinachotakiwa ni kutafuta ushindi utakaoondoa mfumo mzima wa CCM, na sio kubadilisha tu watu chini ya mfumo ule ule. Mimi ninaona Edward Lowassa ni mhimu zaidi kwa sasa. Lengo ni kushiriki uchaguzi mkuu kwa ajili ya kushinda, sio kusindikiza. Kwenye siasa fursa yoyote ikipatikana ni kuitumia vizuri. Sio suala la kujiuliza kuwa una mtu au huna. Unaweza ukawa naye lkn swali ni je atashinda ktk mazingira magumu haya ya CCM? Lkn kumchukua mtu anayeijua vizuri CCM ni silaha nzuri zaidi
 
Rweye
Sasa hivi mnatumia nguvu nyingi sana kuwaaminisha watanzania eti Lowassa ni msafi lakini kamwe na hamtaeleweka, itawasumbua sana hii na mtapata shida kubwa sana

WanaJF Wakuu, hivi waliozunguka nchi nzima na kutangaza kwamba EL, RA na Chenge ni mafisadi kwa hiyo wavue magamba la sivyo Chama chao kitawachukulia hatua walikuwa ni viongozi wa CDM? Mbona hawa CCM hawaeleweki? Magamba hawakuvua, na CCM waliwaacha tu kwa maana walikuwa wasafi wasio na magamba na mmojawao, Chenge, alipewa hata Uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge. Sasa wanataka CDM iwasafishe kivipi? Kwani ni lini walithibitishwa na Magamba kwamba ni wachafu? Akina EL, RA na Chenge ni wasafi sana hawana magamba kabisa CCM wenyewe wanakiri hivyo! CDM hawahitaji kuwasafisha chochote! CDM nyamazeni tu, hawa Ma-CCM wasiwachanganyie rangi!
 
safi silaa kausha hivyo hivyo watuzungumzie na sisi maana wamewazungumzia sana ccm kipindi cha kutia nia. upepo wa siasa now ni ukawa
 
jamni Dr. yupo likizo ya wiki moja, na hilo limesemwwa na mwenyekiti wa chama taifa kupitia Radio One kama haukusikia elewa hivyo. by then kwa nini leo wanaccm wa Lumumba ndo mnaobwabwaja sana? waambieni akina Nape wawaongeze mishahara badala ya buku 7 iwe hata 12 maana mnajitahaidi sana kusema uongo kuhusu Dr. na CHADEMA kana kwamba ninyi ndo wasemaji.
 
Hongera Mh. Lowasa Rais wetu. Hawa wote watoa mada pingamizi ni mamluki. Tusonge mbele na safari ya matumaini. Tunataka mageuzi nchi hii. Tumechoka
 
Ni vizuri mtoa mada ukajua nini lengo la UKAWA na wananchi kwa ujumla. Sisi wenye uchungu wa ukweli na nchi hii ya neema nyingi tunakushauri ujue kuwa swala siyo mtu bali ni kuweza kufanya mageuzi yenye tija kwa faida ya kila mwananchi. Lowasa anakubalika na dunia nzima. Tumpe nafasi atupe mwanzo mzuri.
 
Uko sahihi mkuu, huu ndio mpango mzima kuufikia ushindi, tunataka mabadiliko toka mfumo dola.

Suala sio kupata mtu wa kuwatetea. Mbona 2005 na 2010 waliweka wagombea wakawatetea. Mwaka 2010 alipogombea Dr.Slaa unajua kilichotokea? Sasa hivi kinachotakiwa ni kutafuta ushindi utakaoondoa mfumo mzima wa CCM, na sio kubadilisha tu watu chini ya mfumo ule ule. Mimi ninaona Edward Lowassa ni mhimu zaidi kwa sasa. Lengo ni kushiriki uchaguzi mkuu kwa ajili ya kushinda, sio kusindikiza. Kwenye siasa fursa yoyote ikipatikana ni kuitumia vizuri. Sio suala la kujiuliza kuwa una mtu au huna. Unaweza ukawa naye lkn swali ni je atashinda ktk mazingira magumu haya ya CCM? Lkn kumchukua mtu anayeijua vizuri CCM ni silaha nzuri zaidi
 
Ni vizuri mtoa mada ukajua nini lengo la UKAWA na wananchi kwa ujumla. Sisi wenye uchungu wa ukweli na nchi hii ya neema nyingi tunakushauri ujue kuwa swala siyo mtu bali ni kuweza kufanya mageuzi yenye tija kwa faida ya kila mwananchi. Lowasa anakubalika na dunia nzima. Tumpe nafasi atupe mwanzo mzuri.

Nimekupata,tena cdm hawana cha kujibu,lakini magamba mala esklo,epa, ligoda,gesi....je?Lowasa si ni ka richadi tu nako kakatolea majibu!
 
Kama kuna kosa CHADEMA watalijutia ni kumfanya Lowassa mgombea wao wa urais. Maadili tuliyosimamia tumeyatupa chooni na kuwakatisha tamaa wanachama na wadau wengi mimi nikiwemo.

Chama sasa hakina tofauti na CCM kwa uchafu na sasa imedhihirika kuwa ni Dr Slaa tu ndiye aliyeamini katika uadilifu ndani ya chama.

Viongozi wengine kumbe wako kimslahi zaidi na hawakumbuki wahanga waliouawa na kuumizwa na polisi kwa kuunga mkono CHADEMA wakiamini ni mkombozi wao. Sasa kimepokea wale mafisadi papa ambao hata chama chao hakiwataki! Tumekata tamaa.

Pole Dr Slaa lakini Mungu yuko na atatunusuru.

Sisi wana ukawa tunaassume dr kafa tumeshamzika?kwan mtu akifa chama kitakufa? Wacha aondoke ukawa mbele kwa mbele .
 
Unajua msimamo Wa Dr wewe Lumumba Leo ndio mnajifanya mnauchungu na chadema kuliko wana chadema na propaganda zenu za kuandikiwa na bado mtaweweseka sana na unafiki Wa viongozi wenu wanaoawatuma maana mmekuwa misukule hampunguzi ata nucta na mistari kwenye mada zenu mnapigiwa
 
Nafasi ya mgombea urais Chadema imeuzwa kwa mtu binafsi.

Wafuasi walioamini mabadiiko ya kweli wakumbuke kuwa tuliwaonya kuwa Chadema ni Chama cha kilaghai...

"...Eti tuliwaonya". Ninyi wakina nani, na kwa upendo gani? Kwanini msimwonye anayetaka kufunga gori la mkono? Mwambie atapewa kadi nyekundu.

Wakati wa mabadiliko hata jambazi atatangaza enjili, ndio si kabadilika? Swala la Lowasa kuingia upinzani ndo viashiria vya mabadiliko. Watu watulie waache MUNGU aikarabati nchi yake.
 
Leo asubuhi katika kipindi cha matukio kinachoendeshwa na Radio one stereo alisikika MH.. Tundu Lissu mwanasheria wa cha cha CHADEMA akisema kuwa Mhe. John Mnyika hajaonekana katika hadhara ya mapokezi ya E.LOWASA kwa sababu alikuwa mgonjwa. Akadai kuwa amemwambia ajitokeze hadhazani ili aoneshe msimamao wake. Tunasubiri kutoka kwa Mnyika.je bado ni mwana CHADEMA HALISI AU AMEPOTEZA......
Kwa upande wa MH.DR.SLAA alisema kuwa yeye mwenyewe Lissu ametumia takilibani masaa 6 akiwa NYUMBANI KWA Katibu huyo akijaribu kumshawishi akubali kurudi na kujenga chama. NIKIMNUKUU TUNDU LISSU alisikika akisema kuwa nilikuwa nyumbani kwa DR Slaa nikimwomba arejeshe moyo aje tujenge chama............. mwisho wa kunukuu........................... lakini akakanusha kuwa hachaachia ngazi ya UKATIBU MKUU.

Swali je DR SLAA akubali kutoka wapi kama bado ni katibu? je alikuwa mtu wa kufuatwa nyumbani na Tundu lisu eti wakajenge Chama? kwani yeye kama kiongozi hajui wajibu wake hasa katika kipindi ambacho chama kimepata Mgombea asiye na mpinzani ndani ya chama.......? Ama kwa maneno ya Lissu inadhihirisha wazi kuwa chama kimeyumba tena bila kificho?
CCM inaweza kuwa ilikuwa sahihi kumwacha huyu BWANA MKUBWA WA CHADEMA KWA SASA! Lakini kwa utafiti wa kisayansi ulioipa nguvu chadema inawezekana haukuzingatia maadili na miiko ya chama hiki.
CCM katika mchakato wake wa DODOMA demokrasia ilibakwa!!!!111111111111111
Huku mchakato wa huyu mgombea huyuhuyu ukiwa haujabakwa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!111111111111111111
MY TAKE......................
DR SLAA JE AMEJIUZURU KWA KUKIMBIA KIVULI CHAKE MWENYEWE? AU BADO ANASIKILIZIA MAWAZO YA FAMILIA KAMA MTOA MAKALA ALIVYOSEMA HAPO JUU?
 
Kama kuna kosa CHADEMA watalijutia ni kumfanya Lowassa mgombea wao wa urais. Maadili tuliyosimamia tumeyatupa chooni na kuwakatisha tamaa wanachama na wadau wengi mimi nikiwemo.

Chama sasa hakina tofauti na CCM kwa uchafu na sasa imedhihirika kuwa ni Dr Slaa tu ndiye aliyeamini katika uadilifu ndani ya chama.

Viongozi wengine kumbe wako kimslahi zaidi na hawakumbuki wahanga waliouawa na kuumizwa na polisi kwa kuunga mkono CHADEMA wakiamini ni mkombozi wao. Sasa kimepokea wale mafisadi papa ambao hata chama chao hakiwataki! Tumekata tamaa.

Pole Dr Slaa lakini Mungu yuko na atatunusuru.

Wenzio wanachanua ww unadumaa then unajipongeza
 
Hakuna unafiki zaidi ya huu wa kumuuzia ENL urais, mchango wa Dr Slaa kwa cdm ni zaidi ya unavojua, ni zaidi ya pesa za kiingilio ambazo inasadikika wamegawana shareholders wa hii kampuni CDM. Kundi la ENL ni kubwa sana lina nguvu nyingi sana kiasi cha kuelekea kumuelemea mwenyewe, kundi hili maslahi yake na ideology yake ni tofauti na CDM, walah kundi hili litakipasua CDM. Namuombea apate urais ndo utakapojua nguvu ya mtandao wa ENL....usione wamevaa tishet ulipo tupo hao ni wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, wakurugenzi nk. simaanishi kukuaminisha chochote. ila uamzi waiofanya "shareholders" si kwa sustainable faida ya chama
 
Kazi iliyopo mbele ya cdm ni kumsafisha el,

Wakati huohuo team el inaendelea kuibaka cdm
 
Back
Top Bottom