Nimependa msimamo wa Dr Slaa

Nimependa msimamo wa Dr Slaa

mimi naona anapenda madaraka pia. Yeye kama anataka wapinzani wachukue nchi angetumia busara wawe yeye na edo kitu kimoja. Kwani hii chuki yake Slaa inabomoa upinzani. Naona Zitto anachelekea kwani ataenda Act Chama ambacho kichanga zaidi.

Sidhani kama Slaa ana tamaa na madaraka bali amehuzunishwa na jinsi CDM ilivyokiuka misingi yake ya kupinga ufisadi na mafisadi. Pili ni ile kauli ya Mtei alipomwambia kama hataki Edo aje basi mlango upo wazi yeye kutoka. Ni vema kumkatalia mtu kitu fulani kwa lugha yenye staha na sio kiukatili hivyo.
 
Kuna kundi limeibuka ghafla wakijifanya kuwa na uchungu sana na CHADEMA kumbe ni wanafiki, moyoni wako CCM. Wakati Magufuli anatangazwa kundi hilo hilo liliibuka na kuwashauri CHADEMA wakomae na ubunge. Ujio wa Lowassa umeonyesha rangi za baadhi ya watu. Sasa ni kama wamechanganyikiwa na kujifanya washauri wa CHADEMA.

Mimi nilikuwa mmoja wa watu niliyempinga Lowassa na kumuita mwizi wakati wa mchakato wa kura za maoni CCM ili asipitishwe sababu kubwa niliona upepo wake ulikumba hata wasiokuwemo. Nilijua wakimpitisha tu wapenda mageuzi tumekwisha kwani upepo wake ungepiga hadi kwenye majimbo ya upinzani, na badala ya kuongezeka yangepungua. Kuna wabunge wengi wa CCM walitegemea sana upepo wa Lowassa uwapitie. Sasa hivi wamechanganyikiwa wanaomba bora wangejitoa CCM mapema kabla kura za maoni CHADEMA hazijafanyika.

Ndugu zangu upepo wa wanasiasa ni mbaya sana kuna wabunge CHADEMA upepo wa Dr.Slaa uliwapitia hadi leo hawaamini kama wapo mjengoni. Lowassa upepo wake ni mbaya sana. Dr.Slaa angemsumbua Dr.Magufuli lakini asingemshinda. Vile vile kwenye UKAWA ujio wa Lowassa umeleta mshikamano zaidi. Ninaamini kuna wana CUF na NCCR wasingeweza kumpigia kura Dr.Slaa zaidi ya wabunge wao. Lakini Lowassa ni kama amekuja kuwaunganisha UKAWA. Zitabebwa kura nyingi sana hapa.

Hawo wasiomtaka Lowassa ni wale waliotaka wapinzani wawe wapinzani milele. Ndio wale utawaskia Urais CCM, Ubunge upinzani. Huo ni unafiki mkubwa. Tunahitaji CCM itoke kabisa. Sasa ujio wa Lowassa ni kama umewachanganya sana wamebaki kujifanya wanakishauri chama kumbe wanafki wakubwa. Lengo kuu la chama ni kushika dola kama kuna upenyo umetokea wa kukupeleka huko utumie ipasavyo. Muda ndio huu ukipita CCM itatawala milele.
Utakuwa upo vizuri sana Kichwani. Kwasababu kila point unatema ni madini. Mimi ninafikiri hivi hivi, kila mstari ulioandika. Kuna vikao vimekaliwa na ccm wamekuja na strategy hii, kuwagawa wapinzani. Kujifanya wanasympathy na Dr slaa. Ili ikiwezekana asuse, kutokee mpasuko mkubwa. Lakini wanasahau wakuu wa chadema kabla ya kumkaribisha vilikaa vikao vya muda mrefu, kupima faida na hasara ya kumkaribisha. Wasomi wakashindana kwa hoja, hoja ya mtaji wa lowassa ndani ya ukawa ikashinda. Inaonekana lowassa atumike kama tool ya kuing'oa ccm, kwasababu ana fedha, ana mtandao, ana watu. Na zaidi anajua mbinu za ccm zote kuliko mtu yoyote! Atumike. Dr slaa aliridhika, angekataa lowassa asingekuja. Hata kikao cha jumapili cha kumpokea lowassa walikaa nae Meza kuu. Watu hawajui kwenye siasa hakuna adui wa kudumu. Ungeamini siku moja lowassa na kikwete wangekuwa maadui kiasi hiki? Kwahiyo tutamtumia lowassa kuwamaliza ccm. Tupo nyuma ya lowassa
 
Slaa anasikitisha. Mwanamme wa kweli huwa anakuwa mgumu, hii mambo ya kununa nuna, kuzira zira, kulia lia kama Pinda aachie wanawake

yaan wengine mnaboa sana, yaan badala mzungumzie Lowassa anayeibaka cdm, mna mzungumzia Slaa aliyektaa kubakwa ndni ya cdm, ndio maana nasema humu wamejaa waliotoroka shule.
 
...leo hata manungayembe yanajifanya wanachama wa cdm. sisi waandamizi tunaimani na viongozi wetu na tunaimani na rais wetu lowasa, go go go lowasa go push it kitaeleweka tu....

Wewe ni mpumbavu, hata mwezi haujapita unaimba nyimbo za lowassa wakati hakuwepo kwenye ramani ya chadema, lakini nadhani pia utakuwa umetumwa. Utakufa masikini la ulofa wako. Nkt*
 
Msimamo uliopo sasa si wake bali ni wa mkewe,Hii ni aibu sana kwa familia za kiafrika.

Halafu ndio anataka kuwa Rais si atakuwa anaendesha nchi kutoka bedroom..bora kabainika mapema..aache siasa aone atakula nini? Siasa ndiyo kazi yake na chadema wamekuwa wanamlipa mshahara mkubwa sana..kama anaondoka aondoke tutamteua Lissu kuwa katibu mkuu
 
Dr slaa tunamhitaji sana ndani ya UKAWA lakini hatuwezi kutumia nguvu nyingi sana kumshawish mtu ambaye anajua faida Za UMOJA na MSHIKAMANO kwa manufaa ya Taifa.Ni upuuzi kususa eti kwasababu flani kakaribshwa ndani ya CHAMA na kuruhusiwa kugombea Urais.
 
Suala la kususa ni moja ya njia kuuonesha umma kuwa hukubaliani na jambo flaani, upinzani ukiwa bungeni ulionesha kutokubaliana nakuburuzwa na sisiem ktk mambo mbalimbali hadi kwenye ishu ya katiba nakupelekea kujitoa kwenye ukumbi tulio wengi tulipongeza hatua hiyo lkn leo amesusia Dr ktk masuala ya chama inaonekana ajabu sana ni haki yake msimuhukumu.
 
Unafikiri Lowassa angeenda cdm bila Regina kukubali? Unaongelea nini? For every successful man there is a strong woman behind. Women run this world my friend!

Na pia kinyume chake: For every unsuccessful man there is a weak woman behind.

If Dr Slaa is not careful, atapotezwa kisiasa na Mushumbusi!
 
Yeye na mkewe ni kitu kimoja. Josephine ni lazima aone uchungu kwani aliumizwa na polisi kwenye maandamano ya Arusha tarehe 5/1/2011. Na sasa chama alichopigania kimekosa mwelekeo na maadili. Niwaulize akina Mbowe kweli hizi nyimbo zetu za kuwatukana mafisadi mtazipiga kwenye kampeniza lowasa? Kitakuwa kichekesho!
 
Angekuwa amekaribishwa mtu safi tungefurahi sana lkn kakaribishwa aliyefukuzwa kwa ajili ya ufisadi!! Ccm inajisafisha chadema inajichafua!! Unafiki utatimaliza na wala tusiilaumu ccm.
 
Roho inauma, ikombozi kutoka kwa mafisadi unazidi kwenda mbali.!?!..
 
new tactics huwez kumpiga adui yako pasipo kushilikiana na mtu wake wa karibu tanganyika isingeweza kumpiga iddi amin kama waganda wasingekubali kumsaliti kama tunataka kuitoa ccm lazima ukubali kushilikiana nao sababu wao ndio wanajua mfumo mzima wa ushindi wa ccm
 
Mbweha nyinyi sina uwakika kama kweli Mungu atawasamehe kwani mlisababisha wapumbavu wenzenu wengi

wamwage damu wengine kuziacha familia zao uraina wao wakimalizia adhabu zao..
 
11705083_950504261674314_3464824027126095861_n.jpg
 
yaan wengine mnaboa sana, yaan badala mzungumzie Lowassa anayeibaka cdm, mna mzungumzia Slaa aliyektaa kubakwa ndni ya cdm, ndio maana nasema humu wamejaa waliotoroka shule.
Nitaka radhi dogo mimi ni sawa na baba yako, "shuaini"
 
Back
Top Bottom