Egwugu
JF-Expert Member
- Mar 16, 2011
- 17,558
- 8,552
Potelea mbali liwalo na liwe.
Ilmradi mko tayari basi twende na msije kuanza kupiga kelele wenyewe
Potelea mbali liwalo na liwe.
mimi naona anapenda madaraka pia. Yeye kama anataka wapinzani wachukue nchi angetumia busara wawe yeye na edo kitu kimoja. Kwani hii chuki yake Slaa inabomoa upinzani. Naona Zitto anachelekea kwani ataenda Act Chama ambacho kichanga zaidi.
Utakuwa upo vizuri sana Kichwani. Kwasababu kila point unatema ni madini. Mimi ninafikiri hivi hivi, kila mstari ulioandika. Kuna vikao vimekaliwa na ccm wamekuja na strategy hii, kuwagawa wapinzani. Kujifanya wanasympathy na Dr slaa. Ili ikiwezekana asuse, kutokee mpasuko mkubwa. Lakini wanasahau wakuu wa chadema kabla ya kumkaribisha vilikaa vikao vya muda mrefu, kupima faida na hasara ya kumkaribisha. Wasomi wakashindana kwa hoja, hoja ya mtaji wa lowassa ndani ya ukawa ikashinda. Inaonekana lowassa atumike kama tool ya kuing'oa ccm, kwasababu ana fedha, ana mtandao, ana watu. Na zaidi anajua mbinu za ccm zote kuliko mtu yoyote! Atumike. Dr slaa aliridhika, angekataa lowassa asingekuja. Hata kikao cha jumapili cha kumpokea lowassa walikaa nae Meza kuu. Watu hawajui kwenye siasa hakuna adui wa kudumu. Ungeamini siku moja lowassa na kikwete wangekuwa maadui kiasi hiki? Kwahiyo tutamtumia lowassa kuwamaliza ccm. Tupo nyuma ya lowassaKuna kundi limeibuka ghafla wakijifanya kuwa na uchungu sana na CHADEMA kumbe ni wanafiki, moyoni wako CCM. Wakati Magufuli anatangazwa kundi hilo hilo liliibuka na kuwashauri CHADEMA wakomae na ubunge. Ujio wa Lowassa umeonyesha rangi za baadhi ya watu. Sasa ni kama wamechanganyikiwa na kujifanya washauri wa CHADEMA.
Mimi nilikuwa mmoja wa watu niliyempinga Lowassa na kumuita mwizi wakati wa mchakato wa kura za maoni CCM ili asipitishwe sababu kubwa niliona upepo wake ulikumba hata wasiokuwemo. Nilijua wakimpitisha tu wapenda mageuzi tumekwisha kwani upepo wake ungepiga hadi kwenye majimbo ya upinzani, na badala ya kuongezeka yangepungua. Kuna wabunge wengi wa CCM walitegemea sana upepo wa Lowassa uwapitie. Sasa hivi wamechanganyikiwa wanaomba bora wangejitoa CCM mapema kabla kura za maoni CHADEMA hazijafanyika.
Ndugu zangu upepo wa wanasiasa ni mbaya sana kuna wabunge CHADEMA upepo wa Dr.Slaa uliwapitia hadi leo hawaamini kama wapo mjengoni. Lowassa upepo wake ni mbaya sana. Dr.Slaa angemsumbua Dr.Magufuli lakini asingemshinda. Vile vile kwenye UKAWA ujio wa Lowassa umeleta mshikamano zaidi. Ninaamini kuna wana CUF na NCCR wasingeweza kumpigia kura Dr.Slaa zaidi ya wabunge wao. Lakini Lowassa ni kama amekuja kuwaunganisha UKAWA. Zitabebwa kura nyingi sana hapa.
Hawo wasiomtaka Lowassa ni wale waliotaka wapinzani wawe wapinzani milele. Ndio wale utawaskia Urais CCM, Ubunge upinzani. Huo ni unafiki mkubwa. Tunahitaji CCM itoke kabisa. Sasa ujio wa Lowassa ni kama umewachanganya sana wamebaki kujifanya wanakishauri chama kumbe wanafki wakubwa. Lengo kuu la chama ni kushika dola kama kuna upenyo umetokea wa kukupeleka huko utumie ipasavyo. Muda ndio huu ukipita CCM itatawala milele.
Slaa anasikitisha. Mwanamme wa kweli huwa anakuwa mgumu, hii mambo ya kununa nuna, kuzira zira, kulia lia kama Pinda aachie wanawake
...leo hata manungayembe yanajifanya wanachama wa cdm. sisi waandamizi tunaimani na viongozi wetu na tunaimani na rais wetu lowasa, go go go lowasa go push it kitaeleweka tu....
Msimamo uliopo sasa si wake bali ni wa mkewe,Hii ni aibu sana kwa familia za kiafrika.
Unafikiri Lowassa angeenda cdm bila Regina kukubali? Unaongelea nini? For every successful man there is a strong woman behind. Women run this world my friend!
Nitaka radhi dogo mimi ni sawa na baba yako, "shuaini"yaan wengine mnaboa sana, yaan badala mzungumzie Lowassa anayeibaka cdm, mna mzungumzia Slaa aliyektaa kubakwa ndni ya cdm, ndio maana nasema humu wamejaa waliotoroka shule.