Nimepata mgeni wa ajabu sana

Nimepata mgeni wa ajabu sana

hiyo ndo daslam ukifika tu mwenyeji anakuuliza unakaa hapa siku ngapi?.
 
Binafsi babu na bibi yangu mzaa Baba walikuwa wachoyo sana (babu keshafariki ila bibi bado yupo) sasa ukienda kwao japo Hamna cha maana utakacho kikuta, kwanza vyakula havina hata taste 😀sasa ukikaa zaidi ya wiki nyumbani kwao, yule babu anaenda kuchuma majani ya Tumbaku mbichi halafu anakuja kuyachoma kwenye jiko(hako kajumba unakolalia kenyewe ndio jiko, sebule, bafu na chumba)😀 aisee yaani ule moshi wa tumbaku mbichi unawasha koo ni kiama hicho!! Kesho yake lazima urudi kwenu!!!!! Sasa Mkuu (mleta Uzi) hebu usimfukuze kwa maneno, jaribu kufanya vitimbi, lete upupu mwagia shuka lake,pia chakula chake mwambie waifu wako atie chumvi na pilipili kama zote!! Ndani ya siku mbili tatu Nakuapia utamsahau huyo lazima atafute njia ya kwao😀😀😀
 
Na hilo nalo linahitaji ushauri? wanaume wa dar hivi tatizo nn lakini?
 
Hivi angekuwa kapasua ana div 1 kali afu ndo anapiga fegi na kanywa hayo mapombe yenu ungeleta uzi hapa. Ukoo wenu wote inaonekana ni wa walevi. Vumilia tu huyo ni ndugu yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kaka kwa hiyo umeamua kunifungulia uzi kabisa,halafu kuna heinken moja nilibakiza nimeamka sijaiona nimembana huyu demu wa kazi kasema umechukua wewe,sasa utanitambua ukiludi,mzee mwenyewe alikuwa ananiogopa sembuse wewe boya,
utapata tabu saana
 
NOT IN MY HOUSE!!
nitampasua nimtengeneze soup aseeh!!
Leo asubuhi angejikuta yupo kwenye Basi anarudi kwa babake!!

Boxer sebuleni?
Sigara?
Kutongoza msaidizi wangu?
Pombe kwa mtoto? (Tafsiri yangu ya mtoto ni yeyote aliye chini ya paa langu ni mtoto)
Billie viiiiipi bana?
 
Hapo kama unashindwa kumwambia live aache tabia zake basi chonga plan na Dada wa kazi mwambie atapomtongoza aseme anakuogopa ww kwa maana na wewe una maslahi kwake
Sasa kwa jinsi Huyo mgeni alivyo wa ajabu ataenda kumwambia mkeo kuwa unachepuka na Dada wa kazi then mnamtimua maana anakuwa kaja kugombanisha ndoa za watu
Kwann ukose mamlaka hivo na nyumba yako?
Natakiwa kupanga mbinu na mtu ili KUONDOA mtu anayemissbehave kiwango hicho?
SIFANYI HUO HIYO KITU ASEE!!
ni ataondoka the very moment!!
Babake atakamponiuliza nitamwambia amulize mtoto wake!!
PERIOD!!
 
hivi vitabia wanavyo sana watu wa dar. hapo ukute kaambiwa dogo aje atafte chuo huko kakubali sasa kaona maisha magumu ukute ana chumba na kijisebure sasa kama anakosa uhuru yaani mgeni afike siku moja anywe heinken box moja na st anna afu avute sigara sebureni hahaha huyu jamaa muongo sana
Watu wa Dar hatuna hizo mkuu.

Jaribu kuja kuishi kwangu.
 
Kwanza wewe ni msanii kama Yule wa GPA ya 32,unasema amepata four ya mwisho afu unadai inasemekana mitihani hakufanya,kama hakufanya mitihani hyo four ya mwisho kaipataje?Unaandika inasemekana baba yake alimlea kwa kumdekeza,mtoto wa ba mdogo wako usiwe na uhakika alilelewa vipi? Any way Kama kaja kutembea mvumilie tu ataondoka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwan kwako kuna vyumba vingapi??
Kama havitoshi mwambie arudi kwao umepata mgeni mpya
 
Kwan kwako kuna vyumba vingapi??
Kama havitoshi mwambie arudi kwao umepata mgeni mpya
 
Kuna kijana mtoto wa baba mkubwa kaja kunitembelea hapa nyumbani baada ya kumaliza form six wanasubilia selection za chuo ila huyu kafeli maana kapata four ya mwisho.Sasa nilichoudhika ni hili tukio nililolikuta home kwangu.Yaani nimekuta limekunywa Box zima la Heinken zangu na st.Anna za mke wangu ***** zake cha kushangaza sasa toto dogo nimekuta linakula sigara packet nzima tena sebuleni yaani hili toto lina siku moja limeanza kufanya hivi nimekuta sebuleni kumejaa moshi kama jamaika aisee.AISEE HILI TOTO NASIKIA BABA YAKE ALILEA KWA KULIDEKEZA NA KUNA TETESI HATA HUO MTIHANI WA FORM SIX HALIJAFANYA.WAKUBWA HEBU NISAIDIENI MBINU ZA KULITIMUA KWA SABABU NAHISI NIMETEMBELEWA NA PAMPULA NA SIO MGENI TENA.MBAYA ZAIDI HUYU DADA WA KAZI AISEE KANIHADITHIA VITIMBWI VILIVYOKUWA VINATENDWA NA HILI TOTO MPAKA MENGINE AIBU KUYAANDIKA.NIPENI MBINU WAKUU HAPA KWANGU ANA SIKU MBILI NATAKA NIMG'OE HAPA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Undugu mwisho CHALINZE fukuza huyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom