Hahah Poa Nareem. Just coincidence. Ndio maana nikasema mm na mke wangu hatukukutana JF. Tulikutana mtandao unaitwa The Grid ulikuwa unamilikiwa na voda enzi hizoooo. Sisi ilichukua miaka mitatu tangu kukutana kwa mara ya kwanza hadi kuoana. Tuna miaka mitatu ya ndoa lkn tuna miaka kama saba hivi tangu kukutana kwa mara ya kwanza.
Kwa ujumla lengo ni kuwashuhudia wenzetu kuwa mwenza waweza kutana naye popote pale maana kuna watu hawaamini kama waweza pata mke au mume kwa njia hii.
Nashuhudia uaminifu pia, mm tangu nikutane naye sijawahi kuwa na mahusiano yoyote na wala sitarajii. Naamini mke wangu ni muaminifu pia. So jf watu wema wapo na wabaya pia wapo. Mtandao ni ulimwengu mwingine kuna wezi, majambazi, wauaji, wapole, malaya nk. Be careful.