Bestitoz MMU.
Kwa Kasie wiki hii yaliyojiri ni upande wa ofcn, tangu jumatatu ya wiki hii ofisini kwetu nimejikuta nakuwa mdada peke yangu na wababa 2.
Wengine mmoja kasafiri kikazi, mwingine yuko likizo mwingine yuko training kwa wiki 2 na mwingine yupo ia anaripoti kazini asubuhi kisha anatoka na kuingia kazi za nje.
Sasa tangu jumatatu wababa hao wamekuwa wakiniambia, Kasinde sasa tumebaki sisi tuu, sasa inakuweje.
mara waniambie umependeza sana, mara miguu yako mizuri, mara sijui imekuaje.
Yaani hawa wababa siwaelewi hata kidogo, kabla ya wiki hii huwa maongezi ofisini yako ya kawaida tuu ya utani na si ile ya kivileee. Mara waanze kusema unajua maofisi wengine wakibaki wawili huwa wanafanyana/wanadinyana, sasa hapa tumebaki sisi tuu sasa tufunge mlango.
Hapa nimejikausha wanapiga story zao mie niko busy najidai nimeconcetrate kwenye computer ila naomba ijuaa ifike salama maana huwa sina tabia ya kutoroka kazini siwezi, ingekuwa hivyo ningeshatoroka na kwaachia ofisi.
Tangu jana wananiganda nawanunulia lunch ofcourse tunakula hapahapa ofisini yaani, sijui wamepata genye za ghafla au ni nini kimewakumba.
Naogopa uu wasijenibaka Kasie wa watu, sijui niwatukane? au nianze kuwaongelesha kiingereza.
Maana wanaume wengine wakishapandishaga genye akili inakuwa haifanyi kazi kabisa.
Niombeeni wapendwa wiki 2 ziishe salama.
Na ujanja wangu wote am worried.