SmAlL pDiDy. jr
JF-Expert Member
- Dec 27, 2014
- 392
- 133
Nakumbuka niliwahi kutoka na mdada mmoja hivi maeneo ya makumbusho....
Kwanza kabla hatujafika eneo la tukio nilimwambia live kuwa mfuko mfupi...kwa hiyo mbwembwe na mashauzi sitaki...akasema poa...
Mzee kufika pale maeneo mtoto wa kike kabla maongezi akaagiza heinken..nikasema leo kazi ipo..ikabidi mzee niagize pepsi bariiiiidi ili kuenda sawa na salio mfukoni...huku moyo unanienda mbio mara mtu wa jikoni huyo kaja utadhani kaitwa...anauliza oooh! niwahudumie nini...dah mtoto wa kike kike akaagiza kuku mzima na chipsi...duuh nikachoka kabisa....ikabidi mzee nivunge kuwa nimeshiba...wakati tunaendelea na maongezi kila saa simu yake iko bize kama custmer care.....huku kuku anamla kwa kumdonoa donoa kama mwewe....kabla hatujafikia muafaka ghafla naona simu yake inaita na yakafuatia maongezi kama ya dakika kumi hivi...mwisho wa maongezi ya simu nikaambiwa amepata dharula kwa hiyo anatakiwa aende...dahh!!...nikasemea kimoyo moyo ndio nishaliwa hivyo...ikabidi nimruhusu...
Roho iliniuma sana kumtazama kuku mzima alivyo donolewa ikabidi nichukue mfuko laini nimfunge nikalie ugali nyumbani...wanawake kweli majanga...
WeWe niShIdaaaaq. NimEcheKea Kingese!!