Nimemshangaa General Mirisho Sarakikya

Nimemshangaa General Mirisho Sarakikya

Upuuzi mtupu, mwanaume mzima uache shughuli zako uende ukachangie kwa maandishi ili upate sitting allowance!?

Shughuli zako muda wa kazi? Hivi mwajiliwa analazimika kwenda ofisini kila siku, kazi zote anazozifanya ofisini hawezi kuzifanya nyumbani.
Waswahili wanamsemo kwamba “ukikubali kuolewa, kubali kulala bila c*upi”
Kama haukuona umuhimu wa hizo shughuli zako ukaomba kazi nyingine, kunali masharti yake. Kama ana majukumu mengine nje ya ubunge anayohisi ni muhimu zaidi angeiga mfano wa Mo Dewj.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Shughuli zako muda wa kazi? Hivi mwajiliwa analazimika kwenda ofisini kila siku, kazi zote anazozifanya ofisini hawezi kuzifanya nyumbani.
Waswahili wanamsemo kwamba “ukikubali kuolewa, kubali kulala bila c*upi”
Kama haukuona umuhimu wa hizo shughuli zako ukaomba kazi nyingine, kunali masharti yake. Kama ana majukumu mengine nje ya ubunge anayohisi ni muhimu zaidi angeiga mfano wa Mo Dewj.


Sent from my iPhone using JamiiForums

Ndio hivyo sasa anaona aibu hata kuchangia katikati ya hilo kundi la wajinga.
 
Ndio maana huku udanganyikani mabadiliko yakweli yanachelewa sababu watu wa Vyombo vya Dola na wastaafu hawaamini katika hiyo
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo kulikuwa na kikao cha Washili wa kabila la Wameru.Washili ni viongozi wa kimila wa kabila la kimeru.Ni sawa na viongozi wa kabila la waMaasai Laigwanani.

Washili leo wamekutana kwaajili ya kuunga mkono uamuzi wa Spika wa kumvua ubunge Mh Nassari kwa kosa la kutohudhuria vikao vitatu vya bunge kwa mujibu wa kanuni za Bunge adhabu yake ni kuvuliwa / kufukizwa bungeni.

Katika kikao hicho ambacho kiliitishwa haraka mara baada ya uamuzi wa Spika pia kilihudhuriwa na Mkuu wa JWTZ mstaafu General Mirisho ambaye pia alipongeza uamuzi huo wa Spika.

Kwa wadhifa wake nadhani hakutakiwa kujihushisha na siasa nyepesi nyepesi.

Najiuliza Nassari akienda Mahakamani na kuonekana alionewa General Mirisho atauweka wapi uso wake.CDF ni wadhifa mzito sana,sijawahi kuona au kusikia General Waitara au General Musuguri wakitajwa tajwa katika mambo ya ajabu ajabu.

Mbaya zaidi kikao chenyewe kilikuwa kimetamalakiwa na wanaCCM waliovalia kofia na fulana za Chama.

Naomba kuwasilisha kwa unyenyekevu wa viwango vya kimataifa.

Ngongo mgombea ubunge mtarajiwa Arumeru Mashariki kwa tiketi ya CUF ya Propesa Lipumba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuja kurealise Tanzania Ina watu wanafiki sana haswa wana ccm ubongo wao wameeanika. Juwani mtu alikuwa mkuu wa majeshi anaingia kwenye propaganda hivi kwa nini wana mkweza Magufuli kwa kuvuruga demokrasia kwa ajili ya matumbo yao
 
Utoro ni kukosa nidhamu ;

Nasari kawatusi wana arumeru mashariki wote kwa kukataa wajibu waliompa kwa heshima..

Ameamua kufanya mambo binafsi akaachana na dhamana ya wengi..
 
Aisee huyu Sarakikya hapa chini naye atoe maelezo vizur
images (38).jpeg
images (39).jpeg
images (40).jpeg
 
CCM kwenye madarska wanakua kitu cha ajabu...awamu hii wamezibisha kuliletea aibu taifa..
 
Mkuu nimeangalia post yako namba moja nimebaki nacheka tu. Unamshangaa huyo CDF mstaafu tena ni mwanakijiji naona kama unamuonea tu. Sasa hivi CDF aliye madarakani alikaa kimya rais akipokea madiwani waliohamia ccm katika hafla ya kijeshi huko Arusha, tukio hilo likiwa mubashara mbele ya taifa zima, itakua huko kichochoroni kwa wazee wa kishili? Jeshi limetengwa kabisa na siasa kikatiba na CDF alikuwa kimya jeshi likinajisiwa itakuwa huyo CDF mstaafu?


5/5
 
Utoro ni kukosa nidhamu ;

Nasari kawatusi wana arumeru mashariki wote kwa kukataa wajibu waliompa kwa heshima..

Ameamua kufanya mambo binafsi akaachana na dhamana ya wengi..

Spika kaweka mpira kwapani.
 
Back
Top Bottom