CDF ni wadhifa mzito sana
HATUNA statesmen.
Mkuu wa majeshi sio mtu mzito kuliko Rais Mstaafu Mwinyi, Mkapa na Kikwete
Sio mzito kuliko Waziri wa Ulinzi na Waziri Mkuu Mstaafu Salim Ahmed Salim, na Pinda na Malecela, Msuya na Lowassa.
Sio mzito kuliko Jaji Mkuu Mstaafu Ramadhani, Samatta, Othman na Spika Msekwa na Makinda. Na wale wakurugenzi Usalama, ma kleptocrat wakubwa wa nchi hii.
Wote hao hakuna stateman, mtu anaesimama wima bila woga kutetea misingi na nguzo zinazoshikilia nchi hii.
Jana ripoti ya haki za binafamu imetoka, dunia imeorodheresha katalogi la machafuchafu ya Tanzania, wanasiasa na wananchi waliopigwa mapanga, waliopotezwa, waliofungwa mahabusu miaka 5, 10, waliopigwa risasi, waliotupwa baharini, waliotiwa umaskini, walioshitakiwa, waliofirigiswa kwa kila namna.
Wastaafu wetu wamekaa miguu juu, aloof as door knobs, wanaogopa kunyang'anywa mashamba, landcruiser la serikali na dereva na mwaliko wa Mkutano Mkuu CCM kila miaka mitano. Wanajiuza kwa vitu vidogo, vidogo,vidogo, vidogooooo. Na baadhi vikubwa kama kupelekwa kutibiwa India bure kwa kodi zetu, vitu ambavyo wananchi wao tunaishi na kufa without. Na bado hawatutetei.
Spineless, shameless, selfish African kleptocrats.