Nimempiga mwizi mapanga mawili ya kichwa, akifa Mungu nisamehe

Kitoabu

JF-Expert Member
Jul 7, 2011
10,332
10,946
Mungu anajua sijawahi liua jitu hata siku moja lakini ikitokea lile jamaa likafa shauri yake na familia yake.

Mwaka jana nimeibiwa mara mbili nikahama mtaa.

Wiki iliyopita nimemkosa kidogo tu, ashukuru niliamka usingizini nikiwa na pombe kichwani na kupelekea kupiga kelele akasepa zake. Leo sasa kajikanyaga, asipokufa basi majeraha ya kichwa atayauguza mpaka tutakapo kutana motoni, jinga sana.

Ilikuwa hivi, nimerudi zangu mihangaikoni mida ya jioni kama saa kumi na moja.

Kwa uchovu wa kazi niliokuwa nao (kuchimba jamani sio sawa na kutia sign kwenye makaratasi) nikaamua kuoga na kujipumzisha kidogo, kutokana na uchovu, usingizi ukanipitia na kujikuta nimeamka mida ya tano usiku.

Kwakuwa mida ilishakuwa imeenda na watu walishalala nikaamua wacha itoke tu mpaka kesho.

Lakini kila nilipojaribu tena kulala usingizi ulikuwa haupatikani, nikaamua kutoa simu yangu, cha kwanza nikampigia mke wangu kujua hali zao yeye na watoto, nilipomaliza mazungumzo nikaingia mjengoni (JF) kupata kujua kinachoendelea duniani.

Kipindi naendelea na charting zangu, mara nasikia mtu kama anapushi mlango, nilitulia kidogo, eeh sindio naona kitasa kinavunjwa, hapo nikaifunika simu chini fasta ili asiuone mwanga wa simu, nikainuka na panga langu nikatulia pembezoni na mlango, kwamba akifungua mlango awe amenificha na ule mlango.

Kama aliingia ndani ya akili yangu, jamaa kafosi mpaka akafanikiwa, alivyoingia ndani (mkononi ana nondo) yeye akawa mbele mimi niko nyuma yake na ndani kiza hakuniona.

Mungu anisamehe, nikapeleka la kwanza, sikutaka kungoja fasta nikapeleka la pili mchizi chini kwenye sakafu, alipiga kelele moja tu ya mamaa khinakwa (kwa kimakua maana yake mama nakufa).

Nahisi nje kulikuwa na mwenzie akimpigia saiti mila, maana nilisikia vishindo vya mtu akikimbia.

Nilichofanya niliokota nondo yake na kuishika mkoni, mara jirani yangu tunaekaa chumba jirani akaamka na kuja chumbani kwangu, nikawasha taa, jamaa kafloti analia kwa sauti ya mbali.

Mpangaji mwenzangu nae ni mchimbaji kama mimi, tukashauriana tumbebe tukamtupe nje. Tukalibeba msobe msobe mpaka nje jirani na mitaa hii, tukalitupia huko.

Uzuri wa maeneo haya (mgodini) kila mtu anaangalia lake, hakuna hata alietoka nje, kushabikia.

Hapa nimemaliza kufuta damu chumbani kwangu, na sidhani leo kama nitalala.

Maduka kama yangekuwa hayajafungwa ilibidi nipate kikali (pombe kali) ili kutoa mawenge kichwani.

Akipona safi, akifa shauri yake.
 
Back
Top Bottom