Pac-Man
JF-Expert Member
- Oct 18, 2016
- 465
- 737
Habari za Jumapili wapendwa..
Leo nimeenda kanisani kama kawaida yangu, ikabidi nikae siti za kati kati kabisa ya kanisa. Sasa sisters wa kanisa wawili wakaja wakaketi sit ya mbele yangu, Ibada ikaanza.
Sio kwamba nilikuwa sifatilizi ibada, lakini unaweza ukawa hata umesimama barabarani magari yanapita huyashangai. Ila kuna gari moja linaweza pita ukajikuta umeanza kulitazama hadi likatokomea.
Kwenye ibada kuna kusimama, kupiga magoti, na kukaa.
Yule sister bhana kwenye kukaa, anaangalia sehem anapoketi (kwenye dawati) anavuta nguo yake kwa heshima anaketi. (Mda huo akiwa anafanya hivyo hadi na kasura kake unakaona [nusu face] anapovuta nguo yake ili aketi)
Mh nikajikuta nimemtazama (Mungu asikunyime macho. Macho yanatazama vizuri na vibaya). Kizuri kisifie …yule sister bhana ni mzuri. Ni mzuri wote kwa muonekano hadi anavyo jishugulisha na ibada.
Kijana wa watu nikapotelewa na utulivu wa ibada, nikajikuta kila anaporudi kukaa, nikawa nayaruhusu macho yafurahie uzuri na ustaarabu wa yule sister.
Najua wanaume tukipendaga kitu kuanzia tunapo kiangalia huwa tuna tabia ya kukifikisha kwenye ubongo na ubongo kukipangilia kitu hicho kinastahili vipi, yani kama ni kiwanja tunaonaga hadi nyumba imekamilika na kuisha.
Ibada ikaendelea tukamaliza salama. Wakati natoka nje, sister naye akawa amefika zam yake akanifuata nyuma, tukatoka nje.
Wakati tunashuka ngazi za nje ya kanisa kuna mama gauni lake kilikuwa refu linaburuza chini, nikajikuta nimelikanyaga mguu wa kwanza ile naendelea kushuka ngazi pasipo kujua nmekangaga nguo, mguu wa pili nikajikwaa kwa lile gauni.
Ile naelekea kuanguka kwenda chini. Paap! Nikasikia mtu amenidaka mkono kuzuia nisianguke.
Kutazama nyuma ni sister.
Mama mwenye gauni refu: Samahani kijana poleh!
Mimi: Asante ….. Samahani mama.
Sister: Taratibu kijana poleh
Mimi: Asante sana Sister
Sister: Uwe na Amani.
Sister akaniachia mkono, nikageuka vizuri nimtazame huku nikimjibu Amen sister.
Yule sister ni mzuri nyie.
Sister akanyoosha mkono kuelekeza njia..haya twende 🫱
HIVI KUMPENDA SISTER NI DHAMBI?
Leo nimeenda kanisani kama kawaida yangu, ikabidi nikae siti za kati kati kabisa ya kanisa. Sasa sisters wa kanisa wawili wakaja wakaketi sit ya mbele yangu, Ibada ikaanza.
Sio kwamba nilikuwa sifatilizi ibada, lakini unaweza ukawa hata umesimama barabarani magari yanapita huyashangai. Ila kuna gari moja linaweza pita ukajikuta umeanza kulitazama hadi likatokomea.
Kwenye ibada kuna kusimama, kupiga magoti, na kukaa.
Yule sister bhana kwenye kukaa, anaangalia sehem anapoketi (kwenye dawati) anavuta nguo yake kwa heshima anaketi. (Mda huo akiwa anafanya hivyo hadi na kasura kake unakaona [nusu face] anapovuta nguo yake ili aketi)
Mh nikajikuta nimemtazama (Mungu asikunyime macho. Macho yanatazama vizuri na vibaya). Kizuri kisifie …yule sister bhana ni mzuri. Ni mzuri wote kwa muonekano hadi anavyo jishugulisha na ibada.
Kijana wa watu nikapotelewa na utulivu wa ibada, nikajikuta kila anaporudi kukaa, nikawa nayaruhusu macho yafurahie uzuri na ustaarabu wa yule sister.
Najua wanaume tukipendaga kitu kuanzia tunapo kiangalia huwa tuna tabia ya kukifikisha kwenye ubongo na ubongo kukipangilia kitu hicho kinastahili vipi, yani kama ni kiwanja tunaonaga hadi nyumba imekamilika na kuisha.
Ibada ikaendelea tukamaliza salama. Wakati natoka nje, sister naye akawa amefika zam yake akanifuata nyuma, tukatoka nje.
Wakati tunashuka ngazi za nje ya kanisa kuna mama gauni lake kilikuwa refu linaburuza chini, nikajikuta nimelikanyaga mguu wa kwanza ile naendelea kushuka ngazi pasipo kujua nmekangaga nguo, mguu wa pili nikajikwaa kwa lile gauni.
Ile naelekea kuanguka kwenda chini. Paap! Nikasikia mtu amenidaka mkono kuzuia nisianguke.
Kutazama nyuma ni sister.
Mama mwenye gauni refu: Samahani kijana poleh!
Mimi: Asante ….. Samahani mama.
Sister: Taratibu kijana poleh
Mimi: Asante sana Sister
Sister: Uwe na Amani.
Sister akaniachia mkono, nikageuka vizuri nimtazame huku nikimjibu Amen sister.
Yule sister ni mzuri nyie.
Sister akanyoosha mkono kuelekeza njia..haya twende 🫱
HIVI KUMPENDA SISTER NI DHAMBI?