My dear pole sana tena sana, i knw how it feels, haya mambo yapo saana, me nimeshayasikia kwa mtu zaidi ya mmoja, ila nnachotaka kukwambia katika hayo yote, wewe sali sana tena mmmno najua kuna wakati utasikia kuchoka na kuona pengine Mungu hakusikii ila hiyo ni sauti ya shetani wewe endelea kuomba tu, hakuna aombae akakosa kupokea Mungu ni wa Rehema sana na Neema hatakuacha haijalishi muda gani utapita, Muombe Mungu sana akupe amani, akupe upendo kwa mama yako, na aifungue nafsi ya mama yako, pia na nafsi yako iwe huru na akuepushe namaroho hasa ya kukataliwa, pale unapohisi uchungu umezidi sana mpaka kuwaza mabaya juu mama yako siku isiishe hujatubu ili hiyo dhambi isiote mizizi mana kutokana na situation yako ukiicha hiyo mizizi iote hutaweza kuing'oa. Nakwambia hivyo kwasababu madhara ya situation unayopitia wewe ni makubwa mno, bila kumtegemea Mungu, hali hiyo huleta sana roho za kukataliwa, utajikuta kila mtu unaona hakupendi na wewe pia hutakuwa na upendo katika jamii, utaishi maisha ya kutengwa na kujitenga, na wakati wote utakuwa mtu mwenye uchungu na hasira, utaishi bila amani maisha yako yooote, hakuna utakapoenda au utakaekaa nae kwa amani utakuwa ni mtu wa kuhisi unaonewa wakati wote, usietaka hata kukoselewa hata kama kweli umekosea utakuwa ukiambiwa tu unapanic na kujenga chuki hata ndoa inaweza ikushinde. Kwahiyo mtegemee sana Mungu saaana na muombe sana akuepushe na hiyo roho ya kukataliwa mana kutokana na situation yako haichezi mbali na wewe.