Nimemchoka sana mama yangu

Nimemchoka sana mama yangu

Umesema uliwahi kubakwa ukiwa angali 7 year old......hii bila shaka imekuletea tatizo kwasababu kama ulishindwa kusema kwa mlezi wako itakuwa uliendelea kuficha mambo mengi yaliyotokea baadae...inawezekana huyo aliyekubaka alifanya hivyo zaidi ya mara moja, mara mbili?........hii imekutengenezea hali ya "kuvumilia" mambo maovu katika maisha yako. Unajua ukiwa mtu wa kunungunika tu kwasababu huna namna ya kufanya......na hali hiyo ikaendelea muda mrefu unakuwa huna "mvuto" ni kama vile una-atract mambo mabaya yaje kwako. Ngumu kuelezea.....ila unahitaji kuacha kuwa LEGELEGE kimtazamo......none but ourselves can free our minds......hakuna atakayeweza kukutoa hapo......tafuta kazi, ukipata jaribu kuwa STRONG kwa huyo mama yako na wote wanaokuzunguka. Sisemi uwe strong udharau watu, ugombane na watu.....no....namaanisha usikaribu ku-please watu hata kama ni familia yako. Life is very short usipoteze time.
nilifanyiwa kitendo hicho Mara moja nikawa silali tena labda tuwe wengi chumban.na form one nikaanza kukaa kwa mama..kazi natafta na mimi siyo legelege
 
Mpendwa lady Jay.., Hebu acha kuwa mwizi wa fadhila, huyo ni mama yako alikubeba miezi 9 na akakusomesha hadi kufikia hapo !! Wewe hujui madhila na shida alizopambana nazo huko nyuma !!

Yaani hata ufanyejee huwezi mlipa au kulinganisha fadhila zake !!! So be polite na umtii na kuhakikisha apate mwisho mwema..... !!!
(kama kukaripiwa /kutukanwa/kusimangwa wingi mbona wamepitia)
 
My dear pole sana tena sana, i knw how it feels, haya mambo yapo saana, me nimeshayasikia kwa mtu zaidi ya mmoja, ila nnachotaka kukwambia katika hayo yote, wewe sali sana tena mmmno najua kuna wakati utasikia kuchoka na kuona pengine Mungu hakusikii ila hiyo ni sauti ya shetani wewe endelea kuomba tu, hakuna aombae akakosa kupokea Mungu ni wa Rehema sana na Neema hatakuacha haijalishi muda gani utapita, Muombe Mungu sana akupe amani, akupe upendo kwa mama yako, na aifungue nafsi ya mama yako, pia na nafsi yako iwe huru na akuepushe namaroho hasa ya kukataliwa, pale unapohisi uchungu umezidi sana mpaka kuwaza mabaya juu mama yako siku isiishe hujatubu ili hiyo dhambi isiote mizizi mana kutokana na situation yako ukiicha hiyo mizizi iote hutaweza kuing'oa. Nakwambia hivyo kwasababu madhara ya situation unayopitia wewe ni makubwa mno, bila kumtegemea Mungu, hali hiyo huleta sana roho za kukataliwa, utajikuta kila mtu unaona hakupendi na wewe pia hutakuwa na upendo katika jamii, utaishi maisha ya kutengwa na kujitenga, na wakati wote utakuwa mtu mwenye uchungu na hasira, utaishi bila amani maisha yako yooote, hakuna utakapoenda au utakaekaa nae kwa amani utakuwa ni mtu wa kuhisi unaonewa wakati wote, usietaka hata kukoselewa hata kama kweli umekosea utakuwa ukiambiwa tu unapanic na kujenga chuki hata ndoa inaweza ikushinde. Kwahiyo mtegemee sana Mungu saaana na muombe sana akuepushe na hiyo roho ya kukataliwa mana kutokana na situation yako haichezi mbali na wewe.
You nailed it Mrs ake.

Cha kwanza lady hana budi kumsamehe mama ake Kwa yote. Anapitia na atapitia magumu mengi na mama yake, but hana budi kumsamehe kama anataka aishi kwa amani. Hatujui nini kilitokea, but inawezekana mama yake ni mtu aliyeweka uchungu mkubwa moyoni, unfortunately uchungu huo anaumalizia kwa mtoto. Kuna kitu possibly kinachomuumiza kwenye yale mahusiano na baba mtoto, na hajawahi kukiachilia moyoni mwake wala kumove on. Maumivu yote anayahamishia kwa mtoto, siku akija kuyaachilia utashangaa atakavyoumia na kujuta juu ya yote anayokufanyia. Muombee mama ako, possibly anachokifanya ni out of her control, muombe Mungu aingilie kati.

Inaumiza mnoo, but mchukulie mama ako kama udhaifu wako, kama jaribu lako ambalo huwezi kumtupia mtu mwingine. Muombe Mungu akupe hekima ya kuishi na mama ako, na kila siku muombee mama ako akauachilie huo uchungu

Above all, kemea roho ya kukataliwa, kama alivyosema mrsleo. Muombe Mungu akupe kibali mbele zake na mbele ya wanadamu. Hutokataliwa tena, hutochukiwa tena, utakubalika popote pale utakapokuwa na utakapoingia. Mungu akutie nguvu na akutetee katika hili
 
nilifanyiwa kitendo hicho Mara moja nikawa silali tena labda tuwe wengi chumban.na form one nikaanza kukaa kwa mama..kazi natafta na mimi siyo legelege
Sawa, basi endelea kutafuta kazi umuepuke huyo mama yako anayekuchukia. Watu wanasema huyo ni mama yako huna jinsi.....mimi nakwambia usipoteze muda kwa mtu asiyekupenda.....hata kama ni mzazi. Haijalishi alifanya nini kikubwa angali ukiwa mdogo.....kwani wewe uliomba uje duniani? Kwahiyo kukulea kwa upendo jukumu lake.

Jambo lingine, usikae nyumbani unasema unatafuta kazi, toka nenda kafanye kazi kwenye mashirika kwa kujitolea, nenda kaongee na watu.....tena umesema wewe si legelege? Ukiwa smart utapata sehemu ya kufanya kazi hata week haitaisha.
 
You nailed it Mrs ake.

Cha kwanza lady hana budi kumsamehe mama ake Kwa yote. Anapitia na atapitia magumu mengi na mama yake, but hana budi kumsamehe kama anataka aishi kwa amani. Hatujui nini kilitokea, but inawezekana mama yake ni mtu aliyeweka uchungu mkubwa moyoni, unfortunately uchungu huo anaumalizia kwa mtoto. Kuna kitu possibly kinachomuumiza kwenye yale mahusiano na baba mtoto, na hajawahi kukiachilia moyoni mwake wala kumove on. Maumivu yote anayahamishia kwa mtoto, siku akija kuyaachilia utashangaa atakavyoumia na kujuta juu ya yote anayokufanyia. Muombee mama ako, possibly anachokifanya ni out of her control, muombe Mungu aingilie kati.

Inaumiza mnoo, but mchukulie mama ako kama udhaifu wako, kama jaribu lako ambalo huwezi kumtupia mtu mwingine. Muombe Mungu akupe hekima ya kuishi na mama ako, na kila siku muombee mama ako akauachilie huo uchungu

Above all, kemea roho ya kukataliwa, kama alivyosema mrsleo. Muombe Mungu akupe kibali mbele zake na mbele ya wanadamu. Hutokataliwa tena, hutochukiwa tena, utakubalika popote pale utakapokuwa na utakapoingia. Mungu akutie nguvu na akutetee katika hili
asante
 
Pole sana, jitahidi kutafuta kazi kwa bidii kubwa nadhani hata humu kuna kazi huwa zinawekwa humu jaribu kuapply usichoke na ukifanikiwa kaa mbali kabisa na mama yako kwa kuhakikisha mnakutana mara chache sana hasa kukiwa na ulazima wa kufanya hivyo. Inawezekana mama yako mdogo labda hakuwa mkweli kwako labda huyu si mama yako mzazi au alikupata katika njia ambayo hakuipenda hivyo chuki na hasira zake ya kitendo alichofanyiwa imehamia kwako. Pole sana.
 
Habari zenu wapendwa,

Mimi ni msichana niliyemaliza chuo lakini natafuta kazi. Naishi na wazazi wangu na wadogo zangu wa kike ambao nawapenda sana. Nimekulia na kulelewa na bibi sana na mama mdgo ambao wote walikua wapole na wakarimu ila mama mdogo alitangulia mbele ya haki.

Nilimpenda sana mamdogo kuliko mama yangu mzazi kwasababu alinipenda na kuchukua nafasi ya mzazi wangu na ndiye aliyeniambia mume wake mama siyo baba yangu mzazi ( ila ni baba yao wadogo zangu ) nikiwa darasa la sita.
Niliumia sana kwasababu mama yangu alikuwa hana time kabisa kunieleza hayo. Hapo form one ndo nikaanza kuishi na mama yangu ila jamani ni mkali kwangu adi naliaga. Kuna siku nilimuuliza mama mdgo kama huyu kweli ni mama yangu mzazi au la akasema ndo mamako.

My mum hana ukaribu na mimi, ananifokea kila wakati bila hata sababu. Hanaga shukrani in anything i do. Uzuri darasani nilikua nafanya vzuri sana nikishuka position kidgo atafoka likizo nzima. Nilikua nashika nafasi ya nne nikiwa naongoza wasichana ila nikiwa tu wa tano ataongea likizo nzima.

Anavyokuwa ananiangalia, utafikiri yeye ndo mama yangu wa kambo hata akipiga honi ya gari getini nikiwa tu nje nilikua nakimbilia chooni. Anyway namshukuru kwasababu yeye ndo aliyenisomesha. (japo ni wajibu wake).

Tatizo ni pale mama anavyokuwa hana mother to daughter love au affection. Hajali what I do. Naweza kumuomba hela anakuwa mkali mpaka namwambia basi mama natafuta njia napata na haulizi ila wadogo zangu wanapewa hata extra. Mimi sijawahi kununuliwa simu na mama ila wao wananunuliwa tena mimi ndo namsindikizaga mama kununua na haniulizi mimi napata wapi simu.

Nikitaka tuongee labda angalau nimwambie kitu kinachonisumbua au just kupata faraja ya mama anaongea kwa ukali kwamba kachoka au bwanae ondoka ila roho inaniumaga. Marafiki zangu wanavyoongelea mama zao huwa nawatazama na kuwatamani.

Nyumbani kuna mfanyakazi lakini kazi zote nafanya mimi na mama humtetea dada na kusema mimi sina umuhimu ndani wakati kutwa nzima mimi ndo najishughulisha ila nakaaga kimya hadi nikiwa chuo nikija kusalimia huwa hataki niondoke ili nifanye kazi. Nikimwambia mama nina test atasema bwanae kwani wewe wa kwanza kusoma mpaka nakosa raha nikiwa chuo nakuwaga very lonely na mawazo. Sikufanikiwa kupata mkopo wala hela ya matumizi hvyo nilikua nahudumiwa na mama. Aisee sitokuja kusahau mateso niliyopata chuo.

Nimelala hungry nights mpaka ilibidi nizoee. Hapo ndo nikaona nitakufa nikaanza mahusiano na wanaume kisa nipate hela. Hapo mama uwezo anao wakunisaidia lakini anasema hana hela nitafute wanaume tena kwa ukali.

Anyway nilipunguza ukaribu na mama hata upendo kwasababu nilijaribu kuwa karibu nae nipate mapenzi ya mama lakini nikashindwa. Afu yeye ndo anasema nina roho mbaya, sina upendo kama wadogo zangu. Ninamwangalia tu kwasababu najua yeye ndo hanipendi. Na anasema hivyo kwasababu anawasikiliza sana yuko karibu nao but she pushes me away yaani utafikiri niliokotwa.

Kuna wakati huwa natamani niolewe ila ndoa ina majanga yake pia na sina hata mtu. Na hali ya mama imenifanya nikose upendo kwa watu wengne niponipo tu all alone. Kuna wakati nakaa tu na kulia na kinachoniuma nikiwa 7 yrs nilishawahi kubakwa kijijini kwa bibi na mfanyakazi ila sijawahi kumwambia mama wala mtu yeyote.

Watu watakua wanajiuliza mbona sitaji baba. Baba yangu ana familia yake mkoani na alishasahau kama ana mtoto. Baba yangu wa kambo yupoyupo tu but sana sana anawajali wanae ila hainiumizi roho. Ninachomuomba Mungu niondoke nipate kazi hata mkoani mbali na mama yangu.

NB. Wazazi wa hivi especially wamama jaribu kuweni karibu na watoto wenu kuweni na upendo. Mimi siwezi elezea kila kitu hapa ila umuhimu wa mamangu ni kunisomesha tu tena kwa maneno namshukuru sana kwa hilo.

Wapendwa sjui mtanisaidiaje but nimevumilia sana ni mama yangu huyo ndo maana wengne hukimbia kwao au kutaka ndoa haraka ili waondoke makwao.

Wazazi badilikeni tafadhali.


Pole sana Lady J.
Vumilia umalize masomo yako. Jitunze, uwe Mcha Mungu na baadae utafanikiwa na kuwa nguzo ya kutegemewa katika familia yako. Hakuna lisilokuwa na mwisho. Mtegemee Mwenyezi Mungu utafanikiwa.
Amin.
 
Pole sana Lady J.
Vumilia umalize masomo yako. Jitunze, uwe Mcha Mungu na baadae utafanikiwa na kuwa nguzo ya kutegemewa katika familia yako. Hakuna lisilokuwa na mwisho. Mtegemee Mwenyezi Mungu utafanikiwa.
Amin.
Asante
 
sio wazazi badilikeni wewe ndo ubadilike km ulikua unalala na wanaume bila kinga siku za htr uache yaan kwakifupi ujitambue mambo yanayotokea kati yako ww na mama ako ni matokeo ya mama yako kupewa mimba bila plan yeyote matokeo yake katelekezwa na baba yako usikute na ww unfanana na baba yako bas mihasira yote unapewa...aliyekuambia huyo sio baba ako nae mpuuzi tu ulipaswa kujua badae sn mnk baba ako hakujali uwepo wako...matokeo yake ht ukifeli unataka uchekewe kisa mama yako...ni ujinga huo....mama kutokukupenda ni mihasira yake ya mistakes zake za ujana ambzo ww inabidi ujifunze zisikutokee...si mara zote mara nyingine ht ww unakosea kwahy lzm uzinguliwe kwan wewe nani usisemwe?tafuta kazi kaa nae mbali mpe nfs heshima irudi khs kumchukia ni upuuzi wako mwenywe wa kutojua binadamu si mkamilifu....sikushangai ukikua utaacha...mama ako akikosea jifunze kutokana na makosa yake othrwise ni ngumu
 
sio wazazi badilikeni wewe ndo ubadilike km ulikua unalala na wanaume bila kinga siku za htr uache yaan kwakifupi ujitambue mambo yanayotokea kati yako ww na mama ako ni matokeo ya mama yako kupewa mimba bila plan yeyote matokeo yake katelekezwa na baba yako usikute na ww unfanana na baba yako bas mihasira yote unapewa...aliyekuambia huyo sio baba ako nae mpuuzi tu ulipaswa kujua badae sn mnk baba ako hakujali uwepo wako...matokeo yake ht ukifeli unataka uchekewe kisa mama yako...ni ujinga huo....mama kutokukupenda ni mihasira yake ya mistakes zake za ujana ambzo ww inabidi ujifunze zisikutokee...si mara zote mara nyingine ht ww unakosea kwahy lzm uzinguliwe kwan wewe nani usisemwe?tafuta kazi kaa nae mbali mpe nfs heshima irudi khs kumchukia ni upuuzi wako mwenywe wa kutojua binadamu si mkamilifu....sikushangai ukikua utaacha...mama ako akikosea jifunze kutokana na makosa yake othrwise ni ngumu
sawa nimekuelewa ila sijawahi kufeli.pili silalamiki kusemwa nikoseapo tena nakiri kosa na kuomba msamaha na simchukii mamangu ni upendo tu hupungua kwasababu hana upendo kwangu kabisa na naona hivi tangu udogoni
 
Kuna jambo alilotendwa na Baba yako likamuumiza sasa wewe ndio umekuwa pa kulipia kisasi.
Msamehe ila kama kuna watu wazima anaowaheshimu jaribu kuongea nao ili wamwite na kumuonya! Ingawa hatofurahishwa na wewe kutoa siri yake lakini itakuwa dawa na ataacha kukunyanyasa kwa Uwezo wa Mungu.
 
Mm, kweli mama ni mama tu. Pole sana, ila huyo mama yako kama kuna siku itafika mungu angemfunulia na kukumbuka kwamba wewe ni mtoto, tena na kwamba wewe hukutuma application ili akuzae. Ni wajibu wake kama mzazi kukupa mapenzi. Ni excuse ipi huyo mama atakuwa nayo yakutokukupenda. Mama yako anahitaji msaada wa kisakologia!! Jipige moyo konde na wewe utakuwa na maisha yako. Mwenyezi mungu atakusimamia na kukuguta machozi. Ninarudia tena: mama yako anapashwa kusaidiwa. And girl, you are a brave one, you have made it up to now. Stop crying, just pull up your socks as you have done: maisha mazuri yanakusubiri. Things pass: remember that. Sure, you will make it. Ku share hili tatizo lako na sisi: iwe therapy kwako. Afadhari umefunguka, tangu sasa just look forward, umuangalie mama yako kwenye miwani ya mbao. Na tena usitafute mume kama ndiyo solution ya maisha yako (wanaume nao ni kazi) NO. Rafiki sawa wa kupeana naye mawazo, TIME WILL TELL. Wishing you, all the best!!
 
Mm, kweli mama ni mama tu. Pole sana, ila huyo mama yako kama kuna siku itafika mungu angemfunulia na kukumbuka kwamba wewe ni mtoto, tena na kwamba wewe hukutuma application ili akuzae. Ni wajibu wake kama mzazi kukupa mapenzi. Ni excuse ipi huyo mama atakuwa nayo yakutokukupenda. Mama yako anahitaji msaada wa kisakologia!! Jipige moyo konde na wewe utakuwa na maisha yako. Mwenyezi mungu atakusimamia na kukuguta machozi. Ninarudia tena: mama yako anapashwa kusaidiwa. And girl, you are a brave one, you have made it up to now. Stop crying, just pull up your socks as you have done: maisha mazuri yanakusubiri. Things pass: remember that. Sure, you will make it. Ku share hili tatizo lako na sisi: iwe therapy kwako. Afadhari umefunguka, tangu sasa just look forward, umuangalie mama yako kwenye miwani ya mbao. Na tena usitafute mume kama ndiyo solution ya maisha yako (wanaume nao ni kazi) NO. Rafiki sawa wa kupeana naye mawazo, TIME WILL TELL. Wishing you, all the best!!
asante sana
 
Sasa bi mdashi kama huyo wa kazi gani????

Huyo dawa yake ni kumlia timing kwenye kona ya ukuta na kumkwida Nondo ya bichwa! Aendee akaanzishe ubabe wake huko kuzimu!!
 
Pole sana, Inahuzunisha sana.
Ni bora hata angekuwa ameshafariki ujue moja, Kinachouma zaidi ni kufanyia yote hayo na mama yako mzazi, Mtu ambaye ulipaswa uwe karibu katika nyakati zote maishani.

Kama mama anakufanyia hivyo ni nani zaidi unayeweza kumdekea na akakufariji unapopata matatizo dunia hii.

Inahuzunisha sana,
Inatia hasira sana,

Nini Ufanye?
Mtii kuanzia sasa bila manung'uniko, Fanya kile anachokihitaji kwa ubora au Mara mbili zaidi ya matarajio yake.


Ni kitu kigumu lakini jitahidi kufanya bila kulalamika, Wakati unafanya yote jitahidi kujenga mazoea mazuri na watu hasa was mtaani kwenu huku ukimuomba Mungu.

Naamini baada ya muda, mabadiliko utayaona, Mabadiliko hayo yaweza kuwa ni kwa wewe kupata kazi au mama yako kukuhurumia.

Every Problem has a solution.
 
usijali dada jikaze ndo maisha hayo ipo siku yataisha tu cha muhimu komaa katika kitabu na Mungu pia basi.
 
Habari zenu wapendwa,

Mimi ni msichana niliyemaliza chuo lakini natafuta kazi. Naishi na wazazi wangu na wadogo zangu wa kike ambao nawapenda sana. Nimekulia na kulelewa na bibi sana na mama mdgo ambao wote walikua wapole na wakarimu ila mama mdogo alitangulia mbele ya haki.

Nilimpenda sana mamdogo kuliko mama yangu mzazi kwasababu alinipenda na kuchukua nafasi ya mzazi wangu na ndiye aliyeniambia mume wake mama siyo baba yangu mzazi ( ila ni baba yao wadogo zangu ) nikiwa darasa la sita.
Niliumia sana kwasababu mama yangu alikuwa hana time kabisa kunieleza hayo. Hapo form one ndo nikaanza kuishi na mama yangu ila jamani ni mkali kwangu adi naliaga. Kuna siku nilimuuliza mama mdgo kama huyu kweli ni mama yangu mzazi au la akasema ndo mamako.

My mum hana ukaribu na mimi, ananifokea kila wakati bila hata sababu. Hanaga shukrani in anything i do. Uzuri darasani nilikua nafanya vzuri sana nikishuka position kidgo atafoka likizo nzima. Nilikua nashika nafasi ya nne nikiwa naongoza wasichana ila nikiwa tu wa tano ataongea likizo nzima.

Anavyokuwa ananiangalia, utafikiri yeye ndo mama yangu wa kambo hata akipiga honi ya gari getini nikiwa tu nje nilikua nakimbilia chooni. Anyway namshukuru kwasababu yeye ndo aliyenisomesha. (japo ni wajibu wake).

Tatizo ni pale mama anavyokuwa hana mother to daughter love au affection. Hajali what I do. Naweza kumuomba hela anakuwa mkali mpaka namwambia basi mama natafuta njia napata na haulizi ila wadogo zangu wanapewa hata extra. Mimi sijawahi kununuliwa simu na mama ila wao wananunuliwa tena mimi ndo namsindikizaga mama kununua na haniulizi mimi napata wapi simu.

Nikitaka tuongee labda angalau nimwambie kitu kinachonisumbua au just kupata faraja ya mama anaongea kwa ukali kwamba kachoka au bwanae ondoka ila roho inaniumaga. Marafiki zangu wanavyoongelea mama zao huwa nawatazama na kuwatamani.

Nyumbani kuna mfanyakazi lakini kazi zote nafanya mimi na mama humtetea dada na kusema mimi sina umuhimu ndani wakati kutwa nzima mimi ndo najishughulisha ila nakaaga kimya hadi nikiwa chuo nikija kusalimia huwa hataki niondoke ili nifanye kazi. Nikimwambia mama nina test atasema bwanae kwani wewe wa kwanza kusoma mpaka nakosa raha nikiwa chuo nakuwaga very lonely na mawazo. Sikufanikiwa kupata mkopo wala hela ya matumizi hvyo nilikua nahudumiwa na mama. Aisee sitokuja kusahau mateso niliyopata chuo.

Nimelala hungry nights mpaka ilibidi nizoee. Hapo ndo nikaona nitakufa nikaanza mahusiano na wanaume kisa nipate hela. Hapo mama uwezo anao wakunisaidia lakini anasema hana hela nitafute wanaume tena kwa ukali.

Anyway nilipunguza ukaribu na mama hata upendo kwasababu nilijaribu kuwa karibu nae nipate mapenzi ya mama lakini nikashindwa. Afu yeye ndo anasema nina roho mbaya, sina upendo kama wadogo zangu. Ninamwangalia tu kwasababu najua yeye ndo hanipendi. Na anasema hivyo kwasababu anawasikiliza sana yuko karibu nao but she pushes me away yaani utafikiri niliokotwa.

Kuna wakati huwa natamani niolewe ila ndoa ina majanga yake pia na sina hata mtu. Na hali ya mama imenifanya nikose upendo kwa watu wengne niponipo tu all alone. Kuna wakati nakaa tu na kulia na kinachoniuma nikiwa 7 yrs nilishawahi kubakwa kijijini kwa bibi na mfanyakazi ila sijawahi kumwambia mama wala mtu yeyote.

Watu watakua wanajiuliza mbona sitaji baba. Baba yangu ana familia yake mkoani na alishasahau kama ana mtoto. Baba yangu wa kambo yupoyupo tu but sana sana anawajali wanae ila hainiumizi roho. Ninachomuomba Mungu niondoke nipate kazi hata mkoani mbali na mama yangu.

NB. Wazazi wa hivi especially wamama jaribu kuweni karibu na watoto wenu kuweni na upendo. Mimi siwezi elezea kila kitu hapa ila umuhimu wa mamangu ni kunisomesha tu tena kwa maneno namshukuru sana kwa hilo.

Wapendwa sjui mtanisaidiaje but nimevumilia sana ni mama yangu huyo ndo maana wengne hukimbia kwao au kutaka ndoa haraka ili waondoke makwao.

Wazazi badilikeni tafadhali.

WW LAZIMA UWE WIFE MATERIAL UKIINGIA KWENYE NDOA SIO SIRI NATAFUTA WATU WA HIVI, WALIOPITIA CHANGAMOTO, HAKUNA LINALOSABABISHWA WASUMBUA SIO WABINYA SAUTI WENGINE HUKO MTAANI
 
Back
Top Bottom