Kwa Sasa wanapambana na ukame sijui kama watakukumbukaHabari za muda huu,
Jamani ninaomba kuuliza, tulifanya process za kuomba umeme tangu mwezi wa saba mwaka huu, na tuliwatumia wakandarasi wa hapo hapo tanesco kutujazia na kutuchorea na kurudisha form tanesco Tanga Mjini.
Sasa siku hiyo hiyo alikuja mtu wa kufanya survey na akapima pima pale na kikubwa kilichotakiwa ni nguzo, tukakaa tukisubiri kuitwa kwenda kulipia nguzo iwekwe umeme uingie, tulisubiri mno kwenye mwez wa tisa nikapigiwa sim kama nilishapimiwa nikajieleza tayar wakanambia niende eneo husika niwaelekeze wao wanakuja, nikafika tukaelekezana wakaja wakapima tena baada ya hapo hicho kimya chake skukielewa ikabidi mimi nifunge safar mpaka hapo ofisini kwao.
Nikaomba kuonana na mtu wa kulitatua tatizo langu nikaonana na mama mmoja hivi hata usoni hakuangalii na jibu akataka tu namba na jina la form nikampa akanijibu ukiona tanesco wamekita nguzo kwenye hilo eneo ndio uje.
Nimesubiri kwa muda mrefu mnooo naomba kufahamishwa tatizo ni nini najua wahusika wapo humu nikimpigia yule mkandarasi majibu ni kama hayo sasa sielewi tangu mwezi wa saba had sasa naona zii.
simkumbuki jina wala sura yake na sjui nampatajehii nchi rushwa haaishi kamwe.......fuatilia control number kwa yule survey....mshikishe kiduchu....huyo ndie anaeweza kupush upate control number......then huyo huyo anaweza maliza mchezo..........achana na manager au vikaragosi wengine....surveyor ndo sterling....
sasa shida inakuja nimtafte nani huyo mpimaji hata skukumbuka kumtafta teena mkandaras ndio ninaongea naye hivo naskilizia mana hata leo nimemtafta kasema atanipa majibu bado nasubiriNkono Ntupu haulambwi, mnadharau misemo ya wahenga? endelea kusubiri
hao nilishawachek pm nikawapa na details wakanijibu nisubiri foleni bado na nguzo ni mojapost kwenye UZI wa special thread wa tanesco kuna jamaa aipost alilalamika miezi nguzo iliangukia kwake hawajabadilisha kila akipiga simu kesho kesho baada kupost akaambiwa atume details Pm siku tatu akaja na mrejesho wamebadilisha nguzo
so km ni zile nguzo mbili au moja kuja kwako nina uhakika ukipost utapata suluhu ya halaka jaribu
Kwa kawaida ni wasumbufu, bila kuwasumbua, unaweza sahaulika mazima, ila pia wanao muda wa kumhudumia mteja kulingana na mazingira ya mteja husika, kama unahitaji nguzo, au hauhitaji muda unatofautiana.process zimeanza mwez wa saba mwaka huu akiwa magu ameshafariki umesoma lakini kwa umakini
yan nimeona nikikaa kimya mimi ndio nna shida nipo tayar hata hiyo hela kutoa ngoja niendelee kupambana naoKwa kawaida ni wasumbufu, bila kuwasumbua, unaweza sahaulika mazima, ila pia wanao muda wa kumhudumia mteja kulingana na mazingira ya mteja husika, kama unahitaji nguzo, au hauhitaji muda unatofautiana.
thanks ngoja niwatafuteNAMBA ZETU
0717/ 0788 379696
MALENGO
1.Kusogeza huduma karibu na wewe
2.Kutoa njia mbadala ya wewe kutupatia taarifa.
3.Kutoa njia mbadala kwa sisi kukupatia taarifa na elimu dhidi ya bidhaa,taratibu na huduma zetu.
4.Kujenga uhusiano mzuri baina yako na TANESCO
TAHADHARI
-Tutumie lugha yenye staha na heshima kwa wote
ziko busy hizo my friendNAMBA ZETU
0717/ 0788 379696
MALENGO
1.Kusogeza huduma karibu na wewe
2.Kutoa njia mbadala ya wewe kutupatia taarifa.
3.Kutoa njia mbadala kwa sisi kukupatia taarifa na elimu dhidi ya bidhaa,taratibu na huduma zetu.
4.Kujenga uhusiano mzuri baina yako na TANESCO
TAHADHARI
-Tutumie lugha yenye staha na heshima kwa wote