Mazingira huwa yanawabadilisha. Upambanaji plus upatikanaji wa fursa za kujiingizia kipato kwa urahisi inawafanya kuondokana na roho za kibongo za kwann.
Maana akikupa wewe chochote ana uhakika atapata tena mara mbili yake so haina shida.
Kibongo bongo mtu anaweza kuwa na milioni kwenye akiba ukaomba akuazime 20,000 akipiga hesabu namna kaipata ile milioni anaona hapana, hatoweza kuichenji kwaajiri yako wacha tu asikupe kama ni dhambi MUNGU atasamehe.
Umasikini huwa unawafanya watu kuwa na tabia za ajabu sana kama ushirikina, uchoyo, ubinafsi, kubania wengine, kuchukia wengine bila kukosewa lolote, wivu, ghubu, etec.
Ndio maana babu yetu Nyerere alitusihi sana kuwa tuupige vita sana umasikini kwa maana huwa unaleta matatizo mengi sana.